DC MPWAPWA AWAHADHARISHA WAKULIMA PWAGA.



Mkuu wa wilaya ya mpwapwa mkoani Dodoma  bwana Jabiri Shakimweri  amewataka wananchi  wa vijiji vya Pwaga na Mingui  kuto kuuza ardhi kiholela hasa katika kipindi hiki cha ujio wa serikali mkoani Dodoma
Shakimweri aliyasema hayo juzi alipokuwa akifungua mafunzo ya  kwa wakulima wa vijiji vya pwaga  na Mingui wilayani Mpwapwa yaliyofadhiliwa na Mpango wa kurasimisha rasilimali na biashara za wanyonge  (MKURABITA) juu ya kuweza kuitumia ardhi kama  rasilimali muhimu kwa maendeleo ya mtu mmoja mmoja na  Taifa kwa ujumla.
Aidha Shakimweri amesema kuwa mala baada ya serikali kuanza kuhamia Dodoma kumeibuka baadhi ya watu  wanao zunguka katika wilaya zote za mkoa Dodoma  kununua maeneo ya watu kwa bei nafuu  na kuwaacha  wakazi wa maeneo hayo  katika hali ya umaskini  na kutishia kuwapo katika  mogohoro ya ardhi.
Mkuu wa wilaya hiyo amesema lazima wanannchi hao  kuweza kutumia fursa za  hati za kimila za ardhi  kwa kuweza kuongeza dhamani ya ardhi  kwa kupanda mazao ya biashara ya muda mrefu  kama  korosho  ambayo imeonekana kufanya vizuri  katika wilaya ya Mpwapwa.
Kwa upande wake Meneja wa urasimishaji ardhi  kutoka katika ofisi ya Rais  bwana Anton Mushi amesema  wamepanga maffunzo hayo kwa wakulima wa pwaga na Mingui kutokana na  vijiji hivyo ni miongoni wa vijiji vilivyofanyiwiwa Mpango wa matumizi  bora  ya ardhi  na kupatiwa hati za kimila .
 Mushi  amesema  kuwa lengo la mkurabita  ni kuweza kulasimisha  rasilimali  na biashara za wanyonge Tanzania katika kijiji cha pwaga ikiwa ni kutenga na kupima maeneo ya kijiji kwa ajili ya shughuli mbalimbali za kiuchumi na matumizi bora  ya ardhi.
Hata hivyo Mushi  alisema kuwa ardhi ni moja wapo ya rasilimali kuu ya na muhimu kama ikitumika inavyotakikana hasa kwa kilimo kitaweza kubadilisha  hali ya kipato cha watanzania na nchini.
Mwenye kiti  wa kijiji  cha Pwaga bwana Msemakweli Chahonza ameongeza kuwa jumla ya mashamaba 1277 yamepimwa na tayari hati  1031 hati     za kimila zimekabithiwa kwa wananchi wa Pwaga ambao wataweza kutumia hati hizo kama fulsa  kama dhamana ya kuaminika kwa mkulima na kupelekea  kubadilisha maisha  ya mkulima mdogo.


.


Comments

Popular posts from this blog

KIZIGO AWAPONGEZA RUWASA,AKERWA NA UHARIBIFU WA MAZINGIRA,AWATAJA MADIWANI.

HISTORIA YA MPWAPWA HATARINI KUTOWEKA

DC KIZIGO ATOA MAAGIZO KWA KWA MAAFISA ELIMU KUKABILIANA NA UKATILI MASHULENI.