AKINA MAMA WAJIFUNGULIA MAJUMBANI BAHI.
AKINA
  mama wajawazito wapata 47 katika kata ya mpalanga Wilaya ya Bahi Mkoani
  Dodoma wametajwa kujifungulia nyumbani katika kipindi cha kuanzia mwezi july
  hadi septemba mwaka huu jambo linalohatarisha maisha ya mama na mtoto. 
Zipo
  sababu mbalimbali ambazo zinatajwa kupelekea akina mama wajawazito
  kutojifungulia katika zahanati na vituo vya afya ikiwa ni pamoja ni huduma
  hiyo kukosekana katika baadhi ya vijiji,miundombinu kutokuwa rafiki na
  pengine kupelekea akana mama hao hujifungulia njiani. 
akisoma
  taarifa ya utekelezaji wa shughuli za maendeleo katika kikao cha baraza la
  madiwani wa halmashsuri hiyo cha robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2017/18,
  diwani wa kata hiyo Daudi Magalamile amesema kuwa sababu hizo zimekuwa ni
  changamoto katika maeneo yao. 
Diwani
  huyo amesema hapo awali kulikuwa na utaratibu wa kuwatoza faini akina ambao
  wanajifungulia nyumba ambao utaratibu huo uliwafanya akina mama hao
  kujifungulia katika vituo vya afya na zahanati lakini baada ya kuondolewa
  faini hiyo akina mama wengi wamekuwa wakijifungulia nyumba. 
Kufuatia
  changamoto hiyo diwani huo ameeleza juhudi na hatua za ujenzi wa zahanati
  katika kijiji cha chililo zilianzishwa lengo ikiwa ni kutatua tatizo hilo
  licha ya kuwa ujenzi wa kituo hicho umekuwa wa kusuasua. 
Kutokana
  na kusuasua kwa ujenzi huo mwenyekiti wa halmashauri ya Wilaya ya Bahi
  Danford Chisomi akaahidi kuchangia mifuko 10 ya saruji ili kusaidia
  ukamilishaji wa zahanati hiyo. 
Kwa
  upande wake diwani wa kata ya ibugule Blandina Magawa amemtupia lawama
  muuguzi wa zahanati ya kijiji cha ng,ome kwa kushindwa kuwahudumia akina mama
  wajawazito na kupelekea kujifungulia nje ya zahanati hivyo kuomba halmashauri
  kuwatafutia mganga mwingine. 
Ili kukabiliana na changamoto hiyo serikali na wadau mbalimbali
  wa afya wana kila sababu ya kuchukua hatua madhubuti za kuendelea kupunguza
  tatizo la akina mama kujifungulia nyumbani au njiani ili kuweze
  kupunguza vifo vya mama na mtoto. 
Mwisho. 
 | 
 
Quick Reply 
 | 
 
Comments
Post a Comment