MSIMAMO WA SERIKALI KUHUSU WATUMISHI HEWA.


SERIKALI imetangaza msimamo wake kwa watumishi ambao walibainika kuwa na vyeti feki na wale wasiokuwa na vyeti vya kidato cha nne kuwa hawana madai yoyote ya kuidai serikali baada ya Rais John Magufuli kutangaza kufanyika kwa uhakiki kwa watumishi wa umma.


Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa idara ya uendelezaji sera, Mathias Kabundugulu,wakati akizungumza kwenye kikao cha kazi cha kujadili masuala ya utawala na rasilimali watu kwa mamlaka za serikali za mitaa, wizara na mikoa.

Amesema watumishi ambao wamebainika na kuondoka wenyewe, wamefutwa kwenye orodha ya watumishi wa umma na hawana madai wanayodai serikalini huku amesema pamoja na zoezi hilo kukamilika kwa muda ambao umepangwa, wapo baadhi ya maafisa utumishi wameendelea kuwafumbia macho watu wasiokuwa na vyeti vya kidato cha nne.

Naye katibu mkuu wa wizara ya Tamisemi, Mhandisi Mussa Iyombe, amesema kumekuwepo na changamoto mbalimbali zinazofanywa na maafisa wa utumishi katika halmashauri mbalimbali nchini.



Selemani Jafo ni Waziri wa nchi, ofisi ya rais, tawala za mikoa na serikali za mitaa, Tamisemi, , amewataka makatibu wakuu wa wizara yake na wale wa ofisi ya rais utumishi, kuangalia upya miongozo na sheria ambazo zimekuwa kandamizi kwa watumishi wa umma.


MWISHO

Comments

Popular posts from this blog

KIZIGO AWAPONGEZA RUWASA,AKERWA NA UHARIBIFU WA MAZINGIRA,AWATAJA MADIWANI.

HISTORIA YA MPWAPWA HATARINI KUTOWEKA

DC KIZIGO ATOA MAAGIZO KWA KWA MAAFISA ELIMU KUKABILIANA NA UKATILI MASHULENI.