WANANCHI WALALAMIKIA HUDUMA HAFIFU TANESCO MPWAPWA.
WANANCHI wa wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma wamelalamikia huduma duni na hafifu za shirika la ugavi la umeme TANESCO wilayani hapa kuwa zinawarudisha nyuma kimaendeleo Wananchi hao waliyoataoa malalamiko yao walipo kuwa wakiongea na mwandishi wa habari juu ya kuto ridhishwa na huduma zitolewazo na shirika hilo kuwa zimekuwa za kusuasua na huchukua muda mrefu kushughulikiwa kero zao kitu walicho kisema kuwa kinachangia kudumaza uchumi na maendeleo ya watu wa Mpwapwa. Mmoja wa wananchi wa wilaya hiyo bwana AHMAD UTAMU alisema kumekuwa na ubabaishaji wa ujazaji wa ramani pindi unaomba huduma za kuunganishiwa umeme ndani ya nyumba,kukatika katika kwa umeme mara kwa mara kunakopelekea baadhi ya watu kuunguza vitu vyao na kuwasababishia hasara kubwa. Aidha bwana Ahmad alisema kuwa shirika hilo limekuwa likikiuka mkataba wa huduma kwa mteja ...