MPWAPWA YAMLIZA KAPONDA KIELIMU



OFISA elimu mkoa wa Dodoma  Bwana Juma Kaponda (JJ)amewataka wataalamu ,wanasiasa,  na walimu  kushirikiana  katika kushughulikia  changamoto za Elimu ili kuweza kuinua elimu  wilayani hapa.
Kaponda aliyasema hayo  wilayani hapa  katika mkutano wa wadau wa elimu  uliojumuisha , walimu wakuu wa shule zote, waratibuelimu kata , na  na maofisa wa elimu , uliofanyika  katika ukumbi wa chuo cha ualimu  Mpwapwa  juu ya  kutadhimini  matokeo ya darasa la saba  ya mwaka  2015.
Kaponda  alisema  katika mtihani wa  kumaliza elimu mwaka 2015  wilaya ya mpwapwa ilikuwa wilaya ya mwisho  kimkoa  na ilikuwa wilaya ya 164 kati wilaya 166 nchi zima ,japo ilifanikiwa kutoa mwanafunzi wa kwanza kimkoa kutoka katika shule  ya Mazoezi Mteajeta  mwanafunzi  Airene Chiwanga
Aidha alisema  ufundishaji  mbovu,utendaji wa kimazoea  kwa maofisa Elimu  , kukosekana  kwa mawasiliano  sahihi kati walimu  na maofisa  elimu  imepelekea Mpwapwa  kushidwa kufanya  vizuri katika mtihani huo  kwa mika miwili mfululizo.
Pia alisema   mwamko mdogo wa elimu  katika wilaya ya Mpwapwa imepelekea elimu kuzidi kudidimia siku hadi siku kitu alicho kisema  kuwa kimesababishwa na  na ulegevu wa usimamizi wa sheria   kwa viongozi wa ngazi za vjijiji na kata.
Alisema”kwa mfano kwa watoto walioanza darasa la kwanza mwaka 2010 walikuwa watoto  8048 lakini kufika darasa la sita mwaka 2015 zaidi ya watoto 1702 walikuwa hawapo shueni sawa na asilimia 21% ya wanafunzi wote walioacha masomo kwa sababu mbalimbali”alisema  Juma kaponda.
Kwa upande wake  mkuu wa wilaya ya Mpwapwa  Mwalimu Mohamed Utaly  aliyekuwa  mgeni rasmi  katika mkutano huo  aliwataka  viongozi wote wanao husika na suala  la elimu kuiondoa  Mpwapwa  katika nafasi ya mwisho  kimkoa  nakuipandaisha  hadi nafasi ya kwanza kama ilivyokuwa ikifanya miaka ya nyuma.
Alisema “sitakubali  kuona  Mpwapwa  ikiendelea  kuto kufanya  vizuri katika suala la elimu ukizingatia  Mpwapwa inaongozwa na walimu nikiwamo mimi mwenyewe na mkurugenzi wangu  sasa tujipange tuu kabla hatujanza kutumbuana  majipu”alisema  Utaly.
Hata hivyo mkurugenzi  mtendaji  wa halmashauri  ya wilaya  ya mpwapwa  Mohamed  Maje alisema  watahakikisha  wanaipandisha  elimu  katika  wilaya ya mpwapwa  kwa  kuindoa  changamoto zote zilizo kuwapo  awali ikiwamo kulipa madeni ya walimu na upandaji wa madaraja  kwa walimu wanao stahili.
Maje  alisema  kuwa shule kumi  za mwisho  aliwataka walimu na waratibu elimu  kata   kutoa maelezo ya maandishi ndani ya siku saba  juu ya sababu zilizo pelekea  shule  hizo  kufanya  vibaya.
Mmoja wa Walimu mjini hapa Mwalimu Mohamed Matula alisema  mazingira magumu ya walimu wilayani hapa yanayo sababishwa na Jiografia ya wilaya  kunapelekea mpwapwa kuendelea kufanya  vibaya katika sula la elimu , na mgowanyo mbovu wa walimu pia imekuwa chanzo cha  baadhi ya shule kuendelea kufanya vibaya.
Akizitaja   shule kumi zilizofanya  vibaya  wilayani hapa mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Mpwapwa bwana Majealisema ni Shule ya Msingi Gomuhungile,Idodoma,Kazania ,Chang’ombe ,Rufu, na  Kiboriani,shule zingine ni  shule ya msingi  Kilambo, Njiapanda , Ngalamilo ,Mlunduzi, na Vikundi.

Na shule zilizofanya vizuri ni shule ya msingi  Kikombo,Pwaga,Mtejeta,Mpwapwa, Mang’angu, na Makutupa, shule zingine ni Kimagai, Chazungwa, Lumuma, na Bumira.


Comments

Popular posts from this blog

KIZIGO AWAPONGEZA RUWASA,AKERWA NA UHARIBIFU WA MAZINGIRA,AWATAJA MADIWANI.

HISTORIA YA MPWAPWA HATARINI KUTOWEKA

DC KIZIGO ATOA MAAGIZO KWA KWA MAAFISA ELIMU KUKABILIANA NA UKATILI MASHULENI.