SERIKALI YASHAURIWA KUWAPA KIPAUMBELE CHA AJIRA WALIMU WANAO JITOLEA KWANZA.



 


Baadhi ya wanachuo wa chuo cha ualimu hapa Mpwapwa.

SERIKALI imeshauriwa kuweza kuwapa kipaumbele walimu waliohitimu nmafunzo Yao na wakaamua kujitolea Katika shule mbali mbali hapa Nchini  Ili kuweza kuziba pengo la upungufu wa walimu Katika shule za Msingi na sekondari 

Ushauri huo ulitoleaa na mdau wa Elimu na mbobezi wa masuala ya Elimu hapa Nchini 
Mwl Dkt ,Wiliam Hugo Ndipo alipokuwa akiongea na chombo hiki Nyumbani kwake mjini Mpwapwa (Mji mpya).

Dkt Ndimbo alisema  kwa sasa shule nyingi hapa Nchini zinakabiliwa na uhaba mkubwa wa walimu  hasa shule za vijijin kabisa  japo kuwa vyuo vy kati na vyuo vikuu vikiendelea kutoa wahitimu Kila mwaka .

Alisema " kiukwel kila mwaka vyuo hivi bimeendelea kutoa  wahitimu  wa vyuo vya kati na vyuo vikuu lakin upungufu Bado upo na hivyo husabanisha utoaji wa Elimu kuto kuwa SAWA kati ya maneo  ya mjini na vijijin ,lakin hawa walimu wanaenda wapi mala baada ya kuhitimu wapo ambao wamejiajili ,wapo walio ajiliwa shule binafsi na wapo wanajitolea Katika maeneo wanako toka" alieleza

Ila pamoja na baadhi ya walimu kujitolea lakin inasikitisha  pindi Ajira zinapotoka  utangaaa waliokuwa wanajitolea pamoja na kuwa na vigezo hukosa nafasi wale wengine walikuwa labda kwenye Ajira binafsi au shule binafsi  ndio hupata nafasi kwanza kitu kinacholeta  ukakasi  wa uzalendo na utu Kwa wale wanao jitolea" alieza zaidi 

Alisema ili kuweza kurudisha uzalendo na usawa lazima wanaojitolea wapewe nafasi kwanza  " Tena wapewe maeneo Yale yale wanayojitolea  Ili kupunguza gharama Kwa serikali  pindi wakipangiwa maeneo mengine na kusumbua kutaka kuhama baada ya muda mfupi .

Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolijia  Prof Aldolf Mkenda.

Wizara ya Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) inaeleza kuwa hadi Februari, 2023 ilikuwa na uhitajii wa  walimu katika shule za msingi  ni 362,189 kwa kutumia uwiano wa 1:45 (Mwalimu mmoja kwa wanafunzi 45).

Hata hivyo walimu waliopo ni 175,864 ambao wanafundisha wanafunzi milioni 12.36 waliopo nchi nzima katika ngazi hiyo ya elimu. Hiyo ni sawa na kusema kwa wastani, mwalimu mmoja anafundisha wanafunzi 70. 

Uwiano huo uko juu kuliko mapendekezo ya Serikali ya mwalimu mmoja kufundisha wanafunzi wasiozidi 45 katika darasa moja. 

​Ili kuziba pengo hilo wanahitajika walimu 186,325 au sawa na asimilia 51.44 au zaidi nusu ya walimu waliopo sasa. 


Shule ya MsingWanafunzi wa i moja wapo Mpwapwa.
Pia, mahitaji ya walimu kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum kwa shule za msingi ni walimu 4,462 ambapo waliopo ni 1,517 na upungufu ni walimu 2,945 sawa na asilimia 66. 

Hata wakiajiriwa walimu wote hao, tatizo la uhaba wa walimu katika shule za msingi linaweza lisiishe kabisa kwa sababu kila mwaka idadi ya wanafunzi wa darasa la kwanza wanaondikishwa inaongezeka

Tatizo la uhaba wa walimu siyo tu la shule za msingi bali linazikumba hata shule za sekondari hasa zinazomilikiwa na Serikali.

Tamisemi inaeleza kuwa mahitaji ya walimu kwa shule za sekondari hadi kufikia Februari mwaka huu ni 174,632. 

“Waliopo ni 84,700 na upungufu ni walimu 89,932 sawa na asilimia 51.5. Mahitaji ya walimu kwa shule za Sekondari yanatokana na masomo yanayofundishwa,” amesema Waziri Kairuki. 

Wachambuzi wa masuala ya elimu akiwemo Richard Mabala wanasema uhaba wa walimu unawakosesha fursa wanafunzi kupata maarifa kwa ukamilifu kuwawezesha kufaulu mitihani yao na kupata stadi muhimu kuboresha maisha yao. 

Mwisho.

Comments

Popular posts from this blog

KIZIGO AWAPONGEZA RUWASA,AKERWA NA UHARIBIFU WA MAZINGIRA,AWATAJA MADIWANI.

HISTORIA YA MPWAPWA HATARINI KUTOWEKA

DC KIZIGO ATOA MAAGIZO KWA KWA MAAFISA ELIMU KUKABILIANA NA UKATILI MASHULENI.