VIONGOZI WA UMMA WAKUMBUSHWA KUWA VYEO NI DHAMANA.



 Na noel Stephen –Mpwapwa

  Viongozi wa  umma , viongozi wa  kuteuliwa,  na viongozi wa kuchaguliwa  wilayani mpwapwa wameaswa   kuto tumia  dhamana waliyo pewa na wananchi  kama miradi ya  ya kujinufaisha binafsi

Lai hiyo imetolewa  na   Kamanda wa kuzuia na kupambana na rushwa wilayani mpwapwa mkoani Dodoma Michael Makoba  alipo kuwa akiongea na waandishi wa habari kwa mahojianao maluumu.

Makoba  amesema  kuwa kumekuwako na  kushuka kwa maadili ya viongozi wa umma  ambao hutumia  vyeo vyao kama mitaji ya kujinufaisha na kuwaacha watu wanaowaongoza wakiwa katika lindi kubwa la umaskin na  kusahau kuwa  cheo ni dhamana na kuwatumiakia wananchi hasa  walio katika  sekta zao.

Aidha  Makoba  amedai kuwa   sheria ya  ya maadili  ya viongozi wa umma  na  na 13ya mwaka 1995 sura 398  toleo la 2002 inawahimiza watumishi wa umma kuboresha nguzo ya utawala bora na uwajibikaji  kwa wananchi katika ngazi zote za serikali hasa ngazi ya serikali za mtaa kwa kuzingatia dhana ya maboresho ya serikali za mitaa( ugatuzi wa madaraka  katika  serikali za mitaa.

Ameongza kuwa japo kuwa serikali imekuwa ikipeleka pesa nyingi katika halmashuri nyingi za wilaya lakini ndiko kwenye malalamiko mengi ya wanachi na miradi mingi kutekeleza  chini ya viwango kitu alichokisema kuwa kinaashilia mianya ya rushwa na kuto kuwajibika kwa watumishi wa serikali.

Alisema kuwa amani haiwezi kukuzwa katika nchi yeyote mpaka hapo itakapo kuwa  na maadili katika jamii na  hasa

 kwa kila mmoja  kuwajibika  na kutimiza wajibu wake na wajibu kwa taifa lake na jamii anayo itumikia  kwa kuzingatia haki kwa kila mmoja.

 Pia amesema kunaonekana  dalili za kupungua kwa maadili kwa viongozi wa umma  kwa kushidwa kuvumiliana katika  umoja wa kitaifa na kisiasa,  vitu vinavyo tishia  amani ya nchi  kwa baadhi ya watumishi  kuendekeza  mambo ya kuto kuwajibika ,rushwa,ubinafsi, na upendeleo.

Amedai kuwa mambo yanayo endelea nchini kwa  kwa baadhi ya watumishi wa umma kutuhumiwa na   kashfa za rushwa zinakatisha tama wanachi na kupelekea wanachi kuwakatia viongozi wao walio madarakani  na kushidwa kuwachukulia hatua za kinidhamu.

 Mbali na hilo  alisema sekretalieti ya maadili ya viongozi wa umma   wamejipanga kuhamisisha jamii kupitia vyombo ya habari mikutano  ya hadahara  pamoja na kutumia asasi ziziso kuwa za kiserikali kuweza kueneza   dhana hii kwa  wananchi wengi ili waweze kusimamia rasilmali zao zinazo wazunguka

Kwa upande wake mchambuzi wa masula ya siasa na jamii mwl Issack Chibwae amesema chanzo cha kushuka kwa maadili  ni  baada ya kuanzishwa  kwa azimio la  Zanzibar  lililo ruhusu kuvunjwa kwa  sheria  masharti ya azimio la  Arusha la mwaka 1973 kinyume na mtazamo wa  mwasisi wa taifa hili mwl Nyerere.

Alisema sheria hiyo ilisimamia maadili kwa  watumishi wa uuma na ndio ilikuwa ikisimamia  viongozi kuto jilimbikizia mali na kukataza mtumishi kuwa na mishahara miwili.

Na ameongeza kuwa  “baada hapo hali ikawa tofauti  na ndo sababu kubwa ya kuanza kuvujika kwa maadili ya viongozi wa umma na kutufikisha hapa tulipo”alisema Chibwae.
.







Comments

Popular posts from this blog

KIZIGO AWAPONGEZA RUWASA,AKERWA NA UHARIBIFU WA MAZINGIRA,AWATAJA MADIWANI.

HISTORIA YA MPWAPWA HATARINI KUTOWEKA

DC KIZIGO ATOA MAAGIZO KWA KWA MAAFISA ELIMU KUKABILIANA NA UKATILI MASHULENI.