Madiwani wa wakumbushwa kujaza tamko la mali pindi udiwani unapokoma.


Mpwapwa.
 

Waheshimiwa Madiwani wa Halmashauri yua Wilaya ya Mpwapwa Mkoani Dodoma, wamekumbushwa kujaza za maadili na kuwasilisha Matamko  ya Mali yao na Madeni katika Ofisi za Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma pindi Udiwani wao unapokoma mwezi Julai 2020.

Hayo yalisemwa na Afisa wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Bw. George Shilla wakati akiwasilisha mada ya Tamko la Mali na Madeni katika kikao cha Baraza la Madiwani la Halimashauri ya Wilaya ya Mpwapwa juzi.

“Jukumu la kujaza  fomu ya maadili  ni jukumu la kila kiongozi wa umma  na halimuhusu mwajiri wake au mkuu wake wa idara hivyo kujaza fomu hizi ni takwa la  kisheria   ya Maadili namba 13 ya Mwaka 1995 inayomtambua Kiongozi wa Umma binafsi kila mmoja na sio hiyari ya kiongozi” alifafanua bwana Shilla.
Aidha Bw. Shilla alidai kuwa   Madiwani wana wajibu wao wa kuwasilisha fomu hizo kwa Kamishna wa Maadili  wenyewe na siyo kutegemewa kuwasilishiwa na Mkurugenzi wa halmashauri kwani Sheria ya Maadili namba 13 ya Mwaka 1995 inatambua Kiongozi wa Umma wao binafsi kila mmoja.
 Hata hivyo bwana  Sshilla  aliwambia madiwani juu ya kuijiepusha na maslahi binafsi  kitu alicho kisema kuwa   vitendo vya mgongano wa maslahii umekua na madhara makubwa kwa maendeleo ya  taifa na wilaya   hivyo kudidimiza maendeleo ya nchi  na wananchi kukosa imani na viongozi wao.
Kwa upnde wake makamu mwenyekiti wa halmasahauri ya wilaya ya Mpwapwa Bwana George Fuime  aliwaomba ofisi ya sekretalieti ya maadili  kuweza kuziwahisha fomu hizo katika halmasahauri ili wawez kuzijaza kwa wakati.
Pia aliwaomba sekretalieti ya maadili kufungua ofisi katika wilaya ili kupunguza mlundikano  wa watumishi kwenye ofisi za kanda  na kuweza kuokoa muda wa   viongozi  hao kuwasilisha fomu hizo kwa wakati.
Akijibu hoja ya ujenzi wa Ofisi za Sekretarieti ya Maadili katika Wilaya ya Mpwapwa, Bw. Shilla  alikili kuwepo changamoto hiyo na alisema  bajeti itaporuhusu ofisi hizo zitajengwa kila mkoa na hatimaye kila wilaya tofauti na ilivyo hivi sasa ofisi hizo kupatikana katika Kanda pekee.

Comments

Popular posts from this blog

KIZIGO AWAPONGEZA RUWASA,AKERWA NA UHARIBIFU WA MAZINGIRA,AWATAJA MADIWANI.

HISTORIA YA MPWAPWA HATARINI KUTOWEKA

DC KIZIGO ATOA MAAGIZO KWA KWA MAAFISA ELIMU KUKABILIANA NA UKATILI MASHULENI.