WAZIRI WA JK APATA PIGO AFIWA NA NDUGU 13 KWA MPIGO,MPWAPWA YAZIZIMA.
Na Stephen Noel-Mpwapwa. WATANZANIA 13( kumi na watatu) wamefariki dunia nchini Uganda walikokuwa wameenda kwenye harusi ya binti yao baada ya gari gari lao kugongana na loli karibu na mto Katonga barabara ya Masaka usiku wa kuamkia tarehe 18septemba mwaka huu . Gari hilo lenye namba T 540 DLC mali ya Gregory Teu lilikuwa likuwarudisha Wanzania wa familia yake, walio wakirudi Tanzania kutokea Uganda, Teu aliyekuwa mbunge wa jimbo la Mpwapwa mstafu na naibu waziri wa Viwanda na Biasharakatika serikali ya awamu ya nne bwana Gregory Teu. Kwa mujibu wa taarifa kutoka katika ofisi ya ubalozi wa Tanzania nchini Uganda zinasema watanzania hao walikwenda nchini humo tangu tarehe 16 septemba mwaka huu kwa ajili ya harusi ya mtoto wake bwana Gregory Teu Mkazi wa Dar es salaam nchini Tanzania aliye olewa nchini Uganda . Aidha taarifa hizo zinasema gari hiyo ilikuwa na abilia 19 ambapo abil...