POLISI WABAINI KUWA NABII TITO NI MGONJWA WA AKILI,

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma,Gilles Muroto amesema kuwa katika
uchungizi wa awali uliofanywa imebaini kuwa Titto Onesimo Machibya (44)
anayejiita Nabii Titto anasumbuliwa na matatizo ya akili.


Nabii Titto ambaye ni mkazi wa kijiji cha Ng’ong’ona Manispaa ya dodoma
alikamatwa na jeshi la polisi baada ya kurekodiwa kwa picha za video na
kuanza kusambazwa kwenye mitandao ya kijamii jambo ambalo ni kinyume na
kifungu cha sheria namba 129 cha kanuni ya adhabu sura ya 16 kilichofanyiwa
marekebisho mwaka 2002.


Nabii Titto amekuwa akitumia vibaya kitabu cha Biblia kwa kutoa tafsiri za
upotoshaji ,pia amekuwa akifanya vitendo vya udhalilishaji hadharani na
kuchochea maovu katika jamii kwa akishirikiana na wanawake wawili wanaodawa
ni wake zake pamoja na mtumishi wake wa ndani.


Akizungumza na Waandishi wa Habari leo Mjini hapa,Kamanda wa Polisi Mkoa wa
Dodoma,Gilles Muroto amesema kuwa Nabii Titto aliwahi kupatiwa matibabu
katika hospitali ya mhimbili atiwa anasumbuliwa na matatio ya akili.



Amesema kuwa kutokana na vitendo ambavyo vimekuwa vikifanywa na mtu huyo
baada ya kumkamata januari 16 mwaka huu jeshi hilo lililazimika kumpeleka
hospitali ya mirembe iliyopo mjini hapa kwa lengo la kumchunguza matitizo

Comments

Popular posts from this blog

KIZIGO AWAPONGEZA RUWASA,AKERWA NA UHARIBIFU WA MAZINGIRA,AWATAJA MADIWANI.

HISTORIA YA MPWAPWA HATARINI KUTOWEKA

DC KIZIGO ATOA MAAGIZO KWA KWA MAAFISA ELIMU KUKABILIANA NA UKATILI MASHULENI.