Rais jakaya Kikwete akizungumza jambo na Rais wa Ivory Coast,Allasane Wattara kwenye uwanja wa ndege wa Kilimanjaro(KIA)baada ya kuhudhuria mkutano wa mwaka wa Benki ya maendeleo ya Afrika(AfDB)mjini Arusha.picha na Filbert Rweyemamu
Mkuu wa wilaya ya Mpwapwa Bi Sophia Kizigo akifungua kikao cha wadau wa Ulinzi dhidi ya Mtoto na ukatili wa kijinsia kilicho wezeshwa na Jukwaa la utu wa Mtoto CDF wilayani Mpwapwa. Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la utu wa Mtoto CDF Koshuma Mtengeti akichangia jambo katika kikao cha kujadili ulinzi wa Mtoto wilayani Mpwapwa. Stephen Noel-Mpwapwa. Mkuu wa wilaya ya Mpwapwa Mkoani Dodoma Bi Sophia Mfaume Kizigo ametoa amri kwa maafisa Elimu wote ndani ya wilaya hiyo kuhakikisha shule zote za Msingi na sekondari zinakuwa na walimu walezi kwa lengo la kupunguza vitendo vya ukatili kwa watoto wawapo shuleni. Mkuu wa wilaya hiyo ametoa agizo hilo kwenye mkutano wa Siku moja uliondaliwa na Asasi ya kiraia jukwaa la utu wa mtoto CDF iliyo kutanisha Wadau wote wanao fanya afua za kumlinda mtoto na kujali ustawi wa mtoto. Amesema Ili kuhakikisha watoto wanakuwa Kwenye mazingira ya usalama lazima kunakuwapo na watu wanao ratibu kero zinazo wakabili watoto au pindi wafanyiwapo uk
Na Stephen –noel –mpwapwa. WANANCHI wa wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma wameonyesha wasiwasi wao juu ya vitu vya kihistoria ya wilaya hiyo vilioachwa na wakoloni iko hatarini kutoweka kutokana na sehemu hizo za kihistoria kuto kuhifadhiwa na kulidwa na mamlaka husika. Wakiongea na waandishi wa habari mmoja wa wazee wakongwe wa mji huo bwana Abinoo Mathiasi mkazi wa hazina alisema kuwa miongoni mwa historia hizo ambazo ni njia kuu ya watumwa iliyokuwa ikotokea bara yaani mikoa ya Kigoma na Tabora na kuelekea Bagamoyo na Zanzibar iliyokuwa ikiongozwa na Said Majid TippTip na Abushir ambayo kwa sasa iko mbioni kufutika Mti wa mlumbulumbu ambao kwa sasa umesha anguka na wanachi wameupasua kuni ambapo palichomwa kanisa la Anglikana la kwanza na mfanya biashara ya watumwa mwarabu Abushir kwa vile watu wa eneo hilo walikuwa wanapinga biashara hiyo mwaka 1890 eneo la Vinghawe palipo jegwa kanisa la watakatifu wote. Aidha alisema
Mpwapwa. Habari. Mkuu wa wilaya ya Mpwapwa Bi Sophia Kizigo akiongea kwenye mkutano kazi wa RUWASA na wadau wa maji uliofanyika katika ukumbi wa chuo cha Afya.(picha na Emanuel Uronu(Vaino) Mkuu wa wilaya ya Mpwapwa mkoa wa Dodoma Bi Sophia Kizigo amezitaka jumuiya za watumia maji kuweza kuunganisha nguvu za jumuiya moja na nyingine ili kuweza kutoa huduma bora kwa wananchi. Kizigo ametoa Rai hiyo wakati wa kikao kazi cha wadau wa maji kilichofanyika katika ukumbi wa chuo cha Afya mjini hapa kilicho wajumuisha Viongozi wa jumuiya za watumia maji watendaji wa kata na vijiji napamoja na madiwani wa kata husika , Kizigo amesema pamoja na serikali ya awamu ya sita kuweka dhamira thabiti ya kumtua mama ndoo kichwani lakini bado jamii husika imeendelea na uharibifu wa mazingira unaotishia uendelevu wa miradi mikubwa ya maji inayowekezwa na serikali. Kupitia changamoto hiyo ametoa siku 14 kwa madiwani wote wanasiasa na baadhi ya watendaji wa kata na vijiji wanaowakingia
Comments
Post a Comment