MAENDELEO YA MPWAPWA YAMNYIMA USINGIZI DC,AWATAKA WACHIMBAJI WALIPE KODI.
SERIKALI wilayani Mpwapwa Mkoni Dodoma imewataka wachimbaji wadogo wa madini Kuweza kulipa kodi ya serikali ili kuweza kufikia Tanzania ya Viwanda na uchumi wa kati ifikakapo 2015. Kauli hiyo ilitolewa jana na Mkuu wa wilaya ya Mpwapwa bwana Jabir Shekimweri alipokuwa akifunga mafunzo ya siku moja yaliyo andaliwa na shirika la wachimbaji madini Wanawake Tanzania(TAWOMA) Shekimweri alisema kuwa kuwa Mpwapwa pamoja na kujaliwa madini ya aina nyingi na yadhamani lakini wilaya hiyo aiendani na maendeleo yalikuwanayo kitu alichosema kuwa kinatokana na matumizi mabaya ya rasilimali hizo au usimazi mbovu wa rasilimali hizo au matumizi mabaya mali hizo ambayo ni za watanzania wote. ALISEMA “ukiangalia Mpwapwa haiendanani na hostoria ya wilaya hiyo kimaendeleo japo kuwa na kuwa na Neema ya wilaya hiyokujaliwa vitu vingi sasa nataka mlipe kodi ya serikali ilitufikie uchumi wa viwanda na uchumi ...