ANUSURIKA KIFO BAADA YA KUPIGWA NA TEMBOOMANA

Na OMANA GOUTH  MPWAPWA

Mtu mmoja anayejulikana kwa jina Baraka mlowe (25) mkazi wa kijiji cha pwaga kitogoji cha ikulu wilayani mpwapwa mkoa wa Dodoma amejeruhiwa na tembo na kupasuliwa tumbo hadi utumbo kuwa nje ya tumbo lake.

Akizungumza na waandishi wa habari  kaka yake  majeruhi bwana Geofrey Mlowe alisema kuwa siku ya tukio majeruhi alikuwa  na nyumbani   na alisikia kuwa tembo wameingia mashambani  na wanaharibu mazao na ndipo alipo enda kuangalia hali ya shamba na  kuwafukuza wanyama hao,

 Alisema kuwa ndipo  alifika mashambani alikuta tembo hao na alikuta watu wengi wakiwa wana shangaa  tembo hao lakini yeye alitaka kuwashangaa kwa karibu ndipo tembo huyo  alimrukia  na  kumwangusha chini na kuanza kumkanyaga na alimchoma na mkonga  na ndipo alimtoboa sehemu za tumboni na kumtoa utumbo ukiwa nje.

“Alipo kuwa amekamatwa na  tembo huyo watu wakapiga kelele na  za kuomba msaada   na ndipo tembo huyo alimuachia huku akiwa  katobolewa utumbo na  kuvunjwa mguu wa kushoto chini ya goti kwa kukanyagwa’’alisema bwana Mlowe.

Mganga mkuu wa hospitali hiyo Dk.MOHAMED PATHAN wa hospitali  ya wilaya ya  umedhibitisha kuwepo kwa  majeruhi huyo  na alisema kuwa  atatoa taarifa ya maendeleo yake  hapo baadae watakapo mfanyia uchunguzi kwa kina “ninchoweza kusema kwa sasa ana hali mbaya subiri tufanyie uchunguzi ndipo nitakapo toa majibu ya maendeleo yake”alisema dk pathan

Kaimu  afisa  wanyama poli wa wilaya  ya Mpwapwa Bwana Oska Malima alikili kuonekana kwa tembo katika maeneo ya kijiji hicho na alisema kuwa siku tatu kabla  tembo hao walionekana katika kijiji cha makutupa  laikini hawakuleta madhara yeyote, ila  kinacho onekana tembo huyo anae jeruhi watu inasadikiwa kajeruhiwa na watu hivyo wanyama hao walionekana kujihami na watu  wanaonekana kutokea mbele yake.

 Pia alisema kuwa tembo hao  walionekana wakiwa wanne  na wametorsssoka kutoka hifadhi za wanyama za luaha mbuyuni mkoni iringa ambapo ni mpakani na wilaya ya mpwapwa

Aidha alisema kuwa  sehemu wanamopita tembo hao inaonekana siku nyingi humo  ilikuwa njia za tembo hao  hivyo ni tabia ya tembo kurudia njia zao za zamani.

Na aliwataka wananchi wote wa wilaya ya mpwapwa welewe wanyama poli kwani wanyama poli wasipowachokoza hawawezi kuzuru mtu wa aina yoyote  na kuwataka kuto kwashangaa kwa karibu zaidi ili waweze kujilinda ..



Comments

Popular posts from this blog

DC KIZIGO ATOA MAAGIZO KWA KWA MAAFISA ELIMU KUKABILIANA NA UKATILI MASHULENI.

HISTORIA YA MPWAPWA HATARINI KUTOWEKA

KIZIGO AWAPONGEZA RUWASA,AKERWA NA UHARIBIFU WA MAZINGIRA,AWATAJA MADIWANI.