AKINA MAMA WAJIFUNGULIA MAJUMBANI BAHI.

AKINA mama wajawazito wapata 47 katika kata ya mpalanga Wilaya ya Bahi Mkoani Dodoma wametajwa kujifungulia nyumbani katika kipindi cha kuanzia mwezi july hadi septemba mwaka huu jambo linalohatarisha maisha ya mama na mtoto.

Zipo sababu mbalimbali ambazo zinatajwa kupelekea akina mama wajawazito kutojifungulia katika zahanati na vituo vya afya ikiwa ni pamoja ni huduma hiyo kukosekana katika baadhi ya vijiji,miundombinu kutokuwa rafiki na pengine kupelekea akana mama hao hujifungulia njiani.

akisoma taarifa ya utekelezaji wa shughuli za maendeleo katika kikao cha baraza la madiwani wa halmashsuri hiyo cha robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2017/18, diwani wa kata hiyo Daudi Magalamile amesema kuwa sababu hizo zimekuwa ni changamoto katika maeneo yao.

Diwani huyo amesema hapo awali kulikuwa na utaratibu wa kuwatoza faini akina ambao wanajifungulia nyumba ambao utaratibu huo uliwafanya akina mama hao kujifungulia katika vituo vya afya na zahanati lakini baada ya kuondolewa faini hiyo akina mama wengi wamekuwa wakijifungulia nyumba.


Kufuatia changamoto hiyo diwani huo ameeleza juhudi na hatua za ujenzi wa zahanati katika kijiji cha chililo zilianzishwa lengo ikiwa ni kutatua tatizo hilo licha ya kuwa ujenzi wa kituo hicho umekuwa wa kusuasua.


Kutokana na kusuasua kwa ujenzi huo mwenyekiti wa halmashauri ya Wilaya ya Bahi Danford Chisomi akaahidi kuchangia mifuko 10 ya saruji ili kusaidia ukamilishaji wa zahanati hiyo.

Kwa upande wake diwani wa kata ya ibugule Blandina Magawa amemtupia lawama muuguzi wa zahanati ya kijiji cha ng,ome kwa kushindwa kuwahudumia akina mama wajawazito na kupelekea kujifungulia nje ya zahanati hivyo kuomba halmashauri kuwatafutia mganga mwingine.


Ili kukabiliana na changamoto hiyo serikali na wadau mbalimbali wa afya wana kila sababu ya kuchukua hatua madhubuti za kuendelea kupunguza tatizo la akina mama kujifungulia nyumbani au njiani ili kuweze kupunguza vifo vya mama na mtoto.
Mwisho.

Quick Reply


Comments

Popular posts from this blog

KIZIGO AWAPONGEZA RUWASA,AKERWA NA UHARIBIFU WA MAZINGIRA,AWATAJA MADIWANI.

HISTORIA YA MPWAPWA HATARINI KUTOWEKA

DC KIZIGO ATOA MAAGIZO KWA KWA MAAFISA ELIMU KUKABILIANA NA UKATILI MASHULENI.