MWANASHERIA WASERIKALI WAPINGANA NA DPP

Na noel stephen  mpwapwa
TASISI ya kuzuia na kupambana na RushwaTAKUKURU wilaya ya mpwapwa Mkoani Dodoma  imemfikisha mahakamani  mtumishi wa halimashauri ya mpwapwa   bwana Ignace Saye  kwa tuhuma za  ubadhilifu wa  mali za umma
.
Ikisomewa mashtaka  yake mbele ya hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama ya wilaya bwana JEMSI KAREIMAHA na  mwendesha mashtaka wa TAKUKURU  bwana GARRY  NOMA alidai kuwa  mtuhumiwa huyo anakabiliwa na makaosa  10 ya ubadhilifu wa mali za umma.

Bwana Garry Noma alidai mahakamani hapo kuwa mtuhumiwa alilitenda makosa hayo  katika tarehe mbalimbali za mwaka 2008  hadi mwaka 2010 katika ofisi ya halmashauri ya wilaya ya mpwapwa akiwa kama boharia mkuu wa wilaya hiyo.

Na  mtuhumiwa alikanusha makosa yote hayo na ameachiwa  huru kwa dhamana ya shiliongi million 10  au kitu  chenye dhani ya hiyo pesa kisichi weza kuhamishika na shitaka lake litasomwa tena 12/07/2012 .


 AIDHA katika hali isiyo ya kawaida  mwanasheria mkuu wa serikali kanda ya kati wametofautina  kimaamuuzi na mkurugenzi  mkuu wa mashitaka  DPP juu ya  tuhuma za kesi  inayo mkabili  boharia ya halmashauri  ya wilaya ya mpwapwa Bwana IGNACE SAYE  kwa mwanasheria kudai hana hatia wakati  mkurugenzi wa  mashitaka anadai Bwana Saye ana kesi  ya kujibu.

PIA kwa mujibu wa chanzo chetu kimedai kuwa  mwanasheria mkuu  mfawidhi wa serikali kanda ya  kati bwana  FARAJA  NCHIMBI  alimwandikia  barua  bwana SAYE ya tarehe 20.03.2012 yenye  kumb na  SAD/C/120/5/2/17/2011/08  na nyingine  yenye kumb na DOMR/CID/B1/7/VOLXXII/188 ya tarehe 23/03/2012  kuwa amechunguza na kuona kuwa hana hatia na hana kesi ya kujibu kutokana na  kukosa nakala halisi za vielelezo vya ushahidi   wa ununuzi wa mafuta katika ya kuendeshea mitambo ya kutengeza daraja la GODEGODE ambapo pia nakala moja ikienda kwa mkurugrenzi wa  mashataka  DPP. Kwa taarifa.

 KWA UPANDA WAKE  mwendesha mashtaka ya Tasisi ya Kuzuia na kupambana na rushwa   TAKUKURU  bwana  NOMA  alidai kuwa  mtuhumiwa anashitakiwa kwa mujibu ya  sheria ya  kuzuia na kupambana na  no 11 ya mwaka 2007 anashitakiwa kwa kuhujumu uchumi aya 1jedwali 10 kifungu 57(1) na kifungu cha 60(2) sura na 200R:E2002.


Bwana SAYE  anaye kabiliwa na tuhuma za  ubadhilifu wamali za umma  na  na kosa la kumdanganya  mwajili wake   kwa kugushi na nyaraka za kununulia mafuta za kuendeshea mitambo yenye dhamani ya shilingi milioni 12,150,400/

PIA kwa upande wake mtuhumiwa  bwana saye  ametoa lawama kwa utendaji wa serikali na tasisi zake kuwa hazina  mawasiliano mazuri na  juu uendeshaji wa kesi zinazo ikabili serikali “kwa  maana mwanasheria kasema mimi sina hatia  pccb wananipeleka mahakamanin kwa kosa hilo hilo  sasa nashidwa kuelewa labda  kuna kingine wanacho kitaka kwangu  maana pccb wantumia sheri gani na  polisi na wanasheria wanatumi sheria zipi mbona wanachanaganyana wenyewe”, alisisitiza bwana saye.

Bwana  Saye  na wanzake watatu  walituhumiwa  kugushi  nyaraka za kununulia mafuta ya kuendeshea mitambo ya ujenzi wa daraja la godegode  liligharimu kiasi cha sh million 950 ambalo lilijengwa   na wanajeshi   kuanzia mwaka 2008 nhadi 2011, na alisimamishwa kazi kwa uchunguzi wa kesi hiyo na walipotambua hana hati amerudishwa tena kazini  na tena bado anakabiliwa na shitaka hilohilo.



Comments

Popular posts from this blog

KIZIGO AWAPONGEZA RUWASA,AKERWA NA UHARIBIFU WA MAZINGIRA,AWATAJA MADIWANI.

HISTORIA YA MPWAPWA HATARINI KUTOWEKA

DC KIZIGO ATOA MAAGIZO KWA KWA MAAFISA ELIMU KUKABILIANA NA UKATILI MASHULENI.