GEREZA LA MPWAPWA LAKABILIWA NA UHABA WA NYUMBA.



Gereza la Mpwapwa mkoani Dodoma linakabiliwa na uhaba mkubwa wa nyumba za askari na kusababisha askari kukaa kwenye nyumba ndogo na zisizo na hadhi kwa askari hao.
Haya yamebainishwa na Mkuu wa gereza la mpwapwa mrakibu mwandamizi wa jeshi la magereza bwana Joseph Tembo ameanza jitihada za kupunguza uhaba wa nyumba za askari kwa kuwatumia wafungwa kufanya kazi hizo.
Bwana tembo amesema kuwa mpaka sasa wamefyatua na kuchoma zaidi ya tofali elfu harobaini na tano ambazo zitatumika kujengaea nyumba sita za watumishi gereza hilo,Tembo amesema serikali inazitaka magereza kuwa sehemu ya kuwabadilisha tabia na mtazamo kwa wafungwa wale wanao kinzana na sheria .
 
 
Mkuu wa Gereza la Mpwapwa Joseph Tembo akizungumzia hali halisi ya Mkakati wa Uboreshaji wa nyumba za Askari.
Adha amesema kukamilika kwa nyumba hizo kutapunguza adha ya nyumba kwa askari kumi nambili kupata  makazi bora na  ya kisasa ambapo hapo awali walikuwa wanatumia nyumba za matope na dogo ambapo zolikuwa zinapelekea msongamano kwa maskari hao hasa kwa wenye familia kubwa na, kuongeza kuwa tayari washachimba misingi ya nyumba mbili ambazo ujenzi wake utaanza hivi punde na lengo la gereza hilo ni kufyatua tofali laki moja na elfu hamsini.

Comments

Popular posts from this blog

KIZIGO AWAPONGEZA RUWASA,AKERWA NA UHARIBIFU WA MAZINGIRA,AWATAJA MADIWANI.

HISTORIA YA MPWAPWA HATARINI KUTOWEKA

DC KIZIGO ATOA MAAGIZO KWA KWA MAAFISA ELIMU KUKABILIANA NA UKATILI MASHULENI.