Posts

Showing posts from 2017

MAJI KIKWAZO CHA MAENDELEO IDILO WILAYA YA MPWAPWA

New post el-Mpwapwa Wakazi  wa kijiji cha Idilo kata ya Mazae wilayani  Mpwapwa mkoani hutumia maji yasiyo salama  na kutishia kupata magonjwa ya mlipuko hasa kipindi hiki kuelekea msimu huu wa mvua za vuli. Maji hayo yanayopatika  umbali km 2 hadi 3 kwa  pia ni maji ya makorongoni ambayo  ni hatari kwa afya za wakazi hao. Diwani wa kata hiyo  bwana Wiliam Vahae   amesema  wakazi hao hulazimika kuamka alfajili na mapema ili kuwahi maji katika kisima kabla hayajachafuliwa na wanyama  wa polini lakini kabla ya wafugaji hawajanza kunywesha  Ng,ombe ambao wanakuwa na makundi makubwa ya mifugo. Aidha Vahae amesema kutokana na hali hiyo  kumepelekea wakazi wa kijiji hicho kutumia maji ya visima vya asili na makorongo ambayo si safi na salama na kutishia magonjwa ya mlipuko kama kipindupindi. Amesema kufutia tatizo hilo tayari wakazi wa kijiji hicho wamesha changa kiasi cha shilingi million 450,000/=ambazo ziko benki kwaajili ya kusubiri nguvu ya serikali katika mradi

WAJUMBE WA MKUTANO MKUU UWT WAAONYWA DODOMA.

WAJUMBE wa mkutano mkuu wa uchaguzi wa  Umoja wa Wanawake (UWT) Mkoa wa Dodoma wameaswa kuchagua viongozi makini na imara watakaokifanya chama kiendelee kuwa imara kutokana na  mkoa huo kuwa makao makuu ya Chama. Pia amewataka wana CCM kupendana,kupunguza figisu,visasi,majungu,porojo na kuwa ili kufikia maengo ni lazima wanyanyuane na kuinuana kwa lngo la kumfanya kila mmoja atimize yale aliyoyapanga kwa msaada mkubwa wa mwanamke. Rai hiyo imetolewa leo mjini Dodoma na mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) mkoa wa Dodoma Alhaj Kimbisa wakati akifungua mkutano huo ambapo amesema CCM nyumbani kwake ni Dodoma hivyo viongozi watakaochaguliwa lazima watambue hilo kwa kulinda heshima isipotee. Aidha amewaasa kutochagua viongozi wenye harufu ya rushwa bali wachague viongozi watakaokuwa wepesi wa kuwaunganisha akina na watakaoifanya jumuiya ijitegemee kiuchumi. Mkutano huo umehudhuriwa na wajumbe 473  ambapo miongoni mwa nafasi zinazogombewa ni nafasi ya uenyekiti UW

WAZIRI ATAKA CHANGAMOTO ZA MAJI KUISHA VIJIJINI

Waziri wa maji na Umwagiliaji Mhandisi Izack Kamwelwe amesema katika kukabiliana na kero ya upatikanaji wa huduma ya maji wilayani Kongwa mkoani Dodoma serikali imetenga zaidi ya shilingi milioni 600 kwa ajili ya miradi ya maji wilayamo hiyo. Wilaya ya Kongwa ni miongoni mwa wilaya kongwe zilizopo makao makuu ya nchi Dodoma licha ya ukongwe wa wilaya hiyo bado wananchi wake wanateseka kutafuta huduma ya maji na kulazimika kutembea umbali mrefu kutafuta huduma hiyo muhimu. Hali hiyo inamlazimu Waziri wa maji na umwagiliaji Mhandisi Izack Kamwelwe anafanya ziara wilayani humo na kutoa matumaini mapya kwa wananchi katika kutatua tatizo hilo sugu na kuahidi serikali itamaliza tatizo la upatikanaji wa huduma hiyo ndani ya muda mfupi. Mhandisi Izack Kamwelwe Waziri wa maji na umwagiliaji Deo Ndejembi ni mkuu wa wilaya ya Kongwa mkoani Dodoma akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara amesema kuwa atahakikisha anasimamia ujenzi wa miradi ya maji ili wananchi waweze k

KOROSHO ITAGEUZA UCHUMI WA DODOMA

WAKULIMA  wa Mkoa wa Dodoma wameshauriwa kujikita katika ulimaji wa zao la korosho kwani zao hilo lina faida kubwa kibiashara tofauti na yalivyo mazao mengine.  Korosho ni moja ya mazao makuu ya biashara nchini. Kwa sasa zao hili hulimwa zaidi mikoa ya Kusini mwa Tanzania, yaani Lindi na Mtwara ikifuatiwa na Mkoa wa Ruvuma, Pwani na Tanga. Takwimu kutoka Bodi ya Korosho Tanzania (CBT) zinathibitisha umuhimu wa zao hilo kwa Taifa, ambapo katika msimu wa 2012/13 zao hilo liliiingizia Serikali kiasi cha Sh bilioni 29.5 kutokana na ushuru wa usafirishaji wa korosho ghafi nje ya nchi. Akizungumza wakati wa ziara yake katika baadhi ya wilaya za mkoa huo  Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dr.Binilith Mahenge ameeleza kuwa utafiti umefanywa na kubaini ardhi ya Dodoma inafaa kwa uzalishaji wa zao hilo. Akitoa taarifa ya wilaya kwa Mkuu wa Mkoa,Mkuu wa wilaya ya Kondoa Sezaria Makota amesema wilaya yake imeanza kuwa na mkakati wa zao la korosho kama zao la biashara na hadi sasa wa

WALIMU WAOMBA KUBORESHEWA MAZINGIRA MPWAPWA

MKUU wa wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma Bwana Jabil Shekimweri amewataka waajili kuto kuzalisha madeni Malta kwa wafanya kazi wakati serikali ipo kwenye mkakati mkubwa wa kulipa madeni kwa walimu. Mkuu wa wilaya huyo aliyasema hayo juzi alipo kuwa akifungua mkutano mkuu wa chama cha walimu wilayani hapo kwa mwaka 2017. Shakimweri alisema kuwa Tanzania ikiwa inajiandaa kuingia katika uchumi wa viwanda lazima kuwekeza katika Elimu ili kuweza kupata wataalamu watakao hudumu katika viwanda hivyo kwa mstakabali Tanzania mpya. "Tunapo zungumzia Tanzania ya Viwanda lazima tuwaze juu ya wahudumu katika viwanda hivyo lazima tuwajibike kutoa wanafunzi walio makini watakao fiti katika utaalamu wa viwanda" aliongea Shakimweri. Aidha Shakimweri ameendelea kuvipigia kelele vitendo vya utovu wa nidhamu kwa baadhi ya walimu wanaojihusisha na mapenzi na wanafunzi, V walimu kumamatwa na vitendo vya rushwa na uwizi. Pia Mkuu wa wilaya huyo aliwata walimu hao kujihus

SERIKALI YATOA TAMKO KUHUSU TAHADHARI ZA MVUA.

SERIKALI imetoa tahadhari ya mvua zinazoendelea kunyesha katika maeneo mbalimbali nchini huku ikielekeza wananchi kutumia fursa chanya za mvua hizo kwa shughuli za maendeleo kama kilimo kwa ajili ya kupanda mazao yanayohitaji maji. Mbali na kilimo pia wananchi wametakiwa kutumia mvua hizo kuandaa mabwawa na malambo kwa ajili ya uvunaji wa maji .    Tahadhari hiyo imetolewa leo mjini Dodoma na naibu waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu Sera, Bunge, kazi, ajira,vijana na watu wenye ulemavu Stella Alex wakati akizungumza na waandishi wa habari. Amesema kuwa kamati za usimamizi wa maafa kuanzia ngazi ya kijiji na mtaa zinatakiwa kutekeleza majukumu yake kwa mujibu wa sheria ya usimamizi wa maafa NO.7 ya mwaka 2015 na kanuni za usimamizi wa maafa za mwaka 2017. Amesema kuwa septemba 4 mwaka huu Mamlaka ya hali ya hewa Tanzania ilitoa utabiri wa msimu wa mvua za vuli kwa kipindi cha mwezi Octoba mpaka disemba mwaka huu kwa maeneo yanayopata misimu miwili ya mvua na kuonyesh

UKATILI WA KINJISIA UWEKEWE MKAKATI MADHUBUTI

SERIKALI ya Mkoa wa Dodoma imewataka wakurugenzi wa wilaya zote ndani ya mkoa ,sekretarieti ya mkoa pamoja na watendaji wengine katika ngazi zote kutekeleza kwa vitendo majukumu yote waliyopangiwa kwa mujibu wa mpango wa kitaifa wa kutokomeza  ukatili dhidi ya wanawake na watoto. Maagizo hayo yametolewa hii leo na kaimu mkuuwa mkoa wa dodoma ambaye pia ni mkuu wa Wilaya ya Chamwino Vumilia Nyamoga wakati wa ufunzguzi wa maadimisho ya siku kumi na sita za kupinga ukatili dhidi ya wananwake na watoto ambapo mbali na hayo pia ametoa magizo kwa maafisa maendeleo na ustawi wa jamii huku akisistiza kuwa maagizo hayo yatafatiliwa kwa kadri itakavyotakiwa. Aidha pia Nyamoga amesema wananchi wengi wamekuwa wakiwatoa malalamiko  watendaji wa vijiji na kata kujihusiha na vitendo vya rushwa jambo ambalo linadidimiza jitihada za kutokomeza ukatili dhidi ya wananwake na watoto jambo ambalo kwa mkoa wa dodoma halikubaliki. Kwa upande wake mwakilishi wa katibu mkuu  wizara ya afya ma

AHUKUMIWA MIAKA 60 JELA KWA KUBAKA WATOTO WA MIAKA 9 NA 12

MAHAKAMA ya hakimu makazi wilayani Mpwapwa mkoani Dodoma imemuhukumu kifongo cha miaka 60 jela na kupigwa viboko kumi na mbili Bwana Aloyce Hela (45)  mkaz wa Mwanakianga baada ya kupatikana na hatia ya ubakaji. Kesi hiyo iliyo kuwa inasikilizwa na hakimu mkazi wa mahakama hiyo Bwana Pascal Mayumba ambapo ilivuta hisia za wakazi wa Mpwapwa na watetezi wa haki za watoto wilayani hapa. Bwana Mayumba ameiiambia mahakama kuwa mtuhumiwa alitenda kosa hilo katika tarehe Tofauti kuanzia mwaka 2015 hadi Sasa ambapo alikuwa akiwabaka watoto wawili wa miaka (9)na miaka (12) wanafunzi wa Darasa la pili na la kwanza katika moja wapo wa shule wilayani hapa. Mayumba amesema mtuhumiwa alifanya kosa kinyume na kifungu cha sheria 130na 131 kifungu kidogo cha kwanza cha kanuni ya adhabu iliyo fanyiwa malejeo mwaka 2002. Aidha Mayumba ameambia mahakama kuwa mtuhumiwa huyo alikuwa alifanya kosa hilo zaidi ya mala mbili na kuwapa watoto hao shilling 200 na alikuwa anafanya katika chum

ZAIDI YA BILIONI 15 ZINAHITAJIKA KUKAMILISHA JENGO LA RC DODOMA.

ZAIDI ya Sh.Bilioni 15 zinahitajika ili kukamilisha ujenzi wa jengo la Mkuu wa mkoa wa Dodoma ambalo linatarajiwa kuwa ni ofisi ya Rais na Makamu wa Rais ambapo ujenzi huo kwa sasa umefikia asilimia 56. Akizungumza wakati wa ziara ya mkuu wa mkoa wa dodoma Dk.Binilith Mahenge wakati wa ukaguzi ujenzi wa jengo hilo Msanifu wa majengo wa kampuni ya (CRJE) Peter Kibushi amesema fedha hizo sh. bil 15.9 za awamu ya tano pindi zitakapotolewa zitakamilisha ujenzi huo. Akisoma taarifa ya ujenzi huo, Msanifu huyo amesema ujenzi wa jengo hilo ulianza Juni 2009 na utagharimu zaidi ya Sh.Bilioni 25 ambapo hadi sasa fedha zilizotolewa ni takribani Sh.Bilioni 12. Naye Mhandisi Mshauri wa ujenzi huo, Titus Tesha amesema wamelazimika kujenga kwa awamu kutokana na mtiririko wa fedha kuwa mdogo na hivyo kupanga kazi kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha. Akizungumzia kuhusu utoaji wa fedha kwa ajili ya jengo hilo, Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma Deogratias Yinza amese

MKURUGENZI MPWAPWA AITAKA JAMII KUHAMASIKA KATIKA MAENDELEO.

SHULE ya Msingi Mngangu   wilayani Mpwapwa mkoani Dodoma inakabiliwa   uhaba wa matundu ya vyoo   hali hiyo inapelekea   kuwapo kwa mazingira magumu kwa walimu na wanafunzi kwa   ya kujifunzia na kusomea. Mwenyekiti wa kijiji   hicho   bwana    Sospiter   Nyaombo   amesema kufutia hali hiyo bwana jamii wakajihamasisha na kujenga matundu ya   kumi mbili ya vyoo vitakavyo ondoa adha     kwa wanafunzi kulundikana vyooni wakati wa mapumziko . Bwana Nyaombo amesema “mpaka sasa kupitia nguvu za wananchi   tumesha   jenga matundu kumi na mbili ya    vyoo ambayo yatapunguza adha ya matundu ya vyoo   shuleni hapo lakini kwa kutambua majukumu yetu tumesha chukua hatua ya kuwaondolea kadhia hiyo watoto wetu ili wasome katika mazingira rafiki na hatimae kukuza kiwango cha ufaulu shuleni hapa.”aliongea Bwana Nyaombo. Aidha mwenyekiti wa   kamti ya shule hiyo bwana   Sajilo Nuhu amesema shule hiyo yenye wanafunzi   461 lakini ina matundundu   nane tu ya vyoo yanasababisha mlindik

UMASKINI WA KIPATO CHANZO CHA MIMBA ZA UTOTONI-.CDF

EELEZWA kuwa umaskini wa kipato ni mojawapo ya sababu kuu inayo chochea kuwapo kwa mimba za utotoni katika jamii. Kauli hiyo imebainishwa na mkurugenzi mtendaji wa shirika la Jukwaa la Utu wa mtoto (CDF) Bwana Koshuma Mtengeti katika warsha ya siku moja ya kutambulisha mradi na shirika hilo kwa wadau. Bwana Mtengeti alisema kutokana na utafiti iliyo fanywa na shirika hilo kwa kusaidiana na mashirika mengine walibaini kuwa umaskini wa familia hupelekea familia zenye maisha Mara nyingi Zina pambana kutafuta chakula na mavazi kwa ajili ya watoto wao. Aidha Mtengeti alisema kuwa alisema kuwa kwa mujibu wa utafiti wa demografia ya Afya Tanzania wa 2016 (TDHS) zilionyesha kwamba asilimia 36%ya wasichana wenye umri wa Kati ya 20-24 waliolewa kabla ya kufikia umri wa miaka 18. Pia Mkurugenz Mtengeti alisema kuwa Pia utafiti huo ulibaini kuwa asilimia 50%ya ndoa za utotoni inahusisha wanaume ambao ni wakubwa kwa umri wa miaka 5-hadi 14 huoa watoto hao na kusababisha wanawake

Picha na matukio

Image
Mkuu wa wilaya ya Mpwapwa Jabiri Shekimweri akikagua kazi zilizo fanywa na Mikiwa ni ofisi ya mtendaji wa kata.

MATUKIO KATIKA PICHA MAFUNZO YA MGAMBO LUKOLE.

Image
Mkuu wa wilaya ya mpwapwa asema askari mgambo wasaidie mapambano ya uharibifu wa mazingira Mpwapwa. Mgambo wakisikiliza maelekezo.

DC WATAKA MGAMBO KUZITUMIA FURSA KUJILETEA MAENDELEO

Image
WANANCHI wa wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma wametakiwa kuzitambua fursa zinazopatikana katika wilaya hiyo ili kuweza kujiletea maendeleo kuliko kubaki kulalamika. Shakimweri aliyasema hayo Jana alipo kuwa akifunga mafunzo ya Mgambo katika Kata ya Lukole kwa mwaka 2017 Shakimweri alisema kuwa kwa Sasa wilaya ya Mpwapwa ni miongoni zenye fursa nyingi za kimaendeleo Lakin changamoto inayo wakabili wakazi wake ni kuto kuzitambua fursa zilizopo au kuendelea kuishi kimazoea na kubaki kulalamika.  Mkuu wa wilaya ya Mpwapwa bwana Jabiri shakimweri akiongea na mgambo hawapo pichani. Alisema wilaya ya Mpwapwa ni wilaya iliyo zungukwa tasisi nyingi za kielimu kama tasisi ya utafiti wa mifugo, TARILI, chuo cha Mawakala wa Mifugo Lita, chuo cha ualimu na chuo cha Maafisa afya na Mazingira lakini maisha ya wakazi wengi wamekuwa hayaashilii uwepo wa tasisi hizo. Hata hivyo mkuu wa wilaya hiyo aliwataka vijana waliohitimu mafunzo ya Mgambo kuweza kuisaidia wilaya katika kusima

MAAFISA MAENDELEO TIMIZENI WAJIBU WENU-WAZIRI WA AFYA.

WAZIRI wa Afya Maendeleo ya Jamii,Jinsia ,Wazee na Watoto Ummy Mwalimu amewataka Maafisa Maendeleo ya Jamii wote kutekeleza wajibu wao wa msingi kwa kuhakikisha watoto wanalindwa dhidi ya vitendo vya ukatili wakiwa shule na nje ya shule. Taarifa ya utafiti wa hali ya afya ya uzazi ,mtoto na malaria ya mwaka 2015/2016 inaonyesha kuwa asilimia 27 ya watoto wakike wanapata mimba wakiwa na umri chini ya umri wa miaka 18.. Tatizo hili lipo zaidi mikoa ya Katavi (asilimia 45),Tabora (asilimia 43),Dodoma (asilimia 39), Morogoro (asilimia 39) na mkoa wa mara (asilimia 37) Akizungumza leo mjini Dodoma wakati wa ufunguzi wa Mkutano mkuu wa 12 wa sekta ya maendeleo ya jamii Waziri Ummy amesema kuwa kupitia mkutano huo maafisa maendeleo ya jamii amesema kuwa kupitia mkutano huo maafisa maendeleo ya majii wanatakiwa wanatoka na mikakati madhubuti ya kudhibiti vitendo vya ukatili katika jamii. Naye Katibu Mkuu Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Sihaba Nkinga amesema ku

WAKUU WA MIKOA WAPEWA CHANGAMOTO .JAFFO

Waziri wa nchi ofisi ya Rais Tawala za mikoa na serikali za mitaa TAMISEMI Selemani Jaffo amewaagiza wakuu wa mikoa nchini kuhakikisha wanaandaa miundombinu ya elimu ya kutosha katika mikoa yao ili wanafunzi waliofaulu mtihani wa darasa la saba na kupata nafasi ya kujiunga na kidato cha kwanza january 2018 wanapata nafasi hiyo. Akizungumza mjini dodoma Waziri wa Tamisemi Seleman Jaffo amesema kufuatia kuongezeka kwa ufaulu wa  asilimia 72.76 kwa wanafunzi waliofaulu mtihani wa darasa la saba ofisi yake haina budi kutoa maelekezo hayo ili maandalizi yaweze kufanyika mapema. Kuhusiana na kushuka kwa Somo la kingereza Waziri Jafo anatoa maelekezo. Katika hatia nyingine Waziri Jaffo amewataka makatibu tawala wa mikoa na wakurugenzi wahalmashauri zote nchini kuwapokea watumishi 2058 wa sekta ya afya ambao wamepangiwa vituovya kazi  kwa kuwapatia stahiki zao. Watumishi waliopangwa wanatakiwa kuripoti katika vituo vyao vya kazi ndani ya siku 14 MWISHO.

AKINA MAMA WAJIFUNGULIA MAJUMBANI BAHI.

AKINA mama wajawazito wapata 47 katika kata ya mpalanga Wilaya ya Bahi Mkoani Dodoma wametajwa kujifungulia nyumbani katika kipindi cha kuanzia mwezi july hadi septemba mwaka huu jambo linalohatarisha maisha ya mama na mtoto. Zipo sababu mbalimbali ambazo zinatajwa kupelekea akina mama wajawazito kutojifungulia katika zahanati na vituo vya afya ikiwa ni pamoja ni huduma hiyo kukosekana katika baadhi ya vijiji,miundombinu kutokuwa rafiki na pengine kupelekea akana mama hao hujifungulia njiani. akisoma taarifa ya utekelezaji wa shughuli za maendeleo katika kikao cha baraza la madiwani wa halmashsuri hiyo cha robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2017/18, diwani wa kata hiyo Daudi Magalamile amesema kuwa sababu hizo zimekuwa ni changamoto katika maeneo yao. Diwani huyo amesema hapo awali kulikuwa na utaratibu wa kuwatoza faini akina ambao wanajifungulia nyumba ambao utaratibu huo uliwafanya akina mama hao kujifungulia katika vituo vya afya na zah

NAIBU WAZIRI WA MAJI ATEMBELEA MIRADI YA MAJI MPWAPWA.

Image
Mkuu wa wilaya ya Mpwapwa  Jabir Shekimweriakitoa taarifa ya upatikanaji wa juduma za maji katika mji wa mpwapwa. Naibu waziri wa maji na umwagiliaji Bwana JUMA AWESO akikagua mitambo ya maji katika wilaya ya Mpwapwa.

JAMII YAFICHA TAARIFA ZA UKATILI.

MTANDAO wa polisi wanawake wilayani Mpwapwa mkoani Dodoma umesema kasi ya ukatili kwa watoto inasababishwa na jamii kuficha taarifa za vitendo hivyo. Kauli hiyo ilitolewa na mkuu wa dawati lá njisia katika kituo cha polisi wilayani hapa Bi Elfrida Mapunda katika maadhimisho ya miaka kumi ya kuanzishwa kwa dawati hilo. Bi Mapunda amesema kuwa vitendo vya ukatili vinavyodhidi kushika kasi vinasababishwa na jamii kuzidi kuvifumbia macho vitendo hivyo au kamalizana kienyeji bila kufuata sheria na bila kuangalia madhara. Aidha Bi Mapunda ameitaka jamii kwa kusaidiana na jeshi lá polisi kuweza kushirikiana katika kukomesha vitendo vya ukatili kwa watoto na wanawake. Pia amesema katika kuadhimisha miaka kumi tangu kuanzishwa kwa mtandao huo kumeongezeka kwa taarifa za ukatili ambazo hapo awali zilikuwa zinafichwa kutolewa. Kwa upande wake mkurugenzi mtendaji wa kituo hicho bi Selina Chimwaga amesema kuwa kuwa kundi kubwa lá watoto hao wenye mtindio wa ubongo wanakabiliwa na chan

DC MPWAPWA AWAHADHARISHA WAKULIMA PWAGA.

Mkuu wa wilaya ya mpwapwa mkoani Dodoma  bwana Jabiri Shakimweri  amewataka wananchi  wa vijiji vya Pwaga na Mingui  kuto kuuza ardhi kiholela hasa katika kipindi hiki cha ujio wa serikali mkoani Dodoma Shakimweri aliyasema hayo juzi alipokuwa akifungua mafunzo ya  kwa wakulima wa vijiji vya pwaga  na Mingui wilayani Mpwapwa yaliyofadhiliwa na Mpango wa kurasimisha rasilimali na biashara za wanyonge  (MKURABITA) juu ya kuweza kuitumia ardhi kama  rasilimali muhimu kwa maendeleo ya mtu mmoja mmoja na  Taifa kwa ujumla. Aidha Shakimweri amesema kuwa mala baada ya serikali kuanza kuhamia Dodoma kumeibuka baadhi ya watu  wanao zunguka katika wilaya zote za mkoa Dodoma  kununua maeneo ya watu kwa bei nafuu  na kuwaacha  wakazi wa maeneo hayo  katika hali ya umaskini  na kutishia kuwapo katika  mogohoro ya ardhi. Mkuu wa wilaya hiyo amesema lazima wanannchi hao  kuweza kutumia fursa za  hati za kimila za ardhi  kwa kuweza kuongeza dhamani ya ardhi  kwa kupanda mazao ya biashara y

MADWANI MPWAPWA WALIA NA SHERIA ZA MADINI.

Image
BARAZA la madiwani katika halmasahauri ya wilaya ya Mpwapwa limeiomba ofisi ya ofisa madini mkazi Dodoma  kuweza kuwajengea uwezo madiwani hao  na wadau wanaofanya kazi za madini  katika halmashauri hiyo  ikiwa ni mkakati wa kukuza mapato ya ndani ya halmasahauri hiyo. Akisoma taarifa  ya utekelezaji  wa kamati ya fedha  uongozi  na mipango katika kipindi cha  mwezi julai  hadi septemba 2017 diwani wa kata ya Lumuma bwana Jocktan Cheliga amesema kuwa pamoja na  wilaya ya Mpwapwa kuzungukwa na neema ya madini ya aina tofauti tofauti  lakini wameshidwa kufaidika na rasilimali hiyo kutokana na madiwani wengi kuto kujua taratibu za upatikanaji wa mirahaba  ya madini katika maeneo husika. Diwani wa kata ya Mazae bwana wiliamu Vahae akichangia mjadala katika kikao cha madiwani Mpwapwa. Mwenyekiti wa halmashauri hiyo bwana Donart Ngwezi amesema kuwa lazima kuwepo  na ushirikiano  wa pamoja  kati  ya ofisa madini mkazi  wa Dodoma kuweza kuwapa semina juu ya kuweza kusimamia 

WATANZANIA5 KATI YA 13 WALIO FIA UGANDA WAZIKWA MPWAPWA.

Image
Miili ikiwasili Makaburini. Miili ya marehemu ikishushwa Makabulini.