Posts

Showing posts from February, 2017

UMATI WAJITOKEZA KUWAZIKA NDUGU WA FAMILIA MOJA WALIOFARIKI KWA MAJI.

Image

MKINZANO WA SHERIA KIKWAZO UHARIBIFU MAZINGIRA MPWAPWA.

  Na Stephen Noel. mpwapwa .   MKUU wa wilaya ya Mpwapwa   mkoani Dodoma   bwana Jabir Shekimweri   amesema mkinzano mkubwa uliopo kati ya sheria mama ya mazingira   ya mwaka   2004 na   sheria ndogo ya halmasahauri ya wilaya hiyo ni miongoni mwa sababu zinazo fifisha   harakati za kupambana na uharibifu wa mazingira wilayani hapa. Shekimweri ameyasema hayo mjini hapa alipokuwa akifanya mahojiano maluum majira juu ya hakarakati na mkakati uliopo kwa wilaya ya mpwapwa juu ya uharibifu wa mazingira   na matokeo yake.   Shakimweri amesema kuwa   sheria ya mama ya mazingira   mwaka ya   mwaka 2004   inayo mtaka   mharibifu wamazingira   anapo patikana na hatia   anahukumiwa kifungo cha   cha miezi sita   hadi mika miwili jela au faini ya shilingi   50,000/= hadi   million 50,000,000/= au vyote viwili kwa pamoja. Aidha amesema kuwa sheria ndogo ya halamasahauri hiyo inayo mtaka mharibifu wa mazingira    akipatikana na   hatia     anatakiwa kulipa faini ya shilingi 50,000/=na i