Posts

Showing posts from May, 2020

WANANCHI IGOVU WAHAMASISHANA KUFANYA MAENDELEO

Image
Na Stephen Noel.  Wananchi wa Mtaa wa Igovu kaskazini wakimsikiliza Mwenyekiti wao wa mtaa baada ya kumaliza shughuli za maendeleo. WANANCHI wa Mtaa wa Igovu kata ya Mpwapwa mjini   Wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma   wameushauri uongozi wa serikali za mitaa ngazi ya halmashauri kuweza kushirikiana na uongozi ngazi ya mitaa kutumia rasimali walizonazo   kuondoa chanagamoto   ndogondogo zinazowakabili wananchi kuliko kutegemea bajeti    ya serikali kuu. Wananchi hao walitoa ushauri huo   walipokuwa wakiongea na mwandishi wa habari    jana walipokuwa katika shughuli   za maendeleo za mtaa wa Igovu   kwa kuchimba barabara na   kuweka kufusi   ili kuweza kurahisisha upitakaji wa   njia mtaani   hapo. Kwa mujibu wa mwenyekiti wa mtaa huo bwana Elieza Mwaluko alisema kwa sasa seikali   ina miradi mikubwa ya kimkakati inayotekelezwa “lakini serikali ngazi ya halmashauri na serikali za mitaa ngazi ya mitaa na vijiji wakitumia raslimali walizonazo watapunguza changamoto am

MAHAKAMA YA (W) MPWAPWA YAMFUNGA MIAKA 30 KWA KOSA LA KULIMA BANGI

Image
  MPWAPWA -MWANAWOTA. Mahakama ya hakimu mkazi ya wilaya   ya Mpwapwa mkoa wa  Dodoma  imemuhukumu kifungo cha miaka 30   jela      bwana   Julius Lwagila (52) baada ya kupatikana na kosa   kulima   na kuhifadhi madawa ya kulevya aina ya bangi. Hukumu hiyo iliyokwishatolewa   mwaka  2019,na aliye kuwa hakimu mkazi wa mahakama hiyo bwana Paschal Mayumba lakini haikutekelezwa kutokana  na  mtuhumiwa siku ya hukumu   kutotokea mahakamani. Hata hivyo  mahakama ilitoa adhabu hiyo   bila mtuhumiwa huyo   kuwapo    mahakamani na mahakama kuamauru jeshi la polisi kumtafuta popote alipo ili atumikie adhabu yake.  Hukumu hiyo iliyotolewa na aliyekuwa   hakimu mkazi    wa Mahakam ya wilaya Mpwapwa   bwana Paschal Mayumba ambae kwa sasa amehamia mahakama ya   wilaya ya Dodoma.  Siku ya hukumu  hakimu Mayumba aliiambia mahakama kuwa mtuhumiwa huyo     mkazi wa kijiji cha Isasamambo kata ya Mwanawota na wilaya ya Mpwapwa   alikamatwa na jeshi la polisi Mpwapwa likiwa