Posts

Showing posts from June, 2012

DR ,ULIMBOKA AOKOTWA PORINI AKIWA HOI.

Image
1 digg Dk Ulimboka Mwenyekiti wa Jumuiya ya madaktari  nchini, Dk Stephen Ulimboka amelazwa katika hospital ya Taifa ya Muhimbili baada ya kuokotwa katika pori la Pande nje kidogo ya jiji akiwa taaban.Inasemekana Dk Ulimboka alitekwa jana na watu wasiojulikana.  kwa taarifa zaidi soma gazeti la mwananchi kwa taarifa zaidi.

MKUU WA WILAYA AHIDI KUJIUZULU AKISHIDWA KUPAMABANA NA RUSHWA

  Na Noel stphen mpwapwa ..   MKUU WA WILAYA ya   Mpwapwa bawana   CHRISTOPHER KANGOYE ameahidi   na amesema yuko tayari kujuuzuru ukuu wa wilaya kama   endapo atamkamata mtu yeyote na rushwa   harafu huyo mtu asijukuliwe hatua za kisheria na vyombo vinavyo husika.   Bwana Kangoye ameyasema hayo   mwishoni   mwa wiki   wilayani mpwapwa alipo kuwa akifungua   mjadala   wa wazi   wa Tasisi ya Kuzuia na kupambana   na Rushwa Wilayani hapo mkoni Dodoma   (PCCB)   Alisema kuwa yeye amekuja wilayani mpwapwa kwa   ajili ya kuwatumikia wana mpwapwa na   sio kutumikiwa na wana mpwapwa,   hivyo alisema hapendi kusikia   malalamiko ya wanancjhi juu ya   kunyanyaswa na baadhi ya watendaji wa serikali na tasisi zake kwa kuombwa rushwa kwenye haki zao za msingi kama   afya   elimu maji   na utumishi. Aalisema   kuwa umaskini haiuwezi kuondoka kwa kuendekeza   rushwa na kufichaficha   mambo kwa kulindana kwa baadhi ya watendaji wa serikali pindi    mtu apatikanapo na   tuhuma za rushwa au   ubad

BILIONI 300 ZA VIGOGO ZATIKISA NCHI,

Image
Bilioni 300 za vigogo Uswisi zatikisa nchi  Send to a friend Tuesday, 26 June 2012 21:38 0 digg ZITTO AMTAKA PINDA ATAJE WAHUSIKA, WANANCHI WATAKA FEDHA ZIREJESHWE, MABILIONI ZAIDI YAIBWA MTANDAONI KUBAINIKA kwa Sh303.7 bilioni zilizofichwa katika akaunti za vigogo wa Serikali na wanasiasa nchini Uswisi, kumetikisa nchi huku shinikizo likitolewa kwa vyombo vya dola kuchunguza haraka na kuchukua hatua za kisheria, ikiwamo kurejesha fedha hizo. Jana kutwa nzima, gazeti hili lilipokea simu kadhaa kutoka kwa wasomaji wake wakiwamo wabunge na mawaziri, huku baadhi wakichangia maoni kwenye tovuti na mtandao mbalimbali ya kijamii, wakitaka kujua majina ya wamiliki wa akaunti hizo. Bungeni mjini Dodoma, Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe aliitaka Serikali kuchunguza tuhuma hizo kisha kuwachukulia hatua watu sita wanaotajwa kwamba wanamiliki akaunti zenye mabilioni hayo ya shilingi chini Uswisi. Fedha hizo zimebainishwa na

ASASI ZA KIRAIA ZA LALAMIKIWA KUTO KFIKIA MALENGO.

Na  noel Stephen Mpwapwa I mebainika kuwa  Asssi za kiraia  nchini  japo kuwa  zimefanya kazi kubwa kwa jamii na  serikali lakini bado hajijafikia malengo yanayo takiwa kutokana na rasilimali zilizo tumika na matokeo yanayo onekana.    H ayo yamebainishwa  na  Bwana  AYUBU KUPONA  afisa mipango kitengo cha Sera  na  Maendeleo katika ukumbi wa  Hoteli ya Blue Pearl mjini  Dar –ES-Salaam  alipo kuwa   akifungua  warsha ya  watendaji Wakuu wa AZAKI TANZANIA. Bwana kupona  alisema kuwa  japo kuwa asasi nyingi  zimefanya kazi   nchini bado  kuna changomoto ya kuyafikia malengo  yaliyo kusudiwa  ingawa pesa nyingi imetumika katika kitengo hicho kitu alicho sema kuwa matokeo haya endani  na kiwango cha rasilimali zilizo tumika . Aidha alidai kuwa   asasi nyingi nchini bado hazijafanya kazi za kufuatilia  mambo makuu ya  kitaifa  ili kuweza  kuleta  mabadiliko yanayo mgusa mlegwa wa hali ya chini TANZANIA. Pia alidai kuwa  yapo mabadiliko ambayo yanaonekana  kwa jamii na kuleta matokea  yan

MATATANI KWA DAWA ZA DILI

Na   noel   Stephen Mpwapwa Jeshi la Polisi Wilayani Mpwapwa Linamshikilia mfanya biashara mmoja wa kijiji cha Ng’hambi Bwana   Jeremia mhogo   kwa tuhuma za kukamatwa na dawa za kutibu binadamu      na   baadhi ya dawa hizo zikiwa na nembo ya MSD   kinyume na sheria.   MKUU wa polisi   wilayani mpwapwa   Bwana   JEREMIA SHILA   ametibitisha kutokea kwa tukio hilo na amesema mtuhumiwa bado anashikiliwa na polisi lakini kwa sasa yuko nje kwa dhamana . Bwana Shila   alisema kuwa   mtuhumiwa huyo alikamatwa na maafisa AFYA   WA WILAYA    walio enda   kufanaya uchunguzi katika eneo hilo na ndipo walio   mbaini mtuhumiwa huyo na alisema kuwa   maelezo mazuri anayo bwana afya wa wilaya     Bwana Plaivate Lweimamu amabae alikuwa ndiye mkuu wa msafara siku hiyo na kuwataka waandishi kwenda   kwa Bwana afya kupata maelezo kwa bwana AFYA HUYO.   Akiulizwa bwana LWEIMAMU   kuhusu tuhuma hiyo   bwana Afya   huyo    aliwafukuza   waandishi wahabari kwa madai kuwa   waandishi hao waandike   wa

BAJETI YATANGAZWA V2012 V2013

Image
MCL The Citizen Mwanaspoti Nation Monitor Digital Paper East Africa News Ingia Mwanzo Contacts Email Habari Kubwa Fri 15 June 1:17AM   Mwanzo Habari Biashara Michezo Burudani Ajira Uchambuzi Jumapili Makala Picha Tangaza Kipanya RSS Home BOOKMARK THIS PAGE Bajeti  Send to a friend Thursday, 14 June 2012 22:03 0 digg Waziri wa Fedha, Dk William Mgimwa akionyesha begi lililobeba hotuba ya bajeti ya serikali kwa mwaka wa fedha 2012/2013, wakati akielekea kuingia katika ukumbi wa Bunge, mjini Dodoma jana. Picha na Edwin Mjwahuzi Mussa Juma, Dodoma SERIKALI jana ilitangaza Bajeti ya Sh15trilioni kwa mwaka wa fedha 2012/2013 ambayo pamoja na mambo mengine, imelenga kudhibiti mfumuko wa bei kwa kutangaza kutoa vibali vya kuingiza chakula kutoka nje, huku ikiwabana matajiri kwa kuongeza kodi ya bidhaa zisizo

TAFADHALI MADAKATARI ,VIONGOZI MSIYAPUUZE

Image
MIONGONI mwa habari zilizopo ukurasa wa mbele wa gazeti hili, ni tishio la Chama cha Madaktari Tanzania (MAT) la kufanya mgomo usio na kikomo wiki mbili zijazo, iwapo serikali itashindwa kuyapatia ufumbuzi madai yao ya msingi, ikiwemo nyongeza ya mshahara. Tumeshtushwa na tishio hilo kwa kuwa bado hatujasahau madhara yaliyotokea wakati wa migomo ya Januari na Machi mwaka huu, ambapo watu waliokwenda kwenye hospitali, zahanati na vituo vya afya vya umma kupata matibabu na huduma nyinginezo hawakuzipata. Wapo watu waliopoteza maisha, waliopata vilema vya maisha na athari nyingine nyingi ambazo mpaka hivi sasa serikali imeshindwa kutaja migomo ile iliathiri kwa kiwango gani sekta ya afya. Tunaamini kuwa, tishio hili la madaktari linaweza kufanyiwa kazi kabla ya wiki hizo mbili ili kuepusha hali kama ile tuliyoshuhudia huko nyuma, ambapo pia baadhi ya viongozi na watendaji wa walisimamishwa kazi huku wengine wakipoteza nyadhifa z

POLISI WAJIPANGA KUUKABILI UHARIFU

Image
Na Omana Gouth MPWAPWA Jeshi la polisi wilaya ya mpwapwa linakusudia kutekeleza miradi miwili kwa kuwashirikisha wananchi kwa kuanzisha mtandao wa kiusalama na mpango wa   akiba ya mafuta kwa lengo la kukabiliana na uharifu wilayani humo. Hayo yamesemwa na mkuu wa polisi wilaya ya Mpwapwa Bwana Jeremia Shila katika kikao cha baraza la madiwani kilicho fanyika katika ukumbi wa halmashauri ya wilayani Mpwapwa mkoa wa Dodoma Pia alisema   katika eneo la Mpwapwa lazima waondokane na mifumo ya kizamani wa ulinzi wa kutegemea baiskeli na kutembea kwa miguu, na sasa wanaingia katika mfumo wa kutumia pikipiki kwa kila kijiji na kata. Akizungumza   kwenye kikao hicho Bwana Shila   alisema   kila kijiji kitapatiwa pikipiki moja na kata kupewa pikipiki moja ya polisi kata, na vijana wawili kupatiwa mafunzo kwa kila kijiji na pia kupatiwa mawasiliano ya simu ili kurahisisha dhana ya polisi   jamii. Aidha   alisema mpango huu utasaidia endapo tukio la uhalifu likitokea katika kijiji kimoja  

WATUMISHI WA HALMASAURI WAISABABISIA HALMASHAURI HASARA YA MIL36

Image
Mpwapwa BAADHI ya watumishi wa Halmashauri ya Mpwapwa, wameisababishia hasara ya shilingi 36,720,000 kwa mwaka kutokana na kukwepa kulipa ushuru wa vibanda 153 vya biashara wanavyomiliki. Hasara hiyo ilibainishwa mwishoni mwa wiki kwenye kikao cha kawaida cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo ilidaiwa watumishi wanaomiliki vibanda vya biashara wameshindwa kulipa ushuru na hawajachukuliwa hatua za kisheria. Diwani wa Kata ya Kimagali, Matuluh Kuchela (CCM), alimtaka Mwenyekiti wa Halmashauri, Alexander Nyaulingo kutoa maelezo ni kwanini baadhi ya watumishi wanaomiliki vibanda hawalipi ushuru ilhali wanajulikana. Kuchela alisema wakati halmashauri ikiendelea kulalamika kwa kushindwa kukusanya mapato katika maeneo mbalimbali, wapo watumishi ambao wanamiliki vibanda na hawalipi ushuru kwa makusudi. Alisema inaonesha baadhi ya watumishi wa halmashauri hiyo ambao wamamiliki vibanda wanaisababishia hasara halmashauri ya

CCM WAHAHA WAWAKUSANYA WANACHAMA KWA MAROLI

• Yakusanya watu kwa maroli mkutanoni na Chalila Kibuda VIGOGO na makada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) jana walilazimika kutumia jitihada za ziada kuhakikisha mkutano wake unaufunika ule uliofanywa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wiki mbili zilizopita. Miongoni mwa jitihada hizo, ni kuwapa fursa Waziri wa Ujenzi, Dk. Harisson Mwakyembe, Waziri wa Miundombinu, Dk. John Magufuli, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka na wengine kuzungumzia mazuri yaliyofanywa na chama hicho ambayo yanadhihakiwa na wapinzani. Mwakyembe alitumia mkutano huo kuelezea madudu aliyoyakuta kwenye wizara anayoiongoza, ambayo kwa kiasi kikubwa yamesababishwa na udhaifu wa serikali ya chama chake ambayo kwa muda mrefu imekuwa na utaratibu wa kulindana, kubebana na kufumbia maovu. Alisema tayari ameanza kazi kwa kasi na ameomba apewe miezi mitatu kuishughulikia Mamlaka ya Bandari kwani amepata taarifa kuna madudu mengi ambayo yanasababisha serikali kukosa

SINA MPANGO NA CHADEMA.

Image
0 digg Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye Dotto Kahindi na Leon Bahati KATIBU wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye amesema chama chake hakina mpango wa kuutumia mkutano wake wa leo kwenye Viwanja vya Jangwani kujibizana na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na badala yake, kitajikita zaidi katika kutoa somo kwa wajumbe wapya wa mashina na viongozi wa matawi Mkoa wa Dar es Salaam. Kauli hiyo ya Nape inatoa mtazamo tofauti na tetesi kwamba  CCM kitatumia mkutano huo kukijibu chama hicho kikuu cha upinzani ambacho nacho kilifanya mkutano kwenye viwanja hivyo hivi karibuni. Katika mkutano huo ambao Chadema kilizindua Mpango wake wa Vuguvugu la Mabadiliko (M4C) mwishoni mwa mwezi uliopita, kiliorodhesha shutuma nyingi dhidi ya Serikali ya CCM zikiwemo za kusababisha maisha magumu kwa Watanzania. Nape alisema mkutano huo uliandaliwa na CCM Mkoa wa Dar es Salaam hata kabla ya huo wa Chadema na lengo lak

MWASISI WA CHADEMA AFARIKI DUNIA

Image
0 digg Mzee Bob Makani Na Mwandishi Wetu MWASISI wa Chadema na Mwanasheria mkongwe nchini Bob Makani, amefariki dunia usiku katika hospitali ya Aga khan, jijini Dar es Salaam. Habari zilizopatikana na kuthibitishwa na Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe, Makani alizidiwa ghafla saa 3: 00 usiku wa kuamkia leo na kukimbizwa katika Hospitali ya Aga Khan ambako alifariki dunia saa 4.15 usiku. “Amekuwa anaumwa muda mrefu, mara kadhaa akipelekwa hospitali na baada ya muda anaruhusiwa, lakini hii ya sasa alikua nyumbani akazidiwa ghafla wakampeleka hospitali na ilipofika saa 4.15 wakasema amefariki,” alisema Zitto. Zitto alisema kuwa, suala la wapi utakapozikwa Makani ambaye ni Katibu Mkuu wa Kwanza na Mwenyekiti wa pili wa Chadema, litajulikana baada ya kujadiliana na familia ya marehemu. “Suala la wapi atazikwa kama ni Shinyanga ama Dar es Salaam, litajulikana baada ya kuzungumza na familia yake, kwa sasa tunashughulika kwanza na kuhifadhi mwili wa mzee wetu,”

AMUUNGUZA WIFI YAKE SEHEMU ZA SIRI.

KATIKA hali ya kushangaza na kusikitisha,mkazi wa moshi bar Manispaa ya Ilala,amedaiwa kumuunguza  wifi yake( 15) sehemu zake za siri  na kumsababishia maumivu makali. Hayo yametokea jana Jijini Dar es Salaam, baada ya askari polisi wa kituo cha Stakishari, kupokea taarifa kutoka kwa majirani juu ya unyama huo aliofanyiwa binti huyo. Polisi hao mara baada ya kupata taarifa hiyo, walifika nyumbani kwa mtuhumiwa lakini iliwachukua zaidi ya saa mbili kufanikiwa  kumtoa ndani mtuhumiwa ambaye alidaiwa kujifungia. Hata hivyo, hali ilikuwa tete baada ya wakazi na majirani  wa eneo hilo walioguswa na tukio , walipoamua kuvamia nyumba hiyo baada ya kupokea taarifa za uongo kuwa mtuhumiwa hayupo  na kuamua kuwashinikiza polisi wamtoe au wajichukulie sheria mkononi. Kufuatia mvutano huo, Polisi waliofika kumchukua mtuhumiwa , walizidiwa na kuamua kuondoka  kwa lengo la kwenda kuongeza nguvu kwa kuongeza askari na mabomu ya kurusha ili kuweza kuwatanya wananchi waliokuwa na

MAPACHA WALIO UNGANA WAFARIKI DUNIA

WATOTO mapacha walioungana waliozaliwa juzi katika hospitali ya Muhimbili wamefariki dunia usiku wa kuamkia jana katika hospitali ya Taifa Muhimbili. Watoto hao walioungana kuanzia kifuani walikuwa na jinsi moja ya kike na miguu miwili, lakini katika eneo la juu walikuwa na vichwa viwili na mikono minne. Akizungumza ofisini kwake, Daktari bingwa wa watoto, Augustine Massawe alisema watoto hao wamefariki kabla ya kufanyiwa vipimo ambavyo vingeeleza uhusiano mzima wa kimaumbile. “Hawa ni mapacha walioungana, ni watoto wawili ambao sehemu ya tumbo na kifua havikutengana wakati wa ukuaji akiwa kwenye mfuko wa uzazi, na mara nyingi watoto kama hawa huzaliwa kwa upasuaji,” alisema. Alieleza kwamba kitaalamu watoto hao huitwa ‘Conjoined twins’ ambao hutengenezwa kwenye mfuko mmja na hutumia kondo moja kwa kila kitu katika kupata mahitaji kutoka mama, pia iwapo wangeendelea kuwa hai pengine wangekuwa na matatizo ya ubongo. Dk Massawe alisema kuzaliwa kwa watoto wa aina

GAZETI LA MWANACHI LAPONGEZWA

Image
0 digg Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi,Philip Mulugo akiwapongeza baadhi ya Wanafunzi wanne kati ya 100 wa Mpango wa Elimu wa Paa na Mwananchi wakati hafla ya kuwakabidhi hati za ufadhiri wa Masomo iliyofanyika kwenye Ofisi za MCL zilizopo Tabata jijini Dar es Salaam jana.Picha na Fidelis Felix Ibrahim Yamola NAIBU Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo amezitaka kampuni mbalimbali nchini kuiga mfano wa Mwananchi Communications Limited (MCL), kwa kutoa udhamini kwa wanafunzi nchini ili wapate elimu. MCL, kampuni inayochapisha magazeti ya Mwananchi, Mwanaspoti na The Citizen imeanzisha mpango maalumu wa kusaidia ukuaji wa elimu kwa kuwafadhili wanafunzi katika shule za umma kuanzia kidato cha kwanza hadi cha nne ikianza na wanafunzi 100 kutoka sehemu mbalimbali za Tanzania.Akizindua mpango huo katika Ofisi za MCL, Tabata Dar es Salaam jana, Waziri Mulugo alisema hatua hiyo ni ya kuigwa kwani Serikali haiwezi kufanya kila kitu bila msaada wa

KUKAMATWA KWA BADWELI NI UTATA MTUPU

Image
Kigoma Kusini, David Kafulila ameilipua Kamati ya Bunge ya Serikali za Mitaa (LAAC) kuwa imekithiri kwa rushwa. Kutokana na tuhuma hizo, Kafulila amemtaka Spika wa Bunge, Anne Makinda kuvunja kamati hiyo, vinginevyo yeye atajiondoa. Pia mbunge huyo ameitaka Kamati ya Maadili kulitumia Bunge kumvua ubunge, Badwel, kutokana na tuhuma za kupokea rushwa zinazomkabili. Kafulila alisema hayo jijini Dar es Salaam jana alipozungumza na waandishi wa habari huku akisisitiza kuwa, wananchi hawatakuwa na imani tena na kamati hiyo. “Ikumbukwe Juni 13, 2011 nilieleza bungeni namna wabunge wa Kamati ya LAAC wanavyoomba rushwa kwa watumishi wa Serikali, huku nikimtaja kwa jina Mbunge wa Bahi, Omary Badwel kuwa ni miongoni mwao,” alisema Kafulila ambaye pia ni mjumbe wa kamati hiyo. Mkurugenzi wa Idara ya Upelelezi ya Takukuru, Alex Mfungo alisema juzi kuwa mbunge huyo anatarajiwa kufikishwa mahakamani leo. Hata hivyo, Spika wa Bunge, Anne Makinda alisema hana taarifa zozote za mbun