C WT YAPATA VIONGOZI WAPYA MPWAPWA.




CHAMA  chama cha walimu  wilayani mpwapwa mkoani DODOMA  kimepata  viongozi  wake wapya  watakao kiongoza chama hicho kwa  muda wa miaka mitano  toka sasa.


Viongozi hao waliopatikana kupitia  kuchaguliwa na mkutano mkuu wa chama hicho,  uliofanyika jana katika ukumbi wa  chuo cha walimu mpwapwa mjini hapa .
Akifungua  mktano huo mkuu wa wilaya ya mpwapwa  Dr Jasmini Tiisekwa   alisema ni vyema walimu hao wakatumia  haki yao  ya kikatiba,  kuwachagua  viongozi  wao  ambao  wataweza kushirikiana  katika  harakati za kumkomboa  mwalimu na katika kuweza kujiletea maendeleo endelevu.
Aidha  Dr, Tiisekwa  aliwaasa viongozi   wa chama cha walimu hao kuweza kusimamia haki na wajibu wa wanachama wao  ili kuweza  kupunguza hali ya kutishia kwa kutoweka kwa amani  hapa nchini  kwa madai ya kudai haki kwa migomo na maandamano.
Pai mkuu wa wilaya huyo  aliwataka walimu na wagombea hao kuweza kuendesha kampeni  za kistarabu  ili kuwa mfano wa kuigwa na makundi mengine ambayo wanaotumia demokrasi ya  kuchaguliwa  kwa kuto kubali  vitendo vya fujo ,matusi,na kejeli wakati wa kampeni.
Msimamizi wa uchaguzi  huyo Comred  Mwl David Kisamo alisema nafasi zinazogombewa ni  nafasi ya mwenyeki wa chama , mhasibu wa chama nafasi ya mwakilisi wa shule za sekondari, mwakilishi wa vijana na mwakilishi wa walemavu.
Nafasi nyingine alisema ni nafasi ya uwakilishi wa walimu shule ya msingi,uwakilishi wa nafasi ya  vyuo vya ualimu  na nafasi za tasisi za elimu na uongozi.
Katika matokeo hayo  Comred Mwl .Daniel  Tito  ndiye aliyechaguliwa  kuwa mwenyekiti na kuchukua mikoba ya aliye kuwa mwenyekiti wa chama hicho Richard Kipalamoto, nafasi ya mhasibu wa chama hcho ilichukuliwa na Mwl Kessi Kidifu aliyeitetea nafasi yake  kwa kumshinda mpinzani wake  mwl George Ntale.
Hata  hivyo nafasi ya  uwakilishi wa  shule za awali ulichukuliwa na mwalimu  Paskali Gailanga,nafasi ya uwakilishi wa nafasi za vijana  ulichaguliwa Faustine Chiwanga, nafasi ya uwakilishi wa walimu shule ya msingi  alichaguliwa mwl Samson Kempanju  na Albart Timatuku nawakati uwakilishi wa   tasisi za elimu ilichukuliwa na Mwl Pendael Lesso.
Pia nafasi ya ya uwakilishi wa nafasi ya wanawake ilichukuliwa na Renatha Chawene , nafasi ya uwakilishi sekondari ilichukuliwa na mwl  Michael Mbalasalo na nafsi ya na uwakilishi  walemavu ilichukuliwa  na Mwl Aidani Masima
Akitoa shukrani  baada ya kuchaguliwa  mwenyekiti huyo Mwl Daniel Tito aliwataka walimu hao kuweza kushirikiana  katika kujiletea maendeleo chanya na kupigania haki za mwalimu   ambazo zimeonekana  kuupunjwa kila kukicha

.

Comments

Popular posts from this blog

DC KIZIGO ATOA MAAGIZO KWA KWA MAAFISA ELIMU KUKABILIANA NA UKATILI MASHULENI.

HISTORIA YA MPWAPWA HATARINI KUTOWEKA

KIZIGO AWAPONGEZA RUWASA,AKERWA NA UHARIBIFU WA MAZINGIRA,AWATAJA MADIWANI.