Posts

Showing posts from May, 2018

PAROKO KANISA KATOLIKI ATAKA HUDUMA ZA JAMII KUBOREKA MPWAPWA.

Image
Paroko wa kanisa Katoliki Parokia ya Mpwapwa  Pd Daud Ngimba  akihubiri anisani . PAROKO wa kanisa katoliki Parokia ya Bikira Maria wa Fatima Mpwapwa jimbo   kuu la Dodoma Padre Daud Ngimba imeitaka jamii ya   watu wa Mpwapwa na viongozi wa Serikali   kuweza kutumia fursa ya Serikali kuhamia Mkoani Dodoma   kuboresha huduma za kijamii kama ,   Barabara,shule , Afya na huduma za maji   wilayani hapo. Padre Ngimba aliyasema   hayo mwishoni mwa wiki    alipo kuwa akitoa mahubiri   kwenye Misa ya   Utatu mtakatifu   na alipokuwa akiutambulisha mkakati wa kanisa hilo katika kujikita katika utatuzi wa changamoto zinazo ikabili jamii ya Mpwapwa. Padre   Ngimba alisema wakristu ,Tasisi za dini    pamoja na serikali za mitaa katika mkoa wa Dodoma   zitaweza kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania   Mhe Dkt John Pombe Magufuli kwa kuhamisha makao makuu ya serikali kuja Dodoma na kuipandisha hadhi mkoa wa Dodoma kuwa   kuwa jiji kwa kuboresha huduma za jamii na kuyapatia

DARAJA LA GODEGODE LITAFIFISHA MAPATO YA HALMASAHAURI.

WANANACHI wa kata ya Godegode,Pwaga na Lumuma wameiomba serikali kuweza   kurudisha mawasiliano   ya barabara    baada ya   daraja   la Godegode   ambalo ni kuungo muhimu kati ya kata hizo   na makao makuu ya wilaya   kusomwa na maji   katika msimu   wa mvua mwaka huu. Wanachi wa   kata   hiyo   wametoa   ombi hilo mbele ya naibu waziri wa ujenzi   Mhe Eliasi Kuandikwa (MB) alipokuwa kwenye   ziara   ya   kukakuga ujenzi wa barabara za Mpwapwa na kufika katika   daraja hilo   kuangalia   hali harisi ya   changamoto ya   usafiri katika eneo hilo. Diwani wa kata ya godegode Bwana Tanu Makanyago amesema daraja hilo ambalo ndio muhimili   mkuu wa   mawasiliano kati ya   kata ya Godegode,Pwaga, na Lumuma kwa mawasiliano . Aidha Bwana Mkanyago  amesema kutokana na uharibifu   wa daraja hilo   kumepelekea maisha ya watu wanaoishi katika kata hizo kupanda bei kwa   gharama maisha ikiwemo   usafiri,bidhaa madukani   lakini pia kuchukua muda mrefu kwa kuyafikia makao makuu ya

SARATANI YA SHINGO YA KIZAZI INATISHIA AFYA ZA KINA MAMA.

JAMII imeshauriwa kuziamini   tafiti za kitaalamu   zitolewazo na   Serikali ili kuweza kujiletea maendeleo endelevu au kupunguza athari zinazo weza kujitokeza siku za   mbeleni. Kauli hiyo imetolewa   wilayani Mpwapwa katika Hospitali ya Benjamini Mkapa na Mratibu wa   masuala ya magonjwa ya Saratani   Dkt,Angel Msaki alipokuwa   akiongea   na Majira fisini Kwake   jana. Dkt,Msaki alisema serikali ikiwa katika    mkakati   mkubwa wa    utoaji wa kinga   ya   saratani ya mlango wa kizazi   bado kwa wilaya ya Mpwapwa kunaonekana mwamko kuwa duni na kutishia   watu wengi kuto fikiwa   na   na zoezi hilo. Aidha Dkt. Msaki alidai kuwa    tangu    huduma hizo zianze   kutolewa   hosptalini hapo    kuanzia julai 2017 ni akina mama 530   walifikiwa na huduma   hiyo na kati hayo akina mama   18 walipatikana na   daliiza awali   za mlango wa kizazi na akina mama 10   walifanyiwa matibabu   ya   ugandishaji na akina mama 25   walipewa rufaa kwenda kuchunguzwa katika hospitali ku