CHAMA CHA WALIMU CHAIDAI SERIKALI MILION 412.7 MPWAPWA



 Na noel Stephen  - Mpwapwa
 CHAMA  cha walimu wilayani mpwapwa  mkoani Dodoma  kinaidai serikali kiasi cha tsh milioni  412,701,983 kama madeni ya mapunjo ya mishara, pesa za likizo  na  upandishwaji wa madaraja. Kwa walimu  wake kwa kipindi cha kuanzia  desemba 2012 na  hadi  feb 2014.
Kauli  hiyo imelotelewa na  katibu  wa chama hicho wilayani hapa Donard Kisamaba  alipokuwa akisoma taarifa ya utekelezaji katika  mkutano mkuu wa mwaka wa chama hicho uliofanyika katika ukumbi wa ccm   mjini mpwapwa.
Kisamba  alisema kuwa   madeni hayo ni  mapunjo ya  mishahara   na makato mbalimbali ambayo walimu  wanamdai mwajili kama haki zao za msingi  kazini .
ALISEMA  serikali ikiwa katika mchakato wa   matokeo makubwasasa (big result now) katika idara ya elimu hayatapatikana    kama  serikali  itaendelea kuviona vyama vya wafanya kazi  kama ni adui wa serikali au  wachochezi wa migogoro mahali pa kazi   kitu alicho kisema kuwa ni mtazamo hasi wa serikali kwa vyama hivyo.
 AIDHA alisema kuwa vyama vya wafanyakazi  sio adui wa serikali bali vipo kwa ajili ya  kuisaidia serikali    kuweza kutoa haki zinazo stahili kwa mtumishi ili mtumishi awe n maisha bora na aifurahie kazi yake.
ALIDAI   ili kuweza kupima matokeo makubwa sasa serikali iweze kulipa  madeni inayo daiwa   kutoka  kwa wafanya kazi “ bila hivyo matokeo makubwa yatabaki katika mipango na kwenye makaratasi lakini hayataonekana kwa jamii”alisema na kuongeza Kisamaba.
Katika  mkutano huo uliombana na uchuguzi wa  viongozi mbalimbali   wa kukiongoza chama hicho ambapo   John Kipalamoto  alibuka mwenyekitiki mpya wa chama hicho  kwa  kumshinda mpinzani wake  Edward Mwamakula kwa kura  32 kwa 29,
Nafasi ya mwakilishi wa  sekondari walibuka OMARY JUMA  NA AISHA Hamisi  wakati nafasi ya mwakilishi shule ya msingi alichaguliwa  Savera  Lasoya na  John kipalamoto alichaguliwa mwakilishi vyuo vya ualimu  nafasi aliyo jitoa baada ya kushinda nafasi  ya umwenyekiti wa chama hicho.

Comments

Popular posts from this blog

KIZIGO AWAPONGEZA RUWASA,AKERWA NA UHARIBIFU WA MAZINGIRA,AWATAJA MADIWANI.

HISTORIA YA MPWAPWA HATARINI KUTOWEKA

DC KIZIGO ATOA MAAGIZO KWA KWA MAAFISA ELIMU KUKABILIANA NA UKATILI MASHULENI.