MPWAPWA -MICHEZO


Walimu wa michezo Nchini wametakiwa  kutoa fursa sawa kwa vijana wenye
viapaji  wa mjini na vijijini ili kuweza kufikia ndoto zao kimchezo
kama walizofikia wachezaji wakubwa wa kimataifa.

Kauli hiyo ilitolewa na ofisa Elimu Sekondari  wilaya  ya Mpwapwa
bwana Nelson Milanzi  katika zoezi la kufunga kozi ya siku tatu kwa
walimu wa wa michezo wa wilaya ya Mpwapwa.

Mwalimu Milanzi  alisema michezo ikiwekwezwa vizuri kwa watoto  vijana
inaweza ikapunguza changamoto  ya ajira kwa  kwa vijana  katika taifa
letu “hasa kwa wale wenye vipaji  hasa wale walioko pembezoni kwa
mfano akina Mbwana Samata  waliotokea mbagala huko mbona hutuwasikii
vijana wenye vipaji wanaotoka vijijini  inaamana hawako wenye vipaji
huko sasa nyie nendeni mkawatengeneze akina Samata wengi


Naye  mkufunzi wa kozi hiyo Bwana Charles Maguzu  aliwataka Walimu wa
michezo  katika shule   za msingi na sekondari  kuanza kuipa
kiapumbele  michezo katika shule zao kwa lengo la kuibua vipaji  na
kuendeleza michezo  katika shule zote za msingi na sekondari.
Bwana  Maguzu ambae ni mkufunzi kutoka shirikisho la riadha ya dunia
la  na afisa michezo wa mkoa wa manyara   alidai  lengo la kozi hiyo
kuwajengea uwezo walimu kuweza  kuwatambua ,kuwaendeleza  na kuwalea
wanafunzi wenye viapaji mbalimbali vya kimichezo  ili kuweza  kufikia
ndoto zao.
Alisema kwa tafiti zilizofanywa na  vyama vingi vya michezo katika
nchi zilizo endelea na zinazoendelea zimebaini kuwa michezo pia
hupunguza utoro kwa wanafunzi na kuongeza ufaulu.

Kwa upande wake afisa michezo wilaya ya Mpwapwa bwana  Waziri Lwimbo
alisema  kozi hiyo ni utekelezaji wa igazo la Tawala za mkoa na
serikali za mitaa (TAMISEMI)  la kuzitaka  kila shule kuwa na mwalimu
wa michezo ifikapo 2020 na kozi hiyo ililenga kuwa na walimu 148
lakini walio hudhuria ni walimu  40 tu na alisema  lengo la kozi hiyo
ni kuongezea maarifa walimu wa michezo wa mashuleni.

Miongoni  mwa walimu waliokuwa kwenye kozi hiyo bwana Awalino Makweta
amelalamikia asilimia  kumi zinazotengwa na serikali  kwa ajili ya
michezo  kuwa hazinufaishi ngazi ya chini bali hunafaisha ngazi ya
wilaya na mkoa kitu alicho kisema kuwa kinawakatisha tamaa walimu
ngazi za chini.

Pia  alidai kuwa upungufu maeneo ya michezo na mwamko mdogo wa
wanafunzi na wazazi kuwaruhusu watoto wao kushiriki katika  michezo
kunachania kudumaza vipaji vya watoto.

Comments

Popular posts from this blog

KIZIGO AWAPONGEZA RUWASA,AKERWA NA UHARIBIFU WA MAZINGIRA,AWATAJA MADIWANI.

HISTORIA YA MPWAPWA HATARINI KUTOWEKA

DC KIZIGO ATOA MAAGIZO KWA KWA MAAFISA ELIMU KUKABILIANA NA UKATILI MASHULENI.