vyombo vya habari vyalaumiwa kesi ya LULU

BARAZA la Habari Tanzania (MCT), limevishutumu vyombo vya habari kwa kuandika habari zenye mwelekeo wa kumhukumu msanii Elizabeth Michael, maarufu kama Lulu, kwamba amemuua msanii mwenzake, Steven Kanumba.

Akisoma tamko la Kamati ya Maadili ya MCT Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Jaji mstaafu Thomas Mihayo, alisema wamesikitishwa na ukiukwaji mkubwa wa maadili uliojitokeza kwa baadhi ya vyombo vya habari katika kuripoti kuhusu kifo cha msanii, marehemu Kanumba.

Alisema hatua hiyo ni ukiukwaji mkubwa uliovuka mipaka wa maadili ya uandishi wa habari.

Alisema vyombo hivyo vimemhukumu msichana Lulu kuwa amemuua msanii huyo bila kuzingatia kwamba kufanya hivyo ni kosa.

Alisema ukiukwaji huo umejitokeza baada ya msichana huyo kufikishwa mahakamani ambapo baadhi ya magazeti yanayoheshimika katika jamii yaliandika vichwa vya habari vinavyomhukumu moja kwa moja Lulu kama ni muuaji.

“Kwa mujibu wa sheria na maadili ya uandishi wa habari, mtu yeyote anayekamatwa kwa tuhuma yoyote ile ni mtuhumiwa hadi atiwe hatiani na mahakama.

Comments

Popular posts from this blog

KIZIGO AWAPONGEZA RUWASA,AKERWA NA UHARIBIFU WA MAZINGIRA,AWATAJA MADIWANI.

HISTORIA YA MPWAPWA HATARINI KUTOWEKA

DC KIZIGO ATOA MAAGIZO KWA KWA MAAFISA ELIMU KUKABILIANA NA UKATILI MASHULENI.