CHAMA CHA WAAANDISHI DODOMA CHASHAURIWA KUJIPANGA KUPOKEA MAKAO MAKUU,


MSEMAJI wa Serikali na Mkurugenzi wa Idara ya Habari maelezo Dkt Hassan Abbas amekitaka chama cha waandishi wa habari club ya waandishi wa Habari ya Mkoa wa Dodoma (CPC) kujipange vyema kuhudumia taifa la Tanzania na mataifa mengine kwa kuwapatia habari ambazo hazila viashairia vya uchochezi.

Dkt Abbas ameyasema hayo mjini Dodoma wakati akiongea na wanachama wa chama cha waandishi wa habari mkoani Dodoma katika mkutano wao mkuu uliofanyika mjini Dodoma hapa na kusema (CPC) inatakiwa ijipange vyema kuhudumia serekali kwa kuwa na waandishi wa habarai wenye kufuata misingi ya taaluma yao.


Katika kufanikisha hilo, Dkt Abbas ambaye pia ni muumini wa tasnia ya habari amewakikishia wana CPC kufanya nao kazi wakati wote na idara ya habari maelezo itasaidia mafunzo mbalimbali kwa waandishi wa habari.



Katika kuhakikisha kuwa hilo linafanyika
Kwa uande wake Mkuu wa mkoa wa dodoma Dr. Binilith Mahenge akizungumza wakati wa akifungua mkutano huo akawataka waandishi wa habari nchini kulitanguliza taifa la Tanzania katika hughuli zao za kila siku.



Mwenyekiti wa CPC Habel Chidawali kwa niaba ya wana CPC wote, amemshukuru Mkurugenzi wa Habari Pamoja na mkuu wa mkoa wa dodoma kwa dhamira njema ya kutaka kuisaidia CPC na kuahidi kuyazingatia yote yaliyozungumzwa katika mkutano huo.

.

Comments

Popular posts from this blog

KIZIGO AWAPONGEZA RUWASA,AKERWA NA UHARIBIFU WA MAZINGIRA,AWATAJA MADIWANI.

HISTORIA YA MPWAPWA HATARINI KUTOWEKA

DC KIZIGO ATOA MAAGIZO KWA KWA MAAFISA ELIMU KUKABILIANA NA UKATILI MASHULENI.