MILIONI 850 ZATOLEWA MKOPO NA SACCOS YA MSHIKAMANO MPWAPWA



Na Noel  Stephen Mpwapwa
Jumla ya shilingi milioni 815,000.000/zimetolewa kwa wananachama wapatao 800  wa Chama cha Ushirika Akiba  na mikopo  Saccos ya Mshikamano Baraza cha Mjini MPWAPWA.

 Hayo yamebainishwa na meneja wa wa  Saccos hiyo  Bi  YOKEBEDY PANGAWE alipo kuwa akiongea na waandishi wa habari    jana ofisini kwake.

 Bi Pangawe alisema kuwa chama hicho tangu kianzishwe mwaka  2003 hakijaweza kutoa mikopo  ya kiasi kikubwa  namana hiyo kwa wanachama wake ambapo wanachama hao wameweza kubadilisha maisha na kuongeza kipato cha familia na jamii inayo wazunguka ,

Aidha Bi Pangawe  aliongezea kuwa mikopo iliyo tolewa ni  kwa wanachama hao ni mkopo ya  kilimo ambayo inaghrimu kiasi cha shilingi milioni 350,000,000/ na mikopo ya bishara ni milioni 450,000,000/ na mikopo ya dharula ilitolewa mikpo ya kiasi cha shilingi milioni 15,000,000/-.

Pia  Bi Pangawe alisema kuwa mbali na kutoa mikopo hiyo kwa wanachama wake  lakini wapo baadhi ya wanachama kuto kuitumia mikopo waliyo iomba kwa  malengo yaleyale na kuhamisha matumizi ya mkopo kitu alicho kisema kuwa  kina wapelekea kuingia matatani na mteja wakati wa ulipaji.

Na alidai kuwa wanachama  wajenge moyo wa kusoma mikataba  kabla ya  kujaza fomu ya  mikopo  ili waweze kuelewa  taratibu  na kanuni za mikopo  ili kupunguza mikwaruzano  wakati wa malejesho ukifika au kwa   mteja akishidwa kulejesha au  anapo chukuliwa dhamana zake.

Tena Bi  Pangawe aliwataka akina mama wengi waweze kujitokeza katika kuomba mikopo  amabapo alisema kuwa kwa sasa idadi kubwa ya  wanao chukua mikopo mikubwa n ni wanaume tofauti na akina mama ambao wao huchukua mikopo  ya biashara ndogondogo ambazo haziwaletei tija akina mama wengi hapa nchini.

Alisema kuwa  kwa sasa chama hicho kina wanachama wapatao 1483   na  chama hicho kwa sasa kinauwezo wa kutoa mkopo wa shilingi  milioni 8,000,000/ kwa mala moja kwa mwana chama tofauti na hapo awali amabapo walikuwa na uwezo wa kutoa shilingi 200,000/ laki mbili tu kwa mwanachma anae omba mkopo.

Comments

Popular posts from this blog

DC KIZIGO ATOA MAAGIZO KWA KWA MAAFISA ELIMU KUKABILIANA NA UKATILI MASHULENI.

HISTORIA YA MPWAPWA HATARINI KUTOWEKA

KIZIGO AWAPONGEZA RUWASA,AKERWA NA UHARIBIFU WA MAZINGIRA,AWATAJA MADIWANI.