MPWAPWA KUWA JAGWA BAADA YA MIAKA KUMI.,WATAFITI


NA STEPHEN NOEL MPWAPWA

Imeelezwa kuwa baada ya  miaka kumi   zaidi   ya  wakazi wapatao wapatao 150,000 laki moja na elfu hamsini wa kazi wa wilaya ya mpwapwa na kogwa wataokosa huduma za maji kabisa  kutokana na uharibifu wa mazingira unaoendelea katika  vyanzo ya maji vya milima kiboliani na kwa kwamdyanga.

 Hayo yamebainishwa na watafiti wa huduma za jamii  za kituo cha utafiti na mifugo  cha  Tanzania kilichopo wilayani mpwapwa  Mkoa wa dodoma  kijulikanacho kama LITI – MPWAPWA.

 Akiongea na aliyekuwa mkuu wa wilaya ya mpwapwa amabae kwa sasa amehamia wilaya ya  Karagwe Bi Darling Lwegasila  mkuu wa chuo  cha utafiti cha mpwapwa  Dk,  Devid Sindalo  alisema kuwa kutokana  shughuli za kibinadamu  zinazo endelea katika vyanzo ya  maji vilivyoko kwenye milima  kiboliani   Wilaya ya mpwapwa  wakazi wake watakosa maji kabisa  kutokana na kukauka vyanzo hivyo ambavyo ndilo tegemezi  kwa wilaya ya mpwapwa na kongwa bila  hatua za makusudi kuchukuliwa  kimakini katika jambo hilo.

 Aidha  Dk, SINDALO alisema kuwa shughuli zinazo endelea katika milima  hiyo ni kilimo, uchomaji moto, na shughuli za uchomaji mkaa katika  maeneo yanayo zunguka  vyanzo vya maji hayo.

Pia alisema kuwa mbali na matokeo hayo ya muda mrefu  kutokea bali kuna  matokeo  ambayo mpaka sasa wilaya hiyo imenza  kukabiliana nayo hasa katika  kituo chake cha utafiti kilichopo  liti mpwapwa.

 Madhara ambayo yameanza  kujitokeza  kwenye kituo ni kupungua kwa malisho  ya wanyama katika kituo hicho magonjwa ya mapafu kwa ngombe na mbuzi ambayo yote hayo husababishwa na joto kuongezeka  nchini na magonjwa na kuongezeka kwa kupe wanao umma ngombe na kuwasababishia  ugojwa wa ndigana.

Pia Dk  alisema “ kwa wanasiasa   waache kutumia siasa  kwenye mambo yasiyo hitaji siasa   kwa  maana nakumbuka kulikuwa na mpango wa kuwa hamisha wavamizi katika maeneo hayo ya vyanzo vya maji lakini  siasa ikaingilia kati na wale watu wakaachwa kulekule kwa ajili ya maslahi ya wanasiasa”alisema Dk,sindalo

 Pia naye mkuu wa wilaya hiyo wa zamani  Bi Lwegasila alitoa  lawama  kwa  vyombo vya kiutendaji vya wilaya hiyo ikiwemo polisi na mahakama  kuwa  hawakuwajibika ipasavyo katika swala la kupigania  mazingira katika milima kiboriani kwa kusema kuwa  swala hilo lilikuwa na dalili ya rushwa  kilicho pelekea kushindikana  kwa swala  hilo.

Naye  Askofu mstaafu wa kanisa la ANGLIKANA  MPWAPWA Askofu SIMON Chiwanga amesema kuwa katika kulishughulikia swala hilo   ameamua kuanzisha mradi wa utunzaji utunzaji katika safu za mlima kiboliani  kwa kupanda miti na kulejesha uoto wa asili  kwa  kuanzisha shirika lijulikalo kama  LEAD FOUNDATION
.
Na mkuu wa wilaya mpwapwa  amesema kuwa katika mapango wake wa kazi hiyo ndiyo itakayo kuwa ndiyo shughuli zake za awali hivyo ametoa wito kwa watendaji wake wote kuwa  wakae mkao wa kazi yeye ametumwa kuwahudumia wanachi na kutatua kero, zao  hivyo hajazoea kupindisha pindisha mambo “ nawaambia walio vamia hivyo vyanzo vya maji wakae tayari kuondoka kwa hiari yao wenyewe bila hatua za kisheria. kuanza kuchukuliwa”.

Comments

Popular posts from this blog

DC KIZIGO ATOA MAAGIZO KWA KWA MAAFISA ELIMU KUKABILIANA NA UKATILI MASHULENI.

HISTORIA YA MPWAPWA HATARINI KUTOWEKA

KIZIGO AWAPONGEZA RUWASA,AKERWA NA UHARIBIFU WA MAZINGIRA,AWATAJA MADIWANI.