Posts

Showing posts from 2016

POLISI MPWAPWA YAKABILIWA NA UHABA VITENDEA KAZI.

Image
Na Stephen noel mpwapwa. JESHI la polisi wilayani Mpwapwa mkoani Dodoma linakabiliwa na upungufu  mkubwa wa vityendea kazi ikiwemo magari na pikipiki kitu kinachopelekea jeshi hilo kushidwa kuwahi katika  matukio ya kiuharifu. Kauli hiyo  ilitolewa jana na Mrakibu wa polisi   bwana Paulo Ngonyani mkuu wa kitengo cha Intelinjesia mkoani Dodoma  alipokuwa  katika hafla ya kukabithiwa Pikipiki mbili zilizonunuliwa na wadau wa polisi wa wilayani  Mpwapwa kwa lengo la kupambana  na uharifu wilayani hapa. Bwana Ngonyani alisema katika jeshi la polisi limekuwa likilalamikiwa sana na wanajmii kuwa wamekuwa wakichelewa kufika katika matukio ya kiuharifu kutokana na kukabiliwa na chanagamoto kubwa ya ukosefu wa vitendea kazi kama vyombo vya usafiri,pamoja na mafuta Aidha Ngonyani  alisema  kwamba  ili kuimarisha dhana ya polisi jamii wameamua kuwashirikisha wadau  wa maendeleo katika wilaya husika kuweza kusaidiana kuzikabili changamoto zinazo likabili jeshi
Imeelezwa    kuwa    shughuli za   ajira muda zilizofanywa na walegwa wa mpango wa kaya maskini TASAF awamu ya tatu kama kutunza Misitu ya asili,uvunaji wa maji ya mvua, na utunzaji wa udongo,ikitumika inavyopaswa itaweza kuleta mabadiliko   chanya kwa   jamii   na kuweza kujiletea maendeleo endelevu. Kauli hiyo imetolewa na Mratibu wa Tassaf wa halmasahauri ya wilaya ya Mpwapwa Bwana Paskal Jeremia   alipokuwa akiongea   na waandishi wa habari ofisini kwake juu tadhimini   ya utekelezaji wa mpango wa ajira za muda zijulikanozo kama (PWP)kwa wanufaika wa mpango huo wilayani hapa Jeremia amesema   rasilimali hizo kama ujengaji wa miundo mbinu ya   kuvuna maji ya mvua, wa   utunzaji wa misitu, na   uhifadhi wa   udongo   ngazi ya jamii italeta mabadiliko   kuwa   mazuri   zaidi   na jamii kuweza kujiletea   maendelea endelevu katika maeneo yao yanayoishi. Aidha   amesema kwa sasa zoezi hilo limetekelezwa kwa zaidi ya asilimia 70% katika vijiji vyote   ambavyo   mradi huo ul

LITA MPWAPWA YAPATA MAABARA YA KISASA

Image
Dkt MACIEJ KLOCKIEWICS akiwa katika hafla ya uzinduzi wa maabara ya kisasa MPWAPWA Dkt Justina kutoka Uholanzi katika hafla ya ufunguzi wa maabara ya kisasa LITA MPWAPWA. Dkt Justina akicheza SHOO  na BAADHI YA Wanachuo wa LITA mpwapwa wakifurahia UFUNGUZI w maabara ya uchunguzi wa magonjwa ya mifugo   lita Mpwapwa. Mkuu wa wilaya ya mpwapwa akiongea neno ktika uzinduzi wa hafla hiyo. Dkt Mery Mashingo akiwa katika picha y pamoja na wgeni waalikwa na wafadhili wa maabar hiyo kutoka nchi ya Uholanzi. Dkt Mery Mashingo akifungua maabara ya uchunguzi wa magonjwa ya wanyama yatokanayo na wadudu iliyo fadhiliwa na chuo kikuu cha sayansi cha nchini uholanzi, katika tasisi ya uwakala wa mafunzo ya mifugo LITA kampasi ya Mpwapwa.

Kilimo cha korosho chafikiliwa kukwamua uchumi wa Mpwapwa.

Image
Mkuu wa wilaya awaza kuanzisha kilimo ch korosho Mpwapwa hiyo ni baadhi ya miche ya mkorosho  iliyo otesha katika magereza ya Mpwapwa tayarikwa kwenda shamabani. Mkuu wa Gereza la Mpwapwa SSP .Joseph Tembo  akionyesha taarifa  njisi ya upandaji wa miche ya   korosho . Miche ya mikorosho  iliyo stawishwa KATIKA Gereza la Mpwapwa.

SHAKIMWERI AKAGUA HUDUMA ZA AFYA MPWAPWA

Image
Mkuu wa wilaya ya Mpwapwa akikagua  huduma za afya hapo anazungumza na Kaimu mkurugebzi wa TARILI Mpwapwa Dkt Komuhangilo, Mkuu wa WILAYA  akiongea na wajumbe kamati ya ulinzina Usalama Tarili. Akiangalia baadhi ya dawa katika  katika Zahati ya  TARILI

KIPINDIPINDU CHAUWA WAWILI MPWAPWA.

  JUMLA   ya watu   94   katika   wilaya ya Mpwapwa   katika   mkoa wa Dodoma wamegundulika kuumwa   ugonjwa wa kipindupindu wakati wawili tayari wamesha fariki Dunia kutokana na ugonjwa huo. Hali hiyo imeelezwa   mganga mkuu wa   ya wilaya ya Mpwapwa   Dkt Siad Mawji alipokuwa akiongea   na waaandishi wa   habari juu ya kuwapo kwa wa ugonjwa huo katika wilaya hiyo na kusabaisha   hali ya wasiwasi kwa wakazi wengi wa wilaya hiyo na viunga vyake. Dkt Mawji alisema   kuwa mgonjwa wa kwanza   aligundulika   octoba   26   mwaka huu   akitokea kata ya Mweznele   na wagonjwa wengene waliendelea kujitokeza kutoka katika kata mbalimbali hadi kufikia wagonjwa   94 tangu ugonjwa huo uanze hadi sasa. Hata hivyo alisema w wagonjwa wengine   walitokea katika kata ya Tambi,Mpwapwa mjini,   Lumuma na Matomondo na kufanya   wagonjwa wote kufikia wagonjwa 94. Aliongeza kuwa   hada kufikia jana ni wagonjwa kumi na watano 15 ndio   waliolio lazwa   katika kambi maluum   ya kuwashughulikia

WAGANGA NA MANESI WAONYWA KUTOA HUDUMA KIMAZOEA

SERIKALI   wilayani Mpwapwa moani Dodoma imewata wanganga na manesi wilayani hapa kuweza ku kufanya kazi yao kwa kufauta maadili ya kazi ili kuweza kuokoa maisha ya wagonjwa . Kauli hiyo ilitolewa na mwenyekiti ya kamati ya ulinzi na usalama na   mkuu wa wilaya hiyo   bwana   Jabir Shekimweri   alipopanya ziara za kushitukiza katika   vituo   vya afya na zahati   za serikali na za umma   kwa lengo ya kujionea huduma zinazo tolewa na vituo hivyo na   miundo mbinu yake. Shekimweri alisema kuwa   ameamua kufanya ziara hiyo ili kuweza kuona huduma za afya zinavyo tolewa na vituo hivyo   na   changamoto zinazo vikabili vituo hivyo na njisi ya kuondokana nazo. Aidha   shakimweri alisema   serikali ikiwa inajiandaa kuhamia   mkoani Dodoma lazima wilaya za mkoa huo kujipanga kuboresha huduma za jamii    ikiwamo afya ambayo ndio msingi mkuu wa   huduma zote   katika kuwekeza katika taifa lenye rasimali watu na wazalishaji . Hata hivyo   Shamweri alisema kuwa pamoja na ziara hiyo