Posts

Showing posts from June, 2017

UGONJWA WA NGURUWE WAWATIA UMASKINI WAFUGAJI MPWAPWA.

BAADHI yawafugaji   katika wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma wameingia hasara    kwa   kupoteza mifugo   yao aina ya nguruwe kutokana na kuzuka kwa ugonjwa wa nguruwe    ujulikano kama African swine fever.   Wakiongea na Gazeti hili   kwa nyakati tofauti    mmoja wa wafugaji   bi Tabitha Simbeye alisema tangu ugonjwa huo   uzuke wafugaji wengi wamepteza nguruwe wengi na hivyo kuwasababishia hasara   kubwa.   Tabitha   alisema   katika   mtaa wake zidi ya   zizi lake kulikuwa na nguruwe sita wote walikubwa na ugonjwa baadhi alifanikiwa kuwauza kwa hasara na wengine walikufa na kuwazika. Alisema nguruwe wengi yameathiliwa na ugonjwa   huo   ambapo alisema Nguruwe hutetemeka na kukosa nguvu . kushidwa kutembea. Aidha mmoja wa   watafiti   wa mifugo kutoka katika Tasisi ya utafiti wa mifugo   TARILI Mpwapwa ambae jina lake hakutaka liiandikwe alisema kuwa   ugonjwa ambao   hutokea kwa msimu   hiyo   na ni ugonjwa unao sababishwa na virusi hivyo ni ngumu kutibika wala kukinga.

MIZOGA YA PUNDA IKONEKANA IKITELEKEZWA PORINI BAADA YA KUCHUNWA NGOZI

Image
MIZOGA YA PUNDA KATIKA KIJIJI CHA MZASE KATA BEREGE IKTELEKEZWA PORINI

UWIZI PUNDA UTAONGEZA UMASKINI VIJIJINI

.   Serikali imeobwa kuweka mkakati maluum wa kudhibiti   wimbi la uwizi wa punda ngozi ya   Punda   kutokana na   mnyama huyu kuwa katika hatari kubwa ya kutoweka nchini   na hivyo kusabisha kuongezaka kwa wimbi la umaskini kwa jamii nyingi za vijijini zinazo mtegemea mnyama huyu. Matukio ya uwizi wa punda   yamekuwa yakiongeeka kila kukicha sehemu mbalimbali za wilaya    ya Mpwapwa na mkoa mzima wa Dodoma. Katika Tukio   lililotokea katika kijiji Mzase kata ya Berege wilayani hapa punda watano wamekutwa wameibwa na kuchunwa ngozi huku mizoga yao ikiwa ametelekezwa porini. Mmoja wa wanakijiji   hicho   bwana Naftari Asheri amesema kuwa endapo jitihada za makusudi hazitachukuliwa   za kuweza kuokoa uwizi wa punda kuna uwezekano mkubwa wa wanyama hao kutoweka na   na hivyo kusababisha ongezekao la umaskini sehemu za vijijini kulingana na umuhimu wa mnyama huyo katika maisha ya Mtanzania. Aidha Bwana Naftari alisema kuwa   lazima serikali iweke mkakati   madhubuti w

JESHI LA POLISI LATEKETEZA HEKALI 11 ZA BANGI MPWAPWA.

Kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ya mpwapwa   mkoani Dodoma imekamata na kuteketeza hekali 11 za bangi katika safu za milima   Galigali kitongoji cha Dibulilo. Kamati hiyo iliyo ongozwa na mwenyekiti wa kamati   ambae ni mkuu wa wilaya ya Mpwapwa bwana Jabiri Shekimweri juu ya oparesheni ambayo ni mkakati wa kupambana   na   madawa ya kulevya wilayani hapa. Mkuu wa wialaya   ya ampwapwa bwana Shekimweri alisema kuwa   mkakati   wa kutokomeza madawa ya kulevya   ni endelevu    katiika wilaya yake   na hivyo   lengo kuu ni la kukisaidia kizazi cha wana mpwapwa cha sasa na badae    kwa mstakabali wa taifa   zima. Aidha   Shekimweri   amewataka   watenadaji wa kata na viiji kuweza kuweka mkakati huo kwa nagazi ya kijiji, kata na tarafa . Alisema “Nina wataka watendaji wote wa kata na vijiji kuweza kuweka mkakati huu wa kupambana na madawa ya kulevya kwa ngazi ya kata na tarafa na yeyete kwenye kata yake ikabainika kuna ulimaji wa bangi    na bila yeye kutoa taarifa   a