MKURUGENZI MTENDAJI MPWAPWA AWATAKA WATENDAJI WAKE KUACHA URASIMU.



Na Stephen noel –Mpwapwa
MKURUGENZI  mtendaji wa halmashauri ya wilayaya mpwapwa mkoani Dodoma Bwana Mohamed Maje amesema kuwa atahakikisha  anakomesha urasimu wote kwa watendaji wake wa chini kwa wawekezaji wanaotaka kuwekeza wilayani hapa.
Mkurgenzi huyo ameyasema hayo  wilayani hapa  walipotembelea  kiwanda kidogo cha kusindika siagi ya karanga  kilichopo mjini hapa mtaa wa mji mpya.
Maje amesema hatavumilia kuona watendaji wake wa chini wanawakwamisha wawekezaji wanao taka kuwekeza mpwapwa.
Meneja wa kiwanda cha kusindika karanga wilaya hapa bi Paulina Visent   amesema kuwa  wamekuwa  wakipata shida kutoka idara ya ardhi kupata eneo maluumu la kujenga kiwanda hicho  kwa kile alicho kisema kuwa kinakwamisha  na kurudisha nyuma moyo wawekezaji wengine wanao taka kuwekeza  katika wilaya ya mpwapwa kutokana na urasimu wanao upata kutoka kwa watendaji wa serikali.
Aidha amesema kiwanda hicho kimesaidia kuitangaza Mpwapwa katika nyaja za kibiashara kwa mikoa ya jirani na nje Tanzania kutokana na bidhaa inayotengenezwa  katika kiwanda chake .
Aidha Bi Paulina   amesema  kuwa pamoja na mpwapwa kutangazwa pia imeweza kuajili zaidi ya akina mama  na vijana 20 ambao wanajipatia kipato na kuinua maisha yao kutokana na kuwapo kwa kiwanda  hicho  mjini mpwapwa.
Bi Paulina ameiiomba serikali kuweza kuwasaidia kuwatafutia masoko  ya uhakika  ya bidhaa wanayo zalisha katika kiwanda chao tofauti na sasa ambapo  soko lao si la uhakika sana na kusabaisha uzalishaji kuwa mdogo.
Kwa upande wake mkuu wa wialaya ya Mpwapwa  Mohamed Utaly  amewataka wawekezaji wote wanao ingia mpwapwa kuweza kufuata taratibu zote za kisheria ili kuweza kufanya kazi kwa  uhuru na kuongeza  ufanisi wa kiwanda chao.
Hata hivyo mkuu  wa wilaya huyo amesema  kuwa atahakikisha   wialaya yake inaandaa mazingira wezeshi na yasiyo kuwa na vikwazo  kwa wawekezaji  wanaoataka kuwekeza katika  wilaya ya Mpwapwa ili kuweza kuinua kipato cha wilaya na mkoa kwa ujumla

Comments

Popular posts from this blog

KIZIGO AWAPONGEZA RUWASA,AKERWA NA UHARIBIFU WA MAZINGIRA,AWATAJA MADIWANI.

HISTORIA YA MPWAPWA HATARINI KUTOWEKA

DC KIZIGO ATOA MAAGIZO KWA KWA MAAFISA ELIMU KUKABILIANA NA UKATILI MASHULENI.