SERIKALI YAWAPA MTIHANI WAKUU WA SHULE MPWAPWA


SERIKALI wilayani Mpwapwa mkoani Dodoma  imewataka wakuu wote shule
zote za kidato cha sita zilizopatiwa fedha za ukarabati  kuthaminisha
ukabarabati wa shule hizo  sambamba na uboereshaji wa elimu katika
shule zao.
Kauli hiyo ilitolewa na mkuu wa wilaya ya Mpwapwa  Jabir Shekimweri
alipotembelea  shule hizo kwa ajili ya kuangalia hali halisi ya
ukarabati unaoendelea  katika shule hizo.
Shule zilipatiwa fedha za ukarabati  katika shule  za kidato cha sita
ni Mpwapwa Sekondari ,Mazae Sekondari,Berege sekondari na  Kibakwe
Sekondari.
Shekimweri alisema  hakuna zaidi kwa shule hizi kutoa shukrani kwa
serikali zaidi ya kupandisha kiwango cha ufaulu  katika shule zote
ambazo zimepatiwa fedha za ukarabati.
“haiwezekani shule zinapendeza zinanga’aa lakini ufaulu unakuwa chini
hivyo  wakuu wa shule  na walimu mjipange  sasa uzuri wa miundo mbinu
hii ya shule iendane  na viwango vya elimu vinavyo tolewa shuleni hapa
tunataka kusiwe na  division four wala three hapa tuanzie division
two ndo itakuwa shukrani kwenu kwa serikali” aliongea.
Shakimweri alisema serikali imetoa zaidi ya billion mbili kwa ajili ya
ukarabati wa shule zote za kidato cha sita kwa ajili ya kuboresha
miundo mbinu ya kujifunzia na kufundishia.
Kaimu mkuu wa shule  ya Mpwapwa  Sekondari  Mwalimu Omary Towaqali
alisema  Shele hiyo ambayo imejegwa mwaka 1926 ambayo haikuwahi
kufanyiwa ukarabati tangia ijegwe  kwa zaidi ya miaka 90  hivyo
kupelekea uchakavu mkubwa  na kutishia afya za wanafunzi shuleni hapo.
Aidha alisema kwa kukamilika kwa ukarabati na ujenzi wa bweni jipya la
wanasichana wa kidato cha tano na cha sita kutawasaidia wasichana hao
kupata malazi  mala baada ya bweni la wanafunzi hao kuungua moto
January 20mwaka  2015 wanafunzi wa kidato cha sita cha tano wasichana
iliwalazimu kulala kwenye darasa lililokuwa chumba cha kopyuta
kutokana na  bweni hilo  kuungua moto.
Pia mkuu wa shule hiyo alisema shule inakabiliwa na uchavu mkubwa wa
miundo mbinu ya shule  ikiwemo majengo, matundu ya vyoo na vyumba vya
maabara za masomo ya sayani pamoja na vifaa vya kufundishia.
Mwandisi wa  wa anayesimamia ukarabati katika Shule ya sekondari
Mpwapwa  bwana  Herbert Kimboi aisema  ukarabati huo unatarajiwa
kukamilika kabla ya july 15 mwaka huu na ukarabati huo unakadiliwa
kutumia  jumla ya shilingi bilioni 1.2/=ambapo alisema mpaka ukarabati
huo umetumia jumla ya shilingi million 700 na kwa kutumia mafundi
wazawa  wameweza kuokoa julma ya shilingi zaidi ya million 518,
Alisema ukarabati huo ni  mpango  serikali wa ukarabati  kwa shule
kongwe  hapa nchini kupitia wizara ya elimu  katika mpango wake wa
lipa kutokana na matokeo.
Mwandisi Kimboi alisema  kwa sasa  ukarabati wa shule hiyo umefikia
asilimia 90% na hatua iliyobaki ni umaliziaji wa vitu vidogovidogo
kama usafi  na uapngaji wa vitanda tayari wanafunzi wafuanguapo shule
july 15 wayatumie madarasa hayo na mabweni  hayo.
Shule ya sekondari Mpwapwa ni miongoni shule kongwe hapa nchini iliyo
jegwa mwaka 1926 na serikali ya kikoloni ikiwa na lengo la kuwaandaa
watoto wa machifu kuja kufanya kazi katika serikali yao yao ,kwa
kipindi hicho kazi hizo zilijulikana kama white colar job

Comments

Popular posts from this blog

DC KIZIGO ATOA MAAGIZO KWA KWA MAAFISA ELIMU KUKABILIANA NA UKATILI MASHULENI.

HISTORIA YA MPWAPWA HATARINI KUTOWEKA

KIZIGO AWAPONGEZA RUWASA,AKERWA NA UHARIBIFU WA MAZINGIRA,AWATAJA MADIWANI.