mpwapwa waaswa kujiandaa na majanga ya mafuriko

Na noel Stephen  mpwapwa
W ITO   Umetolewa  kwa wanachi wa wilaya ya mpwapwa  kuweza  kujikinga na majanaga ambayo yanaweza kuzuilika ili kuweza kupunguza matokeo ya maafa kwa jamii .

Wito huo umetolewa na mkuu wa wilaya ya mpwapwa BWANA Chrisopher Kangoye alipokuwa akifungua warsha juu  kwa wakuu wa idara na wakuu wa tasisi  juu kuweza kutumia rasilimali   zilizopo  kwa ajili ya kuweza  kuzua majanga na mafuriko kwa wilaya ya mpwapwa.

Kangoye alisema kuwa  kuna maafa ambayo yanaweza kuzuilika  kama wananchi wanaishi mabondeni kuhama  kabla maafa  hayajafika  na kuweza kuimarisha miundo mbinu kwa  wilaya hiyo ikiwemo barabara,  makazi, na  madaraja.

AIDHA Kangoye alisema kuwa kwa historia  wilaya ya mpwapwa  inakabiliwa na majanaga kama mafuriko,uchomaji moto milima,  kuanzia  mwezi septemba hadi  decemba  ambapo alisema kuwa kutokana na hali hiyo wilaya na taifa inaingia hasara kubwa kwa kuwahudumia watu walio athiriwa na  matukio hayo  ambapo aliwataka wananchi kuchukua tahadhari mapema  na kuacha tabia ya kusubili majanga ili wapate  sababu za kuilaumu serikali.

Na alidai kuwa kwa wilaya ya mpwapwa inaingia hasara kubwa sana kwa kukosa usafiri, watu kufa na makazi yao kuharibiwa  kwa mafuriko ya mvua  ambayo hutokea vijiji vya  msagali na gulwe  kunzia miezi ya novemba na desemba ,hivyo aliwataka wananchi wa kata hizo na vijiji hivyo kuweza kuchukua tahadhari mapema kabla  maafa hayajatokea.

Na alitoa kalipio kali kwa watendaji  wa halimashauri hiyo ambao husubiri maafa  kutumia fursa hiyo kuweza kujinufaisha wao kwa  kujenga  miundo mbinu chini ya viwango au kutumia  fedha tofauti na  malengo yaliyo pangwa.

KWA upande wake  mkurugenzi wa kitengo cha majanga na  maafa kutoka ofisi ya waziri mkuu Brigedia  msatafu  Dakson Mdoe  alisema kuwa  mpwapwa na kilosa  ni miongoni mwa  wilaya ambazo  zinakubwasana na mafuriko  kwa kipindi cha mvua za masika zinapo anza kunyesha katika wilaya hizo  hivyo  alitoa wito kwa uongozi wa  wilaya na halmashauri  kuweza kuzuia kuliko kupambana  na matukio hayo  kwa wilaya mabapo alisema gharama za kuzuia ni ndogo kuliko  za kuweza kupamabana  nayo majanga hayo.

Pia alisema  imebainika kuwa   wilaya hizo zinakubwa na  majanga  ya mala kwa mala  kutokana na  baadhi ya kata  kuwa katika mkondo wa  bonde  la ufa  ambalo huweza kusababisha matetemeko ya ardhi , na mafuriko.

Alieleza kuwa  lengo la warsha hiyo ni  wilaya kuweza kundaa mpango wa  kukabiliana na  maafa  yanayoweza kutokea kwa kipindi cha miezi hiyo, na kuweza kuwashirikisha viongozi wa  wilaya  kuweza kubainisha fulsa zilizopo na vikwazo  ili kuweza kupunguza  matokeo ya  maafa kwa  kufuata  sera ya  taifa ya udhibiti wa maafa .

“ Kwa mfano  mafuriko ya mwaka jana    kukarabati  miundo mbinu ya reli ya godegode na gulwe imigharimu serikali shilingi billion 5 ambazo ni fedha  kubwa kwa nchi maskini kama Tanzania  bora tungejipanaga  tungeweza kufanya kitu cha maana naomba viongozi wote tushirikine katika hili ili kupunguza  ukali wa maisha kwa mlipa kodi’’ alisisitiza MDOE

Wajumbe wa warsha hiyo waliweza kubainisha  majanaga mabayo hui sumbua wilaya ya mpwapwa ambapo walisema kuwa ni magonjwa ya milipuko ya wanayama na binadamu,uchomaji moto misitu, mafuriko na matetemeko ya ardhi.

Comments

Popular posts from this blog

KIZIGO AWAPONGEZA RUWASA,AKERWA NA UHARIBIFU WA MAZINGIRA,AWATAJA MADIWANI.

HISTORIA YA MPWAPWA HATARINI KUTOWEKA

DC KIZIGO ATOA MAAGIZO KWA KWA MAAFISA ELIMU KUKABILIANA NA UKATILI MASHULENI.