WANANCHI WALALAMIKIA HUDUMA HAFIFU TANESCO MPWAPWA.







WANANCHI wa wilaya ya Mpwapwa  mkoani Dodoma  wamelalamikia huduma duni na hafifu za shirika la  ugavi la umeme TANESCO  wilayani hapa kuwa zinawarudisha nyuma kimaendeleo
Wananchi hao waliyoataoa malalamiko yao walipo kuwa wakiongea na mwandishi wa habari  juu ya kuto ridhishwa na huduma zitolewazo na shirika hilo kuwa  zimekuwa za  kusuasua na huchukua muda mrefu kushughulikiwa kero zao kitu  walicho kisema kuwa  kinachangia kudumaza uchumi na maendeleo ya watu wa Mpwapwa.
Mmoja  wa wananchi  wa wilaya hiyo bwana AHMAD UTAMU  alisema kumekuwa na ubabaishaji wa  ujazaji wa ramani pindi unaomba   huduma za kuunganishiwa  umeme ndani ya nyumba,kukatika katika kwa umeme mara kwa mara  kunakopelekea baadhi ya watu kuunguza vitu vyao na kuwasababishia hasara kubwa.
Aidha bwana Ahmad  alisema kuwa  shirika hilo limekuwa likikiuka mkataba wa huduma kwa mteja ambao unalitaka kutoa taarifa  kwa wateja wao pindi umeme utapo katika  na sababu zinazo pelekea kukatika katika kwa umeme.
“Yaani kwa Mpwapwa imekuwa tofauti  yaani mvua kidogo tu umeme umekatika  na hawa watu wa Tanesco hawatoi taarifa hadi siku tatu umeme unakatika bila taarifa huku wateja tukibaki katika sintofahamu ya nini kinaendelea na ukirudi uanarudi kimyakimya na kupelekea vitu vya watu kungua”aliongea Bwana Ahmad
Meneja wa shirika hilo wilaya Mpwapwa Bwana BEATUS KEBWE amekili kuwepo kwa baadhi ya changamoto zinazo ikabili ofisi yake kitu alicho sema changamoto hizo zinasababishwa na  uchache wa watumishi,vitendea kazi  na umbali na jografia ya mpwapwa  kunapelekea kuwapo kwa malalamiko mengi ya wateja.
Aidha Kebwe alisema kuwa “kwa wilaya yangu kijiji cha mwisho ninacho kihudumia  ni umbali wa kilomita 150 kijiji cha Malolo   kwa hiyo tatizo likitokea kule ni ngumu kuliatend kwa wakati kwa kuzingati hatuna magari ya kutosha  lakini pia hata watumishi”alifafanua bwana Kebwe.
Hata hivyo meneja huyo alisema ili kuweza kupunguza  changamoto hizo shirika la Tanesco wialayani hapo limekusudia  kuanzisha  Dawati la huduma ambalo itakuwa ni madwati yatakayo kuwa yanapatika karibu na  wateja  huko kijiji kila kata lazima kutakuwa na dawati la huduma.
Pia alisema  wanampango wa kupanua huduma kwa wateja kwa kufungua ofisi zingine za  Taneco katika   tarafa ya Kibakwe,kijiji cha Chipogoro na kata ya kinusi lengo lake likiwa kusogeza huduma zaidi kwa wananchi.

Comments

Popular posts from this blog

KIZIGO AWAPONGEZA RUWASA,AKERWA NA UHARIBIFU WA MAZINGIRA,AWATAJA MADIWANI.

HISTORIA YA MPWAPWA HATARINI KUTOWEKA

DC KIZIGO ATOA MAAGIZO KWA KWA MAAFISA ELIMU KUKABILIANA NA UKATILI MASHULENI.