HAKI ELIMU WATAMBULISHA MKAKATI WA MIAKA MITANO MPWAPWA.



SHIRIKA  lisilo kuwa  la kiserikali linalojihusisha  na ushawishi katika kuboresha Mazingira ya Elimu hapa nchini  la Haki Elimu limeiomba serikali kuendelea kushughulikia chamngamoto zinazo ikabili Elimu kwa sasa ili kuweza kuwa  wataalamu wenye tija siku za mbeleni.
Kauli hiyo ilitolewa na wadau wa elimuwilayani hapa  katika kikao cha pamoja na  shirika la Haki Elimu  walipokuwa wakitambulisha mkakati wao wa miaka mitano utakao fanywa na shirika hilo juu ya  kuweza kuinua  Elimu hapa nchini.
Ofisa Programu  wa shirika hilo bwana Frolige  Lyelu  amesema pamoja na serikali kuonyesha  nia dhabiti ya kuikomboa elimu  hapa nchini lakini kuna bado baadhi ya changamoto ambazo zinatakiwa kumalizwa na ngazi za chini  kuliko kuendelea kuisubiri serikali .
Frolige alisema  Mpango wa Elimu bila malipo umeweza kuongeza hamasa ya watoto wengi kuandikishwa  darasa la kwanza na wanao jiunga kidato cha kwanza idadi imekuwa ikiongezeka kila mwaka kitu alichosema kuwa  kinaonyesha  kuwa michango mingi shuleni ilikuwa ni chanzo watoto wengi kukosa Elimu.
Hata hivyo  amesema bado kuna uelewa mdogo wa jamii kuhusu mapango wa Elimu bila malipo  na ushiriki wao katika katika shughuli za  maendeleo  ya Elimu.
Pia Frilie amesema kuwa pia serikali inatakiwa kushughulikia  changamoto ya farsafa ya elimu kwa sasa kutokana na elimu yetu kutokuwa na farsafa “tunakumbuka wote katika serikali ya awamu ya kwanza tulikuwa na farsafa ya elimu na kujiteemea lakini hivi sasa farsafa ya elimu ni ipi  hivyo kutokuwapo na farsafa kunapelekea kushidwa kuwa na mwelekeo wa elimu”aliongea.
Hata hivyo  Ofisa Progamu huyo  alisema  katika miaka mitano shirika la haki Elimu nakusudia ,kushawishimabadiliko ya kisera  na utekelezaji wake,kukuza ushiriki wa wananchi na kujishughulisha,na kukuza uwazi na uwajibikaji katika maeneo ya serikai za vijiji  na shule.
Kwa upande wake kaimu Ofisa Elimu  Elexender Kioyi  alikili kuwapo kwa changamoto nyingi katika idara ya elimu  kwa wilaya yake ikiwemo  vyumba vya madarasa,upunufu wa vifaa vya kujifunzia na kufundishia,pamoja na vyumba vya awali na matundu ya vyoo kwa wanafunzi wenye umri mdogo  ambapo baadhi ya shule wanafunzi wa awali husomea nje kwenye miti sana kitu alicho kisema pia nacho ni sababu inayo changia elimu kurudi nyuma.
Kioyi alisema kama wadau wa maendeleo  wakashirikiana na serikali tunaweza kuikomboa serikali  na kufika tunapopatarajia .
“Mwanafarsa mmoja aliwahi kusema kuwasehemu ya mabadiliko unayotaka yatokee dunia kuliko kubaki kupiga kelee tu,kwa mpango haki elimu naona wao pia wameona baada ya kufanya utafaiti wameingia nao kuwa sehemu ya mabadiliko”aliongea Kioyi.


Comments

Popular posts from this blog

KIZIGO AWAPONGEZA RUWASA,AKERWA NA UHARIBIFU WA MAZINGIRA,AWATAJA MADIWANI.

HISTORIA YA MPWAPWA HATARINI KUTOWEKA

DC KIZIGO ATOA MAAGIZO KWA KWA MAAFISA ELIMU KUKABILIANA NA UKATILI MASHULENI.