Posts

Showing posts from January, 2018

VITA YA UHARIBIFU WA MAZINGIRA NI ZAIDI YA UGAIDI.

Image
Hii ni miongoni mwa nyumba za mwanzo am[o baba wa taifa marehemu Nyererealikuwaakifanyia mikutano yake humo ikombioni kusomwa na maji kutokana na uharibifu wa maxingira. VITA YA UHARIBIFU WA MAZINGIRA NI ZAIDI UGAIDI.  MAZINGIRA ni uhai,Mazingira ni vitu vyote vinavyo tuzunguka vyenye na uhai na visivyo na uhai, vitu vyenye uhai ni  mimea na wanyama na visivyo uhai  ni pamoja na hewa  ardhi na  maji, mazigira yanahusisha vitu vyote kuendelea na kuwepo kwa viumbe vingine.  Maisha ya viumbe vilivyopo na vijavyo utegemea   mawasiliano mazuri kati ya mazingira  watu na,uhai, uhuru na usatawi wa taifa letu la sasa hutegemea sana maisha yanayo tuzunguka, leo hii uharibifu wa mazingira umekuwa ni  nitishio kubwa la uhai wa binadamu na mataifa mbalimbai ulimwenguni. Mabadiliko ya tabia ya nchi ni tishio la usalama wa maisha kama ilivyo kwa ugaidi  na vita,  sote tumekuwa mashaidi njisi tunavyoshuhudia njisi mvua zimeendelea kushuka na kuto kuwa za kutabilika  siku hadi  siku ,joto

CHAMA CHA WAAANDISHI DODOMA CHASHAURIWA KUJIPANGA KUPOKEA MAKAO MAKUU,

MSEMAJI wa Serikali na Mkurugenzi wa Idara ya Habari maelezo Dkt Hassan Abbas amekitaka chama cha waandishi wa habari club ya waandishi wa Habari ya Mkoa wa Dodoma (CPC) kujipange vyema kuhudumia taifa la Tanzania na mataifa mengine kwa kuwapatia habari ambazo hazila viashairia vya uchochezi. Dkt Abbas ameyasema hayo mjini Dodoma wakati akiongea na wanachama wa chama cha waandishi wa habari mkoani Dodoma katika mkutano wao mkuu uliofanyika mjini Dodoma hapa na kusema (CPC) inatakiwa ijipange vyema kuhudumia serekali kwa kuwa na waandishi wa habarai wenye kufuata misingi ya taaluma yao. Katika kufanikisha hilo, Dkt Abbas ambaye pia ni muumini wa tasnia ya habari amewakikishia wana CPC kufanya nao kazi wakati wote na idara ya habari maelezo itasaidia mafunzo mbalimbali kwa waandishi wa habari. Katika kuhakikisha kuwa hilo linafanyika Kwa uande wake Mkuu wa mkoa wa dodoma Dr. Binilith Mahenge akizungumza wakati wa akifungua mkutano huo akawataka waandishi wa habari nc

SERIKALI YAJIPANGA KUTOA CHANJO YA SARATANI

Naibu waziri wa afya mandeleo ya jamii, jinsia, wazee, na watoto Dr. Faustine Ndungulile amesema kuwa serikali inatarajia kuanza kutoa chanjo ya kujikinga na saratani ya matiti pamoja na saratani ya shingi ya kizazi kwa mabinti wenye umri wa miaka 14 mapema mwezi April mwaka huu. Kwa mujibu wa Takwimu za shirika la afya duniani ya mwaka 2012 zinaonyesha kuwa 80 ya saratani ya mlango wa kizaza zinatokea katika nchi zinazoendeleo,ukilinganisha na nchi nyingine za afrika mashariki Tanzania inaongoza kwa kuwa na wagonjwa 50.9 kwa kila wanawake 100,000 lakini pia tunaongoza kwa kuwa na vifo 37.5 kwa kika wanawake 100,000. Akizungumza leo mjini hapa wakati akizindua kampeni ya kupima saratani ya shingo ya kizazi pamoja na matiti Dr. Ndungulile alisema kuwa ili kukabiliana na tatizo hilo serikali imeona ni vyema kuanza kutoa chanjo wa ugonjwa huo. Amesema kuwa watarajia ndani ya mwaka huu kutoa chanjo kwa mabinti wapata 6,16,734   nchi nzima. Amesema kuwa wao kama serika

POLISI WABAINI KUWA NABII TITO NI MGONJWA WA AKILI,

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma,Gilles Muroto amesema kuwa katika uchungizi wa awali uliofanywa imebaini kuwa Titto Onesimo Machibya (44) anayejiita Nabii Titto anasumbuliwa na matatizo ya akili. Nabii Titto ambaye ni mkazi wa kijiji cha Ng’ong’ona Manispaa ya dodoma alikamatwa na jeshi la polisi baada ya kurekodiwa kwa picha za video na kuanza kusambazwa kwenye mitandao ya kijamii jambo ambalo ni kinyume na kifungu cha sheria namba 129 cha kanuni ya adhabu sura ya 16 kilichofanyiwa marekebisho mwaka 2002. Nabii Titto amekuwa akitumia vibaya kitabu cha Biblia kwa kutoa tafsiri za upotoshaji ,pia amekuwa akifanya vitendo vya udhalilishaji hadharani na kuchochea maovu katika jamii kwa akishirikiana na wanawake wawili wanaodawa ni wake zake pamoja na mtumishi wake wa ndani. Akizungumza na Waandishi wa Habari leo Mjini hapa,Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma,Gilles Muroto amesema kuwa Nabii Titto aliwahi kupatiwa matibabu katika hospitali ya mhimbili atiwa anasumbuliwa

MVUA ZASABABISHA MADHARA MPWAPWA

  Mvua vua   zinazoendelea kunyesha     hapa wilayani   Mpwapwa mkoani Dodoma kunatishia baadhi         makazi   ya watu   wa   mtaa wa National housing , Majengo na Hazina na vighawe ziko hatarini kusobwa na   maji   kama   hakuna jitihada za makusudi hazitachukuliwa ili kuweza kunusuru   makazi ya watu hao.   Makazi ya watu binafsi ambazo tayari zimesha sobwa upande ni   ni   baa na nyumba za wageni ya Central , Hapeq pamoja na shule ya na kituo cha kulelea watoto cha The Hiral   kinachomilikiwa na Mwalimu Gisela Kapinga.   Mvua hizo   ambazo zimekuwa   zikiumiza vichwa   vya viongozi   hapa wilayani   juu ya kazi   ya kuyanusuru   makazi hayo na muindo mbinu   ya tasisi hizo ambazo zilitumia pesa   nyingi katika kuwekeza   na ukamilifu wake wa tasisi hizo. Mkuu wa wilaya ya Mpwapwa bwana Jabir Shekimweri        alisema   ofisi yake   kwa kuishirikiana na ofisi ya Tanroad Mkoa   wamefanya   tadhimi   ya awali   ya kuweza   kujua ghalama zitakazo weza kutumika kuayanusur

MIMBA ZIMEKUWA KIKWAZO CHA ELIMU MPWAPWA.

Image
Baadhi wa Wadau akisikiliza mjadala wa Elimu  wilayani Mpwapwa. MKUU   wa mkoa wa Dodoma Dkt Binilith Mahaenge amesema nchi zote zinazoendelea   zinatakiwa kuwekeza kwenye Elimu ili kuweza kufikia katika nchi zilizo endelea. Dkt Mahenge alitoa kauli hiyo jana alipokuwa akifungua mkuno wa wadau wa elimu wilayani Mpwapwa uliofanyika katika chuo cha ualimu mjini hapa. Mahenge alisema nchi zote zilizoendelea   ziliwekeza nguvu kubwa katika elimu   hadi kufikia maendeleo zinazojivunia kwa sasa   na kuwa na rasilimali watu wengi   na wazalishaji tofauti na nchi zinazoendelea   kundi kubwa limekuwa si la kuzalisha   na hivyo kubaki kama obwe kubwa la kiuchumi. Dkt Mahenge alisema kuwa “tunaweza kutoka katika nchi zinazoendelea na kufikia nchi zilizo endelea   kwa kuwekeza sana sana katika elimu   tusione nchi zilizoendelea ziko mbali waliwekeza san asana kwenye elimu   ndugu zangu hatuwezi kufika popote tukiendelea kufanya vibaya   katika elimu lazima tuwandae rasilimali

WALIMU MPWAPWA WAASWA KUTO KUKOPA MIKOPO YA KUWAZALILISHA.

Image
Kaimu ofisa Elimu   sekondari   wilya ya Mpwapwa Mkoani Dodoma Bi Frola Mkwama amewataka walimu kijishughulisha na miradi midogo midogo ya kujiongezea kipato kuliko kujiingiza kwenye mikopo ya watu binafsi   ili kuepuka fedheha zinazo wapata pindi washidwapo kulipa. Bi Mkwama aliyasema hayo juzi katika mkutano mkuu wa kumi na tisa wa chama cha kuweka na kukopa cha Mpwapwa Teachers Saccos iliofanyika katika ukumbi wa CCM mjini hapa. Bi Mkwama alisema siku hizi kumeibuka maduka mengi yanayo kopesha   na hivyo walimu    wengi wamejikuta wakidaiwa kadi za Benk na namba za siri kitu kinacho   sababisha walimu wengi kujikuta wakiishi maisha magumu. Aidha Bi Mkwama   alisema “kwa mwalimu kuobwa kadi na namba ya siri ni kinyume na sheria na privace ya mtu lakini pia haya maduka yanayo kopesha sijui kama yamesajiliwa kama tasisi za kukopesha bali yamesajiliwa kama maduka ya kuuza bidhaa hivyo hata watu wa biashara yachunguze maduka hayo. Pia alisema hata riba ya   maduka hayo

UCHAFU WATISHIA KIPINDIPINDU MTAA WA MAJENGO.

Image
Badhii ya wananchi wakifanya  usafi katika  Ndampo  la kwa Nzige  ambalo si rasmi Ndampo hilo limepelekea MVUA  kutaka kusomba nyumba ya mwl Sambae . WANANCHI wa mtaa wa majengo katika kata ya Mpwapwa mjini   wilayani hapa wamelalamikia kitendo cha   uongozi wa wilaya kuweka Dampo la taka   katika maeneneo ya makazi ya watu na kutishia kutokea kwa ugojwa wa kipindupindu katika msimu huu wa mvua za vuri. Kedmoni Mapuga   mkazi wa   mtaa huo alisema kumewako   na   usumbufu mkubwa   na badhii ya wakazi wa mtaa huo wenye watoto wadogo huwalazimu kuhama nyumba   kutokana kukidhiri kwa taka katika mtaa na harufu mbaya pamoja na moshi mkali pindi wachumapo taka hizo kuawathiri kiafya   na kusababisha vikohozi kwa watu wa mtaa huo. Mapuga alisema   baada   wakazi wa mtaa wa majengo   wamekuwa wakiadhiriwa na moshi mkali na wenye harufu kali na kutishia wakazi wa   mtaa huo kupata ugonjwa wa kihozi kama bado halimasahauri ikiendelea kuchoma taka katika eneo la korongo ambalo liko