Posts

Showing posts from January, 2016

MPWAPWA YAMLIZA KAPONDA KIELIMU

OFISA elimu mkoa wa Dodoma   Bwana Juma Kaponda (JJ)amewataka wataalamu ,wanasiasa,   na walimu   kushirikiana   katika kushughulikia   changamoto za Elimu ili kuweza kuinua elimu   wilayani hapa. Kaponda aliyasema hayo   wilayani hapa   katika mkutano wa wadau wa elimu   uliojumuisha , walimu wakuu wa shule zote, waratibuelimu kata , na   na maofisa wa elimu , uliofanyika   katika ukumbi wa chuo cha ualimu   Mpwapwa   juu ya   kutadhimini   matokeo ya darasa la saba   ya mwaka   2015. Kaponda   alisema   katika mtihani wa   kumaliza elimu mwaka 2015   wilaya ya mpwapwa ilikuwa wilaya ya mwisho   kimkoa   na ilikuwa wilaya ya 164 kati wilaya 166 nchi zima ,japo ilifanikiwa kutoa mwanafunzi wa kwanza kimkoa kutoka katika shule   ya Mazoezi Mteajeta   mwanafunzi   Airene Chiwanga Aidha alisema   ufundishaji   mbovu,utendaji wa kimazoea   kwa maofisa Elimu   , kukosekana   kwa mawasiliano   sahihi kati walimu   na maofisa   elimu   imepelekea Mpwapwa   kushidwa kufanya   viz

WADAU MPWAPWA WAJADILI CHANGAMOTO ZA ELIMU

Image
Mwl mkuu shule ya Msingi Mangangu Akichangia mada katika  mtano wa wadau

WANACHI WA MPWAPWA WAMTAKA WAZIRI LUKUVI KUWAANZISHIA BARAZA LA ARDHI LA WILAYA.

Na Steph noel Mpwapwa WANANCHI   wa wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma wamemuomba waziri   mwenye dhamana ya Wizara   ya Ardhi Nyumba na makazi   Mhe , Wiliam Lukuvi   kuwaanzishia   Baraza la Ardhi la wilaya kufuati usumbufu wano upata kufuata huduma hizo katika wilaya ya   Dodoma mjini. Walisema huwalazimu kusafiri umbali wa zaidi ya kilomita 90 hadi 110   kutafuta huduma za kishria juu ya migogoro ya ardhi   na mipaka. Wanachi hao yaliyasema hayo kwa nyakati tofauti wilayani hapa walipokuwa wakiongea na Majira   juu ya usubufu wanao upata kufutia kutafuta haki zao za migogoro ya ardhi iliyo shindikana ngazi ya mabaraza ya kata   na hivyo huwalazimu kutumia muda mrefu na gharama nyingi, na wengine wakiacha kufuatilia haki zao hizo kutokana na kushidwa   gharama . Mmoja wa wakazi wa   wilayani hapa bwana Alex Mwarabu   mkazi wa kijiji cha Kisokwe   alisema kumekuwako na usumbufu mkubwa unaotokana na   huduma nyingi za kutafuta haki kuwa mbali na hivyo hupelekea baadhi ya wa

MKURUGENZI MTENDAJI MPWAPWA AWATAKA WATENDAJI WAKE KUACHA URASIMU.

Na Stephen noel –Mpwapwa MKURUGENZI   mtendaji wa halmashauri ya wilayaya mpwapwa mkoani Dodoma Bwana Mohamed Maje amesema kuwa atahakikisha   anakomesha urasimu wote kwa watendaji wake wa chini kwa wawekezaji wanaotaka kuwekeza wilayani hapa. Mkurgenzi huyo ameyasema hayo   wilayani hapa   walipotembelea   kiwanda kidogo cha kusindika siagi ya karanga   kilichopo mjini hapa mtaa wa mji mpya. Maje amesema hatavumilia kuona watendaji wake wa chini wanawakwamisha wawekezaji wanao taka kuwekeza mpwapwa. Meneja wa kiwanda cha kusindika karanga wilaya hapa bi Paulina Visent    amesema kuwa   wamekuwa   wakipata shida kutoka idara ya ardhi kupata eneo maluumu la kujenga kiwanda hicho   kwa kile alicho kisema kuwa kinakwamisha   na kurudisha nyuma moyo wawekezaji wengine wanao taka kuwekeza   katika wilaya ya mpwapwa kutokana na urasimu wanao upata kutoka kwa watendaji wa serikali. Aidha amesema kiwanda hicho kimesaidia kuitangaza Mpwapwa katika nyaja za kibiashara kwa mikoa y

Mkuu wa wilaya akikagua mashamaba

Image
Mkuu wa wialaya ya Mpwapwa akikagua baadhi ya masahamba ya wakulima Gulwe yaliyosomwa na maji  wilayani Mpwapwa mkoani DODOMA.

makazi yabomolewa na mvua

Image
baadhi ya njumba ya wakazi wa gulwe ikiwa imebomelewa.

mjumbe

Image
mjumbe wa kamti ya ulinzi na usalama  JOSEPH TEMBO akionyuesha kitu kwe eneo la tukio.
Image
Kipande cha reli ya gulwe kilicho haribiwa na mvua na kusababisha reli hiy kufugwa kwa muda.

MVUA ZASABABISHA MAFURIKO GULWE MPWAPWA

Na Stephen noel –Mpwapwa. Zaidi ya kaya 30 za kijiji cha Gulwe wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma hazina mahala pa kuishi kufutia mvua kubwa ilionyesha   usiku wa kuamkia jana na kusababisha nyumba zao kubomoka katika kijiji hicho. Sambamba na nyumba hizo kubomoka pia mvua hiyo imeharibu hekali 47 zamashamaba ya   mazao mabli mbali yalisomwa na maji . Diwani wa kata ya gulwe   bwana Gabriel Kizige alisema pamoja na maafa hayo pia yamesabaisha   zaidi ya kaya 50 nyumba zao kuingiliwa   na kusababisha badhii ya mali kuharibika ikiwemo chakula na mali zingine . Akitotaarifa ya madhara yaliyo patikana   mbele ya kamati ya maafa mwenyekiti wa kijiji cha gulwe Bwana Peter Sogodi alisema kuwa nyumba 30 za wakazi wa gulwe zilimomoka na nyumba 50 zilingia maji na hekali 47 za mazao   mbalimbali ziliharibika kwa kusobwa na maji. Aidha ofisa mkaguzi wa   njia ya treni Steshen Gulwe bwana Moses Magoha alisema pia mvua hiyo imesababisha hasara katika njia ya reli hiyo   kwa kufukiwa