KIPINDIPINDU CHAUWA WAWILI MPWAPWA.




 JUMLA  ya watu  94  katika  wilaya ya Mpwapwa  katika  mkoa wa Dodoma wamegundulika kuumwa  ugonjwa wa kipindupindu wakati wawili tayari wamesha fariki Dunia kutokana na ugonjwa huo.
Hali hiyo imeelezwa  mganga mkuu wa  ya wilaya ya Mpwapwa  Dkt Siad Mawji alipokuwa akiongea  na waaandishi wa  habari juu ya kuwapo kwa wa ugonjwa huo katika wilaya hiyo na kusabaisha  hali ya wasiwasi kwa wakazi wengi wa wilaya hiyo na viunga vyake.
Dkt Mawji alisema  kuwa mgonjwa wa kwanza  aligundulika  octoba  26  mwaka huu  akitokea kata ya Mweznele  na wagonjwa wengene waliendelea kujitokeza kutoka katika kata mbalimbali hadi kufikia wagonjwa  94 tangu ugonjwa huo uanze hadi sasa.
Hata hivyo alisema w wagonjwa wengine  walitokea katika kata ya Tambi,Mpwapwa mjini,  Lumuma na Matomondo na kufanya  wagonjwa wote kufikia wagonjwa 94.
Aliongeza kuwa  hada kufikia jana ni wagonjwa kumi na watano 15 ndio  waliolio lazwa  katika kambi maluum  ya kuwashughulikia  wagonjwa  wa kipindupindu  na wagojwa 71 tayari hali zao zimekuwa nzuri  kurudi tena majumbani mwao wakati wagonjwa wawili walifariki dunia.
Aidha alisema  chanzo kikubwa cha ugonjwa huo katika kata hizo ni kutokana na kuwapo kwa tataizo la uhaba wa maji  na hivyo watu hulazimika kutumia maji ambayo si safi na salama  ambayo ni maji ya mtiririko baada ya visima vyao kuharibika .
“Katika katazenye ugonjwa wa kipindupindu tatizo kubwa la maji safi na salama  kutokana na  hali hiyo  watu wanatumia  maji amabayo si safi na salama  ambayo ni maji ya visima  vifupi na maji ya mtiririko ambayo si salama sana”aliongea  aiongea Dkt Mawji
Alisema chanzo kingine   kilicho changia kuenea kwa ugonjwa huo kirahisi ni  watu wengi  katika kata hizo kuto kufuata kanuni za afya  na kuto kuwa na vyoo  pia mwingiliano wa watu katika kata za mipakani kama kiosa na Gairo,kusababisha  ugonjwa huo kulipuka kutokana na husaidi kusambaza wadudu hao kirahisi na maji machafu kunchanganyika  na maji ya visima.
Alisema  kutokana  hali hiyo wamechukua  hatua ya kutibu maji yote ya visima  kwa kuyawekea  dawa maluum  ilikuweza kuweza kuua wadudu wote  ambao wanaweza kusambaza  ugonjwa huo kwa watu kirahisi na kuwahamasisha watu kufuata kanuni za afya.
Dkt Mawji alisema  kwa  sasa wananchi  wanapatiwa  elimu  ya kuhakikisha  wanaishi  katika  mazingira  salama  ikiwa  ni pamoja  na kuwa  na vyoo  bora  kwa lengo la kujiepusha  na mlipiko wa  magonjwa kama hayo   na magonjwa mengine ya mlipuko.
Mbali na hilo alisema  katika kata ambazo wagonjwa wametoka kwa wingi wametakiwa  kuunda kamati za kudhibiti na kutoa elimu  ya kanuni za afya  na sula la usafi wa mazingira ili watu  na jamii hiyo kuishi  katika mazingira mabayo ni salama zaidi.
Katika  wilaya hii tayari watu wawili kutoka katika kata ya Mwezele,na Lumuma wamesha poteza maisha  kautokana na  ugonjwa huo.
Kwa sasa katika mkoa Dodoma wilaya ya Mpwapwa ni miongoni  mwa wilaya ambayo ugonjwa wa kipindupindu umeumkumba kwa kasi  ukiachilia  mbali   wilaya ya kilosa na Gairo mkani Morogoro .
Mwisho.


Comments

Popular posts from this blog

DC KIZIGO ATOA MAAGIZO KWA KWA MAAFISA ELIMU KUKABILIANA NA UKATILI MASHULENI.

HISTORIA YA MPWAPWA HATARINI KUTOWEKA

KIZIGO AWAPONGEZA RUWASA,AKERWA NA UHARIBIFU WA MAZINGIRA,AWATAJA MADIWANI.