Posts

DR ,ULIMBOKA AOKOTWA PORINI AKIWA HOI.

Image
1 digg Dk Ulimboka Mwenyekiti wa Jumuiya ya madaktari  nchini, Dk Stephen Ulimboka amelazwa katika hospital ya Taifa ya Muhimbili baada ya kuokotwa katika pori la Pande nje kidogo ya jiji akiwa taaban.Inasemekana Dk Ulimboka alitekwa jana na watu wasiojulikana.  kwa taarifa zaidi soma gazeti la mwananchi kwa taarifa zaidi.

MKUU WA WILAYA AHIDI KUJIUZULU AKISHIDWA KUPAMABANA NA RUSHWA

  Na Noel stphen mpwapwa ..   MKUU WA WILAYA ya   Mpwapwa bawana   CHRISTOPHER KANGOYE ameahidi   na amesema yuko tayari kujuuzuru ukuu wa wilaya kama   endapo atamkamata mtu yeyote na rushwa   harafu huyo mtu asijukuliwe hatua za kisheria na vyombo vinavyo husika.   Bwana Kangoye ameyasema hayo   mwishoni   mwa wiki   wilayani mpwapwa alipo kuwa akifungua   mjadala   wa wazi   wa Tasisi ya Kuzuia na kupambana   na Rushwa Wilayani hapo mkoni Dodoma   (PCCB)   Alisema kuwa yeye amekuja wilayani mpwapwa kwa   ajili ya kuwatumikia wana mpwapwa na   sio kutumikiwa na wana mpwapwa,   hivyo alisema hapendi kusikia   malalamiko ya wanancjhi juu ya   kunyanyaswa na baadhi ya watendaji wa serikali na tasisi zake kwa kuombwa rushwa kwenye haki zao za msingi kama   afya   elimu maji   na utumishi. Aalisema   kuwa umaskini haiuwezi kuondoka kwa kuendekeza   rus...

BILIONI 300 ZA VIGOGO ZATIKISA NCHI,

Image
Bilioni 300 za vigogo Uswisi zatikisa nchi  Send to a friend Tuesday, 26 June 2012 21:38 0 digg ZITTO AMTAKA PINDA ATAJE WAHUSIKA, WANANCHI WATAKA FEDHA ZIREJESHWE, MABILIONI ZAIDI YAIBWA MTANDAONI KUBAINIKA kwa Sh303.7 bilioni zilizofichwa katika akaunti za vigogo wa Serikali na wanasiasa nchini Uswisi, kumetikisa nchi huku shinikizo likitolewa kwa vyombo vya dola kuchunguza haraka na kuchukua hatua za kisheria, ikiwamo kurejesha fedha hizo. Jana kutwa nzima, gazeti hili lilipokea simu kadhaa kutoka kwa wasomaji wake wakiwamo wabunge na mawaziri, huku baadhi wakichangia maoni kwenye tovuti na mtandao mbalimbali ya kijamii, wakitaka kujua majina ya wamiliki wa akaunti hizo. Bungeni mjini Dodoma, Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe aliitaka Serikali kuchunguza tuhuma hizo kisha kuwachukulia hatua watu sita wanaotajwa kwamba wanamiliki akaunti zenye mabilioni hayo ya shilingi chini Uswisi. Fedha hizo zimebainishwa...

ASASI ZA KIRAIA ZA LALAMIKIWA KUTO KFIKIA MALENGO.

Na  noel Stephen Mpwapwa I mebainika kuwa  Asssi za kiraia  nchini  japo kuwa  zimefanya kazi kubwa kwa jamii na  serikali lakini bado hajijafikia malengo yanayo takiwa kutokana na rasilimali zilizo tumika na matokeo yanayo onekana.    H ayo yamebainishwa  na  Bwana  AYUBU KUPONA  afisa mipango kitengo cha Sera  na  Maendeleo katika ukumbi wa  Hoteli ya Blue Pearl mjini  Dar –ES-Salaam  alipo kuwa   akifungua  warsha ya  watendaji Wakuu wa AZAKI TANZANIA. Bwana kupona  alisema kuwa  japo kuwa asasi nyingi  zimefanya kazi   nchini bado  kuna changomoto ya kuyafikia malengo  yaliyo kusudiwa  ingawa pesa nyingi imetumika katika kitengo hicho kitu alicho sema kuwa matokeo haya endani  na kiwango cha rasilimali zilizo tumika . Aidha alidai kuwa   asasi nyingi nchini bado hazijafanya kazi za kufuatilia  mambo makuu ya  kita...

MATATANI KWA DAWA ZA DILI

Na   noel   Stephen Mpwapwa Jeshi la Polisi Wilayani Mpwapwa Linamshikilia mfanya biashara mmoja wa kijiji cha Ng’hambi Bwana   Jeremia mhogo   kwa tuhuma za kukamatwa na dawa za kutibu binadamu      na   baadhi ya dawa hizo zikiwa na nembo ya MSD   kinyume na sheria.   MKUU wa polisi   wilayani mpwapwa   Bwana   JEREMIA SHILA   ametibitisha kutokea kwa tukio hilo na amesema mtuhumiwa bado anashikiliwa na polisi lakini kwa sasa yuko nje kwa dhamana . Bwana Shila   alisema kuwa   mtuhumiwa huyo alikamatwa na maafisa AFYA   WA WILAYA    walio enda   kufanaya uchunguzi katika eneo hilo na ndipo walio   mbaini mtuhumiwa huyo na alisema kuwa   maelezo mazuri anayo bwana afya wa wilaya     Bwana Plaivate Lweimamu amabae alikuwa ndiye mkuu wa msafara siku hiyo na kuwataka waandishi kwenda   kwa Bwana afya kupata maelezo kwa bwana AFYA HUYO.   Akiulizwa bwana L...

BAJETI YATANGAZWA V2012 V2013

Image
MCL The Citizen Mwanaspoti Nation Monitor Digital Paper East Africa News Ingia Mwanzo Contacts Email Habari Kubwa Fri 15 June 1:17AM   Mwanzo Habari Biashara Michezo Burudani Ajira Uchambuzi Jumapili Makala Picha Tangaza Kipanya RSS Home BOOKMARK THIS PAGE Bajeti  Send to a friend Thursday, 14 June 2012 22:03 0 digg Waziri wa Fedha, Dk William Mgimwa akionyesha begi lililobeba hotuba ya bajeti ya serikali kwa mwaka wa fedha 2012/2013, wakati akielekea kuingia katika ukumbi wa Bunge, mjini Dodoma jana. Picha na Edwin Mjwahuzi Mussa Juma, Dodoma SERIKALI jana ilitangaza Bajeti ya Sh15trilioni kwa mwaka wa fedha 2012/2013 ambayo pamoja na mambo mengine, imelenga kudhibiti mfumuko wa bei kwa kutangaza kutoa vibali vya kuingiza chakula kutoka nje, huku ikiwabana matajiri kwa kuongeza kodi ya bidh...

TAFADHALI MADAKATARI ,VIONGOZI MSIYAPUUZE

Image
MIONGONI mwa habari zilizopo ukurasa wa mbele wa gazeti hili, ni tishio la Chama cha Madaktari Tanzania (MAT) la kufanya mgomo usio na kikomo wiki mbili zijazo, iwapo serikali itashindwa kuyapatia ufumbuzi madai yao ya msingi, ikiwemo nyongeza ya mshahara. Tumeshtushwa na tishio hilo kwa kuwa bado hatujasahau madhara yaliyotokea wakati wa migomo ya Januari na Machi mwaka huu, ambapo watu waliokwenda kwenye hospitali, zahanati na vituo vya afya vya umma kupata matibabu na huduma nyinginezo hawakuzipata. Wapo watu waliopoteza maisha, waliopata vilema vya maisha na athari nyingine nyingi ambazo mpaka hivi sasa serikali imeshindwa kutaja migomo ile iliathiri kwa kiwango gani sekta ya afya. Tunaamini kuwa, tishio hili la madaktari linaweza kufanyiwa kazi kabla ya wiki hizo mbili ili kuepusha hali kama ile tuliyoshuhudia huko nyuma, ambapo pia baadhi ya viongozi na watendaji wa walisimamishwa kazi huku wengine wakipoteza nyadhifa z...