Posts

Showing posts from September, 2017

MADWANI MPWAPWA WALIA NA SHERIA ZA MADINI.

Image
BARAZA la madiwani katika halmasahauri ya wilaya ya Mpwapwa limeiomba ofisi ya ofisa madini mkazi Dodoma  kuweza kuwajengea uwezo madiwani hao  na wadau wanaofanya kazi za madini  katika halmashauri hiyo  ikiwa ni mkakati wa kukuza mapato ya ndani ya halmasahauri hiyo. Akisoma taarifa  ya utekelezaji  wa kamati ya fedha  uongozi  na mipango katika kipindi cha  mwezi julai  hadi septemba 2017 diwani wa kata ya Lumuma bwana Jocktan Cheliga amesema kuwa pamoja na  wilaya ya Mpwapwa kuzungukwa na neema ya madini ya aina tofauti tofauti  lakini wameshidwa kufaidika na rasilimali hiyo kutokana na madiwani wengi kuto kujua taratibu za upatikanaji wa mirahaba  ya madini katika maeneo husika. Diwani wa kata ya Mazae bwana wiliamu Vahae akichangia mjadala katika kikao cha madiwani Mpwapwa. Mwenyekiti wa halmashauri hiyo bwana Donart Ngwezi amesema kuwa lazima kuwepo  na ushirikiano  wa pamoja  kati  ya ofisa madini mkazi  wa Dodoma kuweza kuwapa semina juu ya kuweza kusimamia 

WATANZANIA5 KATI YA 13 WALIO FIA UGANDA WAZIKWA MPWAPWA.

Image
Miili ikiwasili Makaburini. Miili ya marehemu ikishushwa Makabulini.

WAZIRI WA JK APATA PIGO AFIWA NA NDUGU 13 KWA MPIGO,MPWAPWA YAZIZIMA.

Image
Na Stephen Noel-Mpwapwa. WATANZANIA 13( kumi na watatu) wamefariki dunia nchini Uganda   walikokuwa wameenda kwenye harusi   ya binti yao baada ya gari gari lao kugongana   na loli karibu na mto   Katonga barabara ya Masaka   usiku wa kuamkia   tarehe 18septemba mwaka huu . Gari hilo lenye namba T 540 DLC   mali ya Gregory Teu lilikuwa likuwarudisha Wanzania wa familia yake, walio wakirudi Tanzania kutokea Uganda, Teu aliyekuwa mbunge wa jimbo la Mpwapwa mstafu na naibu waziri wa Viwanda na Biasharakatika serikali ya awamu ya nne bwana Gregory Teu. Kwa mujibu wa   taarifa kutoka katika ofisi ya ubalozi wa Tanzania nchini Uganda zinasema   watanzania hao walikwenda nchini humo tangu tarehe 16 septemba mwaka huu kwa ajili ya   harusi ya   mtoto wake   bwana Gregory   Teu Mkazi wa Dar es salaam nchini Tanzania aliye olewa nchini Uganda . Aidha taarifa hizo zinasema   gari hiyo ilikuwa na abilia 19 ambapo abilia 13 walifariki papo hapo na wengine sita kujeruhiwa    na kukimbizw

DC PANGANI AWAOMBA VIONGOZI WA DINI KUWAOMBEA.

Image
. Mkuu wa wilaya ya Pangani mkoani Tanga Bi Zainabu Abdalah   amewataka viongozi wa Dini na   watanzania wote   kote nchini kuweza kumuombeombea Raisi ya Jamhuri ya Muungano   wa Tanzania Dkt, John Pombe Magufuli pamoja na viongozi wote   ili kuweza kuafanikiwa katika vita kubwa ya kiuchumi wanayo pambana nayo. Sambamba na hili Bi Zainabu   amewataka akina mama wote kuweza kuwasomesha watoto   wa kike   ambao ndio kundi kubwa linalo adhiliwa na   haki ya kunyimwa   fursa za elimu kutokana na chanagamoto lukuki zinazo wakabili watoto wa kike. Bi Zainabu aliyasema hayo wilayani Mpwapwa mkoani Dodoma   alipokuwa akiongea na wananchi wa wilaya hiyo alipokuwa akihudhuria msiba wa mama mzazi wa   mkurugenzi wa halmasahauri ya Pangani    bwana Sabasi   Chambasi   ambae ni mzawa wa Mpwapwa. Mkuu wa wilaya huyo bi Zainabu   akiwa ndiye mkuu wa wilaya pekee mwenye umri mdogo katika   wakuu wa wilaya wote   hapa nchini alisema “mimi pia ni mtoto wa kike   hivyo natambua changamoto z

GEREZA LA MPWAPWA LAKABILIWA NA UHABA WA NYUMBA.

Gereza la Mpwapwa mkoani Dodoma linakabiliwa na uhaba mkubwa wa nyumba za askari na kusababisha askari kukaa kwenye nyumba ndogo na zisizo na hadhi kwa askari hao. Haya yamebainishwa na Mkuu wa gereza la mpwapwa mrakibu mwandamizi wa jeshi la magereza bwana Joseph Tembo ameanza jitihada za kupunguza uhaba wa nyumba za askari kwa kuwatumia wafungwa kufanya kazi hizo. Bwana tembo amesema kuwa mpaka sasa wamefyatua na kuchoma zaidi ya tofali elfu harobaini na tano ambazo zitatumika kujengaea nyumba sita za watumishi gereza hilo,Tembo amesema serikali inazitaka magereza kuwa sehemu ya kuwabadilisha tabia na mtazamo kwa wafungwa wale wanao kinzana na sheria .     Mkuu wa Gereza la Mpwapwa Joseph Tembo akizungumzia hali halisi ya Mkakati wa Uboreshaji wa nyumba za Askari. Adha amesema kukamilika kwa nyumba hizo kutapunguza adha ya nyumba kwa askari kumi nambili kupata   makazi bora na   ya kisasa ambapo hapo awali walikuwa wanatumia nyumba za matope na dogo ambapo zolikuwa