Posts

Showing posts from May, 2023

DC KIZIGO ATOA MAAGIZO KWA KWA MAAFISA ELIMU KUKABILIANA NA UKATILI MASHULENI.

Image
  Mkuu wa wilaya ya Mpwapwa Bi Sophia Kizigo akifungua kikao   cha wadau wa Ulinzi dhidi ya Mtoto na ukatili wa kijinsia kilicho wezeshwa na Jukwaa la utu wa Mtoto CDF wilayani Mpwapwa.   Mkurugenzi Mtendaji wa  Shirika la utu wa Mtoto CDF Koshuma Mtengeti akichangia jambo  katika kikao cha kujadili ulinzi wa Mtoto wilayani Mpwapwa.   Stephen Noel-Mpwapwa.   Mkuu wa wilaya ya Mpwapwa Mkoani Dodoma Bi Sophia Mfaume Kizigo ametoa  amri kwa maafisa Elimu wote ndani ya wilaya hiyo kuhakikisha shule zote za Msingi na sekondari zinakuwa na walimu walezi kwa lengo la kupunguza vitendo vya ukatili kwa watoto wawapo shuleni. Mkuu wa wilaya hiyo ametoa agizo hilo kwenye mkutano wa Siku moja uliondaliwa na Asasi ya kiraia jukwaa la utu wa mtoto  CDF  iliyo kutanisha Wadau wote wanao fanya  afua za kumlinda mtoto na kujali ustawi wa mtoto. Amesema Ili kuhakikisha watoto wanakuwa Kwenye mazingira ya usalama lazima kunakuwapo na  watu wanao ratibu  kero zinazo wakabili watoto au pindi wafanyiwapo uk