DARAJA LA GODEGODE LITAFIFISHA MAPATO YA HALMASAHAURI.



WANANACHI wa kata ya Godegode,Pwaga na Lumuma wameiomba serikali kuweza  kurudisha mawasiliano  ya barabara   baada ya  daraja  la Godegode  ambalo ni kuungo muhimu kati ya kata hizo  na makao makuu ya wilaya  kusomwa na maji  katika msimu  wa mvua mwaka huu.

Wanachi wa  kata  hiyo  wametoa  ombi hilo mbele ya naibu waziri wa ujenzi  Mhe Eliasi Kuandikwa (MB) alipokuwa kwenye  ziara  ya  kukakuga ujenzi wa barabara za Mpwapwa na kufika katika  daraja hilo  kuangalia  hali harisi ya  changamoto ya  usafiri katika eneo hilo.

Diwani wa kata ya godegode Bwana Tanu Makanyago amesema daraja hilo ambalo ndio muhimili  mkuu wa  mawasiliano kati ya  kata ya Godegode,Pwaga, na Lumuma kwa mawasiliano .

Aidha Bwana Mkanyago  amesema kutokana na uharibifu  wa daraja hilo  kumepelekea maisha ya watu wanaoishi katika kata hizo kupanda bei kwa  gharama maisha ikiwemo  usafiri,bidhaa madukani  lakini pia kuchukua muda mrefu kwa kuyafikia makao makuu ya wilaya.

Chihimba amesema Chanzo cha Madaraja hayo kusobwa na maji ni uharibifu mkubwa wa mazingira  unaoendelea katika milima, amabapo watu huendesha  shughuli za kibinadamu  katika vilele vya milima na hivyo kusababisha maji kutiririka na kwa kasi   kwenye madaraja na hivyo kupelekea  madaraja kuvunjika .

Mwananchi Mwingine aliyejitambulisha kwa jina  Mwl,Fustine Valelian  alisema  kutokana na kuvunjika kwa daraja hilo  kunatishia pia maisha ya akina mama wajawazito na wagonjwa pindi apatikanpo mgonjwa wa dharula na hivyo hupelekea kuzunguka  sana  na hivyo kutishia usalama wa wagonjwa.

Tena ameongeza  kuwa  endapo daraja hilo  halitajegwa kwa wakati  pia kunatishia halmashauri kukosa mapato  ya ndani yanayo tokana  na mazao  hasa kipindi hiki cha msimu  wa mavuno kwa “maana magari hayatapita tena mpwapwa yatazungukia Lumuma na kutokea kilosa  hivyo daraja hili ni muhimu kwa maendeleo  ya halamsahauri, kiuchumi,kijamii kisiasa pia”aliongea  Mwl Faustine.

Kwa upande  wake Naibu  waziri wa  wa ujenzi  Mhe  Elias Kuandikwa (MB) alisema  kuwa serikali imejipanga kujeresha mawasiliano hayo yaliyokuwa wamekatika   na wananchi hao kuendelea kupata huduma kama awali .

Naibu  Waziri  alisema “ Kwa sasa natambua  adha mnayo  ipata mala baada ya daraja hili kukatika  lakini serikali yenu ni sikivu  na hivyo inajitahidi kurejesha  mawasiliano mala moja  ili kuweza kuwaondolea adha hii hata kwa fedha za dharula”aliongea  Mhe ,Kuandikwa.

Hata hivyo  Naibu waziri  alisema  kuwa changamoto iliyo kuwapo ni kwamba serikali  ilipanga bajeti kidogo   lakini kutokana na uharibifu mkubwa  wa uliosababishwa na  mvua   uliongeza gharama   ujenzi  wa daraja hilo.

Mhe, Kuandikwa liwataka  wananchi  kata ya Godegode  kuweza kuhifadhi na kutunza mazingira  ili kuweza  kutunza miundo mbinu  ya seriakali  iliyopo na inayotarajiwa kujenga katika maeneo hayo ikiwemo  Reli ya  mwendo kasi inayotarajiwa kupita  katika kata ya Godegode.

Comments

Popular posts from this blog

KIZIGO AWAPONGEZA RUWASA,AKERWA NA UHARIBIFU WA MAZINGIRA,AWATAJA MADIWANI.

HISTORIA YA MPWAPWA HATARINI KUTOWEKA

DC KIZIGO ATOA MAAGIZO KWA KWA MAAFISA ELIMU KUKABILIANA NA UKATILI MASHULENI.