Posts

Showing posts from February, 2018

TANZANIA YA KESHO INATISHIWA NA WIMBI LA WATOTO WA MITAANI.

IMEELEZWA kuwa   tunaweza kuitengeneza Tanzania ya kesho kwa kuwekeza   katika masalahi mapana ya watoto kimaadili,kiuchumi ,kielimu. Kauli   hiyo ilitolewa na   mkurugenzi mtendaji wa kituo   cha kompasheni namba TZ 236 KKKT   bwana Mboka Mwaipopo alipkuwa akiongea na waaandishi wa habari   ofisi kwake   hivi karibuni. Bwana Mboka alisema kuwa kumekuwako na vituo hivyo vilivyo anzishwa chini ya makanisa   vikiwa na lengo la kuwalea watoto katika Nyanja za kielimu, kiroho na   kiuchumi ili   waweze kuwa wazalishaji na    kuwezesha kuifikia Tanzania viwanda . Aidha Mboka alisema   kuwa siku zinavyo zidi   kusonga mbele kuna kunazidi kuongezeka kwa watoto wanaojulikana kama watoto wa mitaani kitu alicho kisema kuwa kinatishia ustawi wa taifa lolote siku za mbeleni. “Hiki ni kizazi cha watanzania wa Tanzania ya   kesho tukiendelea kuwaita watoto wa mitaani   tutambue kuwa Tanzania ya kesho nayo itakuwa ya mitaani kwa sabubu hii ndio picha ya Tanzania ya Kesho ,hivyo lazima

KIPINDUPINDU CHAUA 8 MPWAPWA .

  JUMLA   ya watu   8 wameafiriki dunia kutokana na ugonjwa wa kipindu pindu na wengine 189 wamegundulika kuumwa   ugonjwa huo katika wilaya ya Mpwapwa mkoa wa Dodoma tangu ugonjwa huo ulipotiwe kuingia wilayani humo nov 2017 . Mganga mkuu wa wilaya hiyo Dkt Said Mawji aliyasema hayo alipokuwa akitoa taarifa katika kikao cha baraza la madiwani mjini Mpwapwakilicho fanyika hivi karibuni. Mawji alisema   kuwa mgonjwa wa kwanza   aligundulika   octoba      mwaka jana   akitokea kata ya Chipogoro   na wagonjwa wengine waliendelea kujitokeza kutoka katika kata mbalimbali hadi kufikia wagonjwa   189 tangu ugonjwa huo uanze hadi sasa. Aliongeza kuwa   hadi kufikia feb   mosi mwaka huu kulikuwa na wagonjwa wapya 14 ndio waliolio lazwa   katika kambi maluum   ya kuwashughulikia   wagonjwa   wa kipindupindu . Aidha alisema   chanzo kikubwa cha ugonjwa huo katika kata hizo ni kutokana na kuwapo kwa tatizo la uhaba wa maji   na hivyo watu hulazimika kutumia maji ambayo si safi na s

JAFFO ATOA MIEZI MINNE KWA WATUMISHI IDARA YA MAJI.

Image
Waziri wa TAMISEMI Selemani Jafo ametoa miezi minne kwa mamlaka zote za maji nchini kuhakikisha zinafunga dira za maji kwa wateja wake wote kwa asilimia 90 na kuwa na miundombinu ya kutibu maji watakaoshindwa kufikia hapo watachukuliwa hatua. Waziri jafo ametoa agizo Hilo mjini Dodoma wakati akizindua ripoti ya utendaji wa mamlaka za maji za makao makuu ya wilaya na miji midogo nchini na ku sema hakuna sababu ya watu hao kuendelea kuwepo kama watakuwa wameshindwa kufikia asilimia 90 katika kufunga dira za maji. Amesema baada ya kipindi hicho cha miezi minne kupita na ikatokea kuna mamlaka ambayo haijafunga dira ya maji atavunja bodi ya mamlaka hiyo na kumfukuza kazi meneja wake kwa kushindwa kutimiza masharti hayo. Amesema hatua hiyo imefikiwa ili kudhibiti wizi wa maji ambao unafanywa na baadhi ya wateja kwa kushirikiana na baadhi ya watendaji wa mamlaka za maji ambao siyo waamifu na hivyo kusababisha mamlaka hizo za maji kujiendesha kwa hasara. Kaimu mkuru

MSIMAMO WA SERIKALI KUHUSU WATUMISHI HEWA.

SERIKALI imetangaza msimamo wake kwa watumishi ambao walibainika kuwa na vyeti feki na wale wasiokuwa na vyeti vya kidato cha nne kuwa hawana madai yoyote ya kuidai serikali baada ya Rais John Magufuli kutangaza kufanyika kwa uhakiki kwa watumishi wa umma. Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa idara ya uendelezaji sera, Mathias Kabundugulu,wakati akizungumza kwenye kikao cha kazi cha kujadili masuala ya utawala na rasilimali watu kwa mamlaka za serikali za mitaa, wizara na mikoa. Amesema watumishi ambao wamebainika na kuondoka wenyewe, wamefutwa kwenye orodha ya watumishi wa umma na hawana madai wanayodai serikalini huku amesema pamoja na zoezi hilo kukamilika kwa muda ambao umepangwa, wapo baadhi ya maafisa utumishi wameendelea kuwafumbia macho watu wasiokuwa na vyeti vya kidato cha nne. Naye katibu mkuu wa wizara ya Tamisemi, Mhandisi Mussa Iyombe, amesema kumekuwepo na changamoto mbalimbali zinazofanywa na maafisa wa utumishi katika halmashauri mbalimbali nchini.

UCHUMI WA MADINI UTAKUZA UCHUMI WA VIWANDA NCHINI.

Image
UCHUMI WA MADINI NA   UTASAIDIA UCHUMI WA VIWANDA TANZANIA.     Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Mhe John Pombe Magufuli.     Tanzania   ni nchi   iliyojaliwa   na utajiri mkubwa   wa madini   ya aina mbalimbali kama   yenye thamani kubwa kama ,Dhahabu,Fedha,Chuma,zink,Shaba,Nikel,bati Urani na mengine mengi. Wawekezaji wamekuwa   wakifutiwa na kubembelezwa kujakuwekeza   nchini katika sekta ya madini   ili   nchi iweze kuendelea ,uchumi wa madini ilianza kusikika   kuanzia miaka ya themanini,kufuatia   ongozeko   la ushiriki   wa wawekezaji   wa kigeni   katika sekta hii ya madini. Tangu mwanzo   ni kwamba madini   yalitumika   kwa kiasi   kikubwa katika   uzalishaji     viwandani hasa kwa   mawe yenye madini.na sehemu muhimu ya biashara ya ndani   na kimataifa,madini yenye   manufaa kiuchumi ambayo   si   metali ni   grafati,baadhi feldisipa,kwatzi,almasi na chembechembe nyingi   ningene zenye   thamani kubwa kutokana na umuhimu wake kimatumizi.