WAKUU WA MIKOA WAPEWA CHANGAMOTO .JAFFO




Waziri wa nchi ofisi ya Rais Tawala za mikoa na serikali za mitaa TAMISEMI
Selemani Jaffo amewaagiza wakuu wa mikoa nchini kuhakikisha wanaandaa
miundombinu ya elimu ya kutosha katika mikoa yao ili wanafunzi waliofaulu
mtihani wa darasa la saba na kupata nafasi ya kujiunga na kidato cha kwanza
january 2018 wanapata nafasi hiyo.

Akizungumza mjini dodoma Waziri wa Tamisemi Seleman Jaffo amesema kufuatia
kuongezeka kwa ufaulu wa  asilimia 72.76 kwa wanafunzi waliofaulu mtihani
wa darasa la saba ofisi yake haina budi kutoa maelekezo hayo ili maandalizi
yaweze kufanyika mapema.

Kuhusiana na kushuka kwa Somo la kingereza Waziri Jafo anatoa maelekezo.

Katika hatia nyingine Waziri Jaffo amewataka makatibu tawala wa mikoa na
wakurugenzi wahalmashauri zote nchini kuwapokea watumishi 2058 wa sekta ya
afya ambao wamepangiwa vituovya kazi  kwa kuwapatia stahiki zao.

Watumishi waliopangwa wanatakiwa kuripoti katika vituo vyao vya kazi ndani
ya siku 14



MWISHO.


Comments

Popular posts from this blog

KIZIGO AWAPONGEZA RUWASA,AKERWA NA UHARIBIFU WA MAZINGIRA,AWATAJA MADIWANI.

HISTORIA YA MPWAPWA HATARINI KUTOWEKA

DC KIZIGO ATOA MAAGIZO KWA KWA MAAFISA ELIMU KUKABILIANA NA UKATILI MASHULENI.