WANANCHI WA MPWAPWA WALILIA GARI LA ZIMA MOTO.



Moto  wateketeza nyumba na mali  zenye dhamani ya shilingi million 34 mali ya Bwana Mohamed Mounsor (Mokili)mkazi wa kota  Kata ya Mpwapwa mjini.
Bwana Monsour amesema kuwa chanzo cha moto huo bado hakijajulikana  ila serikali kwa kushirikiana na shirika la Tanesco wanafanya uchunguzi wa kujua  chanzo cha moto huo uliweza kuteketeza nyumba yenye vyumba vitano, na bidhaa za ndani vyote  vyenye dhamani ya shilingi  million 34.
Kutokana na hali hiyo  wananchi wa mji huo wameitaka uongozi wa wilaya hiyo  kuwa na gari la Zima moto ili kuweza  kukabiliana  na majanga  ya moto.
Akiongea mwenyekiti  wa mtaa wa kota Bwana Mwakiseyo ya katika tukio la Nyumba ya bwana Mohamed Monsour (Mokili) baada ya kuungua moto na kusidwa kuzima moto huo  kutokana na  wilaya hiyo kuto kuwa na gari la zima moto.
Bwana Mwakiseyo amesema pamoja na wilaya hiyo kuwa ni miongoni mwa wilaya Kongwe hapa nchini na  wilaya iliyo zungungukwa na tasisi nyingi za serikali lakini imeshidwa kuwa na gari la zima moto kitu alichosema mala tukio la moto likitokea  mali huteketea zote.
Aidha amesema  kwa sasa  wilaya hiyo imekuwa   na matukio kadhaa ya nyumba za watu na tasisi za serikali kuungua  moto na  mali nyingi za  watu kuuteketea kabisa .
Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama  ambae ni mkuu wa wilaya ya Mpwapwa  bwana Jabir Shekimweri  alisema kuwa   katika tukio hilo hakuna mtu aliye weza kupoteza maisha  bali aliamuru jeshi la polisi kwa kushirikiana na shirika la ugavi wa umeme  TANESCO kufanya uchunguzi wa haraka wa kubaini chanzo cha moto huo.
Shekimweri amesema kutokana na wilaya hiyo kuwa na matukio kadhaa sasa ya moto na ukuaji wa mji huo na  Mpango wa serikali kuhamia mkoani Dodoma  kuna haja ya wilaya hiyo kuwa  kuwa na gari la zima moto na kikosi cha zima moto katika wilaya hiyo ili kuweza kunusuru mali za wananchi au za serikali kuteketea .


Comments

Popular posts from this blog

KIZIGO AWAPONGEZA RUWASA,AKERWA NA UHARIBIFU WA MAZINGIRA,AWATAJA MADIWANI.

HISTORIA YA MPWAPWA HATARINI KUTOWEKA

DC KIZIGO ATOA MAAGIZO KWA KWA MAAFISA ELIMU KUKABILIANA NA UKATILI MASHULENI.