UVCCM ACHANE KUTUMIKA - KIMTENDE




Katibu  wa jumuiya ya  umoja wa  vijana wa vijana UVCCM  wilwywni Mpwapwa mkoani  Dodoma bwana Jumanne Kimtende amewataka vijana kuweza kujitokeza kuwania nafasi mbalimbali  za ndani ya chama ya hapo mwakani 2017.
Kimtende ameyasema hayo  jana ofisini kwake alipokuwa akiongea na waandishi wa habari juu ya maandalizi ya kuingia katika chaguzi ndani ya chama znazo talajiwa  kufanyika mwaka 2017 nchini kote.
Kimtende amesema kuwa  vijana wamekuwa walalamikaji wakubwa kuwa  wamekuwa watu wa kufanyiwa maamuzi yanayo wahusu na watu ambao sio vijana, kitu alicho kisema kuwa kinatokana na vijana wenyewe kutojiingiza katika  mfumo wa kufanya maamuzi ambao ni ungozi  ndani ya chama na wao ubaki kutumiwa kuwanadi wagombea kitu alicho kisema kuwa vijan wajitambue na waaache kutumika.
Aidha Kimtende amesema   kuwa lazima vijana wajiandae kuwanai nafasi mbalimbali ndani ya jumuiya hiyo ili kuweza kukiweka chama katika msingi mzuri na ulio imara  na dhabiti  ndani ya chama na serikali
Hata hivyo kimtemnde ametumia  fursa  hiyo  kumshukuru Rais wa awamu ya Tano  Dkt.John Pombe Magufuli  kwa kuwaamini  na kuwapa majukumu ya uongozi  vijana mbalimbali katika seikali na tasisi zake.
Pia amesema viongozi vijana wote walio teuliwa raisi lazima kuweza kuonyesha viongo vya juu vya uwajibikaji  ili raisi aendeee kuwa na imani na vijana  na kuondoa dhana iliyo kuwa imejengeka miongoni mwa jamii kuwa vijana ni taifa la kesho.
Akizungumzia migogoro inayo endelea katika vyama vya siasa kimtende alisema lazima vyama hivyo kuweza kufuta katiba zao za vyama  ili kuweza kuwa na amani  katika vyama vyao.

Comments

Popular posts from this blog

KIZIGO AWAPONGEZA RUWASA,AKERWA NA UHARIBIFU WA MAZINGIRA,AWATAJA MADIWANI.

HISTORIA YA MPWAPWA HATARINI KUTOWEKA

DC KIZIGO ATOA MAAGIZO KWA KWA MAAFISA ELIMU KUKABILIANA NA UKATILI MASHULENI.