Na Stephen noel –Mpwapwa. JUMLA ya shilingi bilioni moja na na million miatano zilitolewa kama mkopo mbalimbali na Benk Finca tawi la Mpwapwa Mkoa wa Dodoma kwa wateja wake wapatao 2000 kwa mwaka 2013/2014. Kauli hiyo ilibainishwa na meneja wa Finca tawi la Mpwapwa Bw,Edson Joel alipokuwa akiongea na waaandishi wa habari ofisini kwake jana kwa mahojiano maluum. Joel alisema mikopo walioyo itoa ni kwa ajili ya biashara kwa wafanya biashara wakubwa wa kati, na wajasilia mali wadogo wa wilaya ya mpwapwa. Meneja huyo alisema Lengo la Benk hiyo ni kukuza biashara na kuimarisha uchumi kwa jamii na pia kuondoa umaskini kwa watanzania ambao wengi wao hufanya kazi ya kupambana na umaskini lakini hukabaliwa na chanagamoto ya ukosefu wa mikopo na elimu ya ujasilia mali . Amesema wao kama wad...