WASTAFU WALIA KUKOSA UMOJA



 
Katibu wa  chama cha walimu wilayani Mpwapwa mkoani Dodoma  bwana Pankras Ngamesha ameiomba serikali ya awamu ya tano kuwachukulia hatua waajili wanaozembea kuwasilisha michango ya makato katika mifuko ya pesheni hapa nchini
Ngamesha  alitoa kauli hiyo  alipokuwa akiongea katika hafla ya kuwashika mkono wa pongezi walimu 34 wa wilaya ya mpwapwa mkoa wa Dodoma  walio stafu  utumishi wao  mwezi march na mwezi mei mwaka 2016.
Ngamesha alisema kumekuwako na chanagamoto kubwa kwa wastafau kuishi maisha magumu mala baada ya kumaliza utumishi wao serikali kutokana na kucheleweshewa  mafaoa yao kutoka katika mifuko ya hifadhi ya jamii  (PSPF).
Aidha  Ngamesha aliwakabidhi  bati 20 kila mmoja walimu kumi  waliostafu ambao walikuwa wanachama wa chama cha walimu hapa  wilayani kama kuwashika mkono wa kwaheri na kutambua mchango wao wa kukutumikia chama hicho na serikali  kwa ujumla .
  Mwl Ngamesha alisema kuwa  kufuatia mabadiliko ya katiba ya chama cha walimu nchini mabadiliko ya 2014  ndio yaliyo zaa maazimio ya  utoaji wa mkono wa kwa heri  kwa wananchama wake walio tumikia  chama hicho  kwa muda  usio pungua miezi 180  au miaka 15.
Akisoma lisala ya wastafu kwa niaba ya walimu wenzake mwalimu  Mark  Maganza alisema  ili  kuondokana  na changamoto hiyo kwa walimu lazima chama hizo kufikirie kuanzisha  mfuko wa jamii ili kuweza kukabiliana na chanagamoto ya ucheleweshaji wa pensenkwa wastafu  wa fani ya ualimu  hapa  nchini
 Pia Maganza alisema pamoja na changamoto ya  na wastafu kucheleweshewa  mafao yao lakini pia kuna chanagamoto kubwa inayaowakabili wastafu ni  waajili kuto kuwasilisha michango yao katika mifuko ya jamii na hivyo kupelekea kupunguza pesheni ya mtumishi .
Hata hivyo Mangaza alisema kuwa  wastafu wameshidwa kuwa na sauti ya pamoja na kutoa malalamiko yao kutokana na kutokuwa na  chombo cha kitaaluma cha kuwasemea  wastafu  wa fani hiyo, hivyo kupelekea kila mmoja kuitafuta haki yake kivyake na  kusababisha kuingia kwenye rushwa ili kuweza kupata haki yao au kuwaishiwa mafao yake.
Pia aliiomba serikali kuweza kutoa mafao ya walimu kwa wakati  ambapo kwa sasa alisema huchukua muda wa miezi tisa hadi mwaka mmoja mtumishi anapo stafu kupata mafao yake kitu alicho kisema kuwa  kwa kucheleweshewa mafao yao kunaashiria mianya ya rishwa kwa wahusika
“Iweje mimi najiliwa serikali inajua nimeajiliwa na siku yangu ya kustafu wanaijua mala baada kustafu wanaanza kunisumbua kalete hiki mala hiki hii si nikujitengenezea mianya ya rushwa  tu na usumbufu usio na sababu “aliongea Mangaza.
 Kwa upande wake  mkurugenzi mtendaji wa halmasahauri ya wilaya ya Mpwapwa Bwana Mohamed  ilikili kudaiwa na walimu hao lakini alisema tayari amesha  anzakulipa  madeni ya walimu hao na alisema wataendelea kufanya hivyo kutokana na uwezo wa halmasahauri


Comments

Popular posts from this blog

KIZIGO AWAPONGEZA RUWASA,AKERWA NA UHARIBIFU WA MAZINGIRA,AWATAJA MADIWANI.

HISTORIA YA MPWAPWA HATARINI KUTOWEKA

DC KIZIGO ATOA MAAGIZO KWA KWA MAAFISA ELIMU KUKABILIANA NA UKATILI MASHULENI.