RAISI AZITKA HALMASHAURI KUTUMIA VIZURI PESA ZA MFUKO WA BARABARA



Na Stephen noel- mpwapwa
 RAISI wa jamuhuri wa muungano wa Tanzania  Dkt Jakaya Mlisho Kikwete  amezitaka halamashauari zote nchini kuweza   kutunza na kutumia vizuri fedha za ruzuku za barabara  zinazotolewa na serikali ili ziweze  kuondoa kero za barabara  vijijini.
Raisi Jakaya aliyasema hayo katika siku yake ya pili ya ziara mkoani Dodoma wilayani mpwapwa alipokuwa  akiongea na wananchi wa mpwapwa katika viwanja vya shule ya msingi  Mtejeta.
Dkt   Jakaya alisema kuwa  serikali imewekeza pesa  nyingi sana katika  ruzuku ya barabara kwa serikali  lakini pesa hizo zimeonekana  kuto kuondoa kero ya barabara vijijini  kutoka na  baadhi wa watendaji wa halmashauri za  wilaya kushidwa kuzitumia pesa hizo kwa malengo yaliyo kusudiwa  bali hujinufaisha wao wenyewe.
Alisema lengo la serikali ni  kuweza  kuunganisha  barabara za vijijini  ili sehemu nyingi za vijijini ziweze kufika kirahisi na kurahisha maisha ya watu na kukuza uchumi kwa kupata  faida katika mazao yao wanayo lima kwa kuyauza kwa bei kubwa inayo  endana na hali ya sasa.
Aidha Kikwete alisema mwaka 2008  serikali ilikuwa inawekeza  kwenye halmashauri kiasi cha shilingi  billion 55 kufikia  mwaka 2012 serikali imekuwa ikiwekeza pesa kiasi  cha shilingi billion  751 amabocho  alisema kuwa nikiasi kikubwa cha pesa  ambacho kinatakiwa kionyeshe  matokeo  kwa  jamii na kuondoa kero  za barabara  vijijini.
“Ikumbukwe kuwa miaka  mitano  nyuma serkali ilikuwa inawekeza kiasi cha shilingi  billion 55 kwa halmashauri kwa ajili ya shughuli za barabra vijijini  hii ni pesa nyingi  sana ambazo tunatamani zionyeshe matokeo kwa jamii lakini halamashauri hizi zimekuwa zikizitumia vibaya  pesa hizi  sehemu penye mchwa mingi kwenye halmashauri  pesa hizi haziwezi kuonyesha matokeo ila pasipo na mchwa pesa hizi zinaweza kuwa ni mkombozi  kwa jamii kuhusu masula ya barabara vijijni.”aliongea Rais
Kuhusiana na suala la elimu Dkt kiwete  amewataka  maafisa elimu na wadau wa elimu wilayani hapa kuweza kutafuta sababu zinazo pelekea  wanafunzi wengi kuweza  kuacha shule   njiani kabla ya kufika darasa la saba au kidato cha nne .
Alidai kuwa kwa mwaka   2007 wanfunzi waliondikishwa darasa la kwanza walikuwa  wanafunzi 9486 wakati walio fanikiwa kuhitimu  darasa la saba walikuwa  6554 ambapo wanafunzi  3430 hawakumaliza darasa la saba
Kwa kidato  cha kwanza  mwaka 2010  wanafunzi 2596 waliweza kuanza kidato  cha kwanza lakini walioweza  kuhitimu kidato cha nne walikuwa wanafunzi  1967  ambapo wanafunzi 629 hawakuweza  kuhitimu  kidato cha nne, “nawaaagiza maafisa elimu nataka mkae chini mtafute sababu za hawa wanafunzi kwanini  hawamalizi shule kama wanaolewa basi sheria isimamiwe vizuri akamatwe aliye oa mwanafunzi afunguliwe mashitaka tunataka huyu mtoto wa kike asome na asiwe mke wa mtu”alisisitiza Rais.
Akizungumzia masula ya  maabara aliwataka viongozi wa wilaya hiyo kuongeza nguvu katika ujenzi wa maabara hizo kutokana na kile alicho kisema hajaridhishwa na kasi ya  ujenzi wa maabara hizo katika wilaya hiyo amewagiza  viongozi wa wilaya hiyo kumaliza kazi hiyo mapema ifikapo Dec, 2, 2014 na alisema zaidi ya hapo hataitaji maelezo zaidi kutoka kwa kiongozi yeyote.
Kwa upande wake waziri wa maji  Pro.Jumanne Magembe  alisema kutoka na  adha ya maji  inayo ikumba mji wa mpwapwa na viunga vyake kutokana na mamlaka ya  maji wilayani hapo kushidwa kulipia Ankara za umeme wanazo diwa  na shirika la ugavi umeme Tanzania  TANESCO  alisema wizara itailipa  tanesco kiasi cha shilingi billion 82 inazo idai mamlaka ya maji hapa mjini mpwapwa ili kuweza kuimaliza kero ya maji hapa mjini mpwapwa na kubadilisha mfumo wa mita za ruka katika mashine za maji na kuweka mita za kawaida.
Pro Magembe amzitaka  tasisi za serikali  zinazodaiwa na mamlaka hiyo  Ankara za maji kuweza kulipa  Ankara hizo mapema iwezekanavyo.
Raisi kikwete katika ziara yake wilayani mpwapwa aliweza kuweka jiwe la msingi katika miradi kadhaa ikiwemo ujenzi wa barabara ya  rami inayotoka mbande kongwa na mpwapwa yenye urefu wa km 101 na jenzi wa daraja  la gulwe lenye mita za mraba 70 ilanalo unganisha  jimbo la mpwapwa na jimbo la kibakwe.


Comments

Popular posts from this blog

KIZIGO AWAPONGEZA RUWASA,AKERWA NA UHARIBIFU WA MAZINGIRA,AWATAJA MADIWANI.

HISTORIA YA MPWAPWA HATARINI KUTOWEKA

DC KIZIGO ATOA MAAGIZO KWA KWA MAAFISA ELIMU KUKABILIANA NA UKATILI MASHULENI.