BABA AMBAKA MWANAE WA MIAKA 12 NA KUMMPA MIMBA.

Mtu mmoja  aliyefahamika kwa jina la Jemsi Leuna mkazi wa kijiji cha Chitemo wilaya  ya Mpwapwa Mkoa wa Dodoma   amefikishwa mbele ya hakimu makazi mfawidhi  bi Nurupedesia Nassar kufutia tuhuma ya kumbaka na kummpa mimba mtoto wake wa kumzaa mwenye umri wa miaka 12 mwanafunzi wa darasa nne.
Mwendesha mashitaka wa polisi Bwana Michael Joseph  aliiambia mahakama kuwa mtuhumiwa huyo akitambua kuwa  huyo ni mtoto wake wa kumzaa aliweza kumbaka  na  kutenda kosa hilo kinyume na  kifungu cha namba 130 kifungu kidogo(1) na kifungu 131kifungu kidogo(1)iliyo fanyiwa malejeo mwaka 2002.
Bwana Machael  aliiambia mahakama  kuwa kosa la pili  ni kummpa mimba mwanafunzi darasa la nne kinyume na  sheria ya Elimu namba 353 kifunfu cha 60Akifungu kidogo cha kwanza  iliyofanyiwa malejeo mwaka 2016.
Mtuhumiwa alipo ulizwa juu ya tuhuma hizo alikanusha kutenda kosa   na kesi yake iliahirishwa  hadi itakapo somwa tena march 26 mwaka huu.

Comments

Popular posts from this blog

KIZIGO AWAPONGEZA RUWASA,AKERWA NA UHARIBIFU WA MAZINGIRA,AWATAJA MADIWANI.

HISTORIA YA MPWAPWA HATARINI KUTOWEKA

DC KIZIGO ATOA MAAGIZO KWA KWA MAAFISA ELIMU KUKABILIANA NA UKATILI MASHULENI.